Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA aliuliza:- Inapotokea wazazi wametengana na mama akaondoka na mtoto na kwenda kuishi naye, lakini tangu wazazi hao watengane mama hatoi nafasi kwa baba kwenda kumtembelea mtoto:- Je, baba ataipata wapi haki hiyo ya kumwona mtoto?

Supplementary Question 1

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Spika, nashukuru Mheshimiwa Naibu Waziri amenijibu vizuri lakini nina maswali ya nyongeza. Ni kweli kabisa aliyosema, nakubali wazazi wote wapate haki kamili ya kumlea mtoto.
Ikiwa mtoto yupo kwa mama aruhusiwe kwenda na kwa baba. Hata hivyo, katika Tanzania yetu wananchi wengi hawampi baba haki ya kumlea mtoto au hata kumwona, je, Serikali inasemaje kuhusiana na suala hili? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Huyu mtoto
kuanzia miaka mitatu hadi saba yupo kwa mama, ikiwa mtoto huyo amefikisha miaka saba, je, baba anayo haki ya moja kwa moja kumlea, kumsomesha na kumuangalia kiafya? Kwa sababu watoto wengi wa Tanzania hawapati
nafasi ya kulelewa na baba. Kwa hiyo, baba apate nafasi ya kulea, baada ya miaka saba apewe mtoto.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Yaani kumtia mwanamke mimba haitoshi kukufanya uitwe baba. Ili kuwa baba kamili, pindi unapompa mimba mwanamke unapaswa kwanza kuitunza
mimba yenyewe, lakini baada ya hapo kumtunza mtoto baada ya kuzaliwa, muwe mnaishi pamoja ama hamuishi pamoja na huyo mwanamke. Hilo ni jukumu la kwanza unapokuwa mwanaume na imetokea umempa mimba mwanamke. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kama kuna mgogoro wowote ule unaoweza kutokea katika mchakato huu kuna taratibu za kufuatwa. Moja ya taratibu ni za kimila ambapo yanaweza yakatokea mashauriano ya kimila kwenye jamii kati ya upande wa baba na upande wa mama na
wakaelewana kimila na kuna gharama za kutoa. Kwa mfano, kwa Wasukuma kuna ngwegwe na nafahamu kwenye makabila mengine pia kuna taratibu za kufuata. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kama ikishindikana kimila ndiyo unafuata huo mchakato wa kisheria niliousema ambapo utapaswa kwanza kumpa haki mama kumlea mtoto mpaka miaka saba ifike na katika kipindi hiki cha miaka saba unapaswa kuwa umemtunza yule mama. Pale mwanzoni
kama hukumuoa huyo mwanamke unapaswa
ukajitambulishe rasmi kwamba wewe unahusika na ile mimba, siyo umeikataa mimba halafu mtoto akizaliwa anafanana na wewe unasema mtoto ni wa kwako, hapana! (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwanza kwa mujibu wa sheria unapaswa ama ufuate taratibu za kimila ujitambulishe kwamba wewe ndiye uliyetia mimba, uilee mimba na mwisho wa siku umlee mtoto au kwa taratibu za kisheria ujitambulishe mahakamani kwamba wewe ndiye umetia mimba na utailea. Sasa ikifika ile miaka saba una haki ya kudai mtoto. Nadhani Mheshimiwa Meisuria amenielewa.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, nataka kuongezea hiyo sehemu ya pili.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto Na.21 ya mwaka 2009, presumption ni kwamba mtoto anatakiwa akae na mama in the best interest of the child lakini akifika miaka saba sheria inasema in the opinion of the court anaweza akakaa na mzazi yeyote pale mahakama
itakapojiridhisha kwamba mtoto huyu atapata matunzo na malezi mazuri.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimtoe wasiwasi
Mheshimiwa Bhagwanji kwamba kama mtoto amefikisha miaka saba siyo lazima akae na mama, mahakama itapima na kuona in the best interest of the child mtoto huyu atapata malezi mazuri wapi, kwa baba au kwa mama.

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA aliuliza:- Inapotokea wazazi wametengana na mama akaondoka na mtoto na kwenda kuishi naye, lakini tangu wazazi hao watengane mama hatoi nafasi kwa baba kwenda kumtembelea mtoto:- Je, baba ataipata wapi haki hiyo ya kumwona mtoto?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Spika,
ahsante sana. Nami naomba nimuulize Naibu Waziri swali
dogo la nyongeza. Kwa kuwa ongezeko la watoto wa
mitaani linachangiwa na akinababa kukataa mimba na
kukataa familia zao. Je, Serikali inaweza kusema mpaka sasa
hivi ni akinababa wangapi wameshatiwa hatiani na
kufunguliwa mashtaka ili kutunza familia zao?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII,
JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, kwanza hatuna takwimu sahihi za watu waliochukuliwa hatua kwa kukataa mimba. Hata hivyo, nimhakikishie tu kwamba tuko makini katika kufuatilia kesi za namna hiyo ili kuweza kuchukua hatua pindi inapojitokeza.

Name

Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA aliuliza:- Inapotokea wazazi wametengana na mama akaondoka na mtoto na kwenda kuishi naye, lakini tangu wazazi hao watengane mama hatoi nafasi kwa baba kwenda kumtembelea mtoto:- Je, baba ataipata wapi haki hiyo ya kumwona mtoto?

Supplementary Question 3

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Nami kwanza kabla ya yote niungane na Waheshimiwa Wabunge wote kwa kumtakia afya njema Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na
familia yake kwa jinsi alivyotuongoza kipindi chake. Pamoja na hayo, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Basi nitauliza swali moja la nyongeza lenye kifungu (a) na (b).
Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri na Waziri wake kwa kuwa makini wakati wa kujibu suala hili lakini kuna kadhia kama hii imetokea kwa baba kufariki na watoto kubaki na huyu mtu akaenda kulalamika Ustawi wa Jamii nao wakapendekeza kwamba
watoto hawa ikifika muda waende kwa babu yao na ukitazama chimbuko la hawa watoto ni babu. Leo kwa nini babu ananyimwa haki yake ya kuwasomesha watoto wale? La kushangaza, baadaye bibi huyo akakimbilia mahakamani
nayo ikaamua kuwa shule zikifungwa wakatembelee tu watoto asiweze kuwachukua. Haki ya mtoto iko wapi hapo katika vifungu ulivyotaja 21 na 7?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, Sheria ya Mtoto iko wazi katika kifungu cha 37 ambacho kinahusu custody of the child. Katika kifungu hicho utaratibu unawekwa kwamba pale mtoto anapokuwa amefika umri wa miaka saba utaratibu unabadilika badala ya kubaki tu kwamba atakuwa chini ya usimamizi wa mama yake sasa mahakama inaweza ikaamua mtoto ama aende kwa baba au kwa mama kwa kuzingatia mahali ambapo huyo mtoto atapata malezi bora.
Mheshimiwa Spika, lakini kama imetokea sasa mzazi ambaye ni baba amefariki, maana yake mzazi anayebaki automatically ni yule mmoja kwa sababu mtoto ni wa wazazi wawili. Kwa hiyo, kama mama yupo maana yake naturally tu mama anapata haki ya kumlea yule mtoto siyo tena kwa
babu mzaa baba, hapana! Kama mama yupo lakini baba amefariki haki inabaki kwa mama.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kama inatokea
kwamba mama anaonekana hana uwezo wa kumlea yule mtoto ama mtoto hapati haki ama mtoto anafanyiwa vitendo vya ukatili kwa namna yoyote ile na wazazi na jamii ipo, basi hao wazazi kama babu wanaweza wakaenda mahakamani kwenda kushtaki na shauri hili likajadiliwa pale
na hatimaye mahakama itaamua kutafsiri kifungu hicho in the best interest of the child.