Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Joyce Bitta Sokombi
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JOYCE B. SOKOMBI aliuliza:- Barabara ya kutoka Tarime kwenda Serengeti ni barabara muhimu sana kwa wakazi wa Wilaya hizo na kwa maisha yao ya kila siku:- Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 1
MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Majibu ya Waziri hayajaniridhisha. Barabara hii ina umuhimu mkubwa kwani hutumiwa na watalii wengi wanaotoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta kuja Serengeti National Park. Je, hamuoni kwamba tunapoteza watalii wengi kutokana na ubovu wa barabara hii?
Mheshimiwa Spika, kwa taarifa niliyoipata ni kwamba barabara hii ilikuwa iishe 2017, lakini nashangaa kwa majibu ya Waziri kwamba barabara hii inaisha 2018. Sasa nataka
nijue barabara hii inaisha 2017 au 2018? Je, upembuzi yakinifu unaisha 2017 au 2018? Je, kwenye bajeti 2017 barabara hii imetengewa bajeti?
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii unaisha mwaka 2018 kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi. Nimhakikishie Mheshimiwa Sokombi kwamba hicho tunachokisema ndicho tutakachokitekeleza na umuhimu wa barabara hii
umetokana na hao watalii wengi ambao wameanza kuonekana. Tunataka barabara hii pamoja na hiyo nyingine, kama unavyofahamu tunajenga barabara nyingine ya kutoka Sanzatu, zote hizi tutazijenga kwa ajili ya kufungua utalii. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge hawa watalii mara baada ya kukamilisha kujenga barabara hizi wataongezeka.
Name
Esther Nicholus Matiko
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JOYCE B. SOKOMBI aliuliza:- Barabara ya kutoka Tarime kwenda Serengeti ni barabara muhimu sana kwa wakazi wa Wilaya hizo na kwa maisha yao ya kila siku:- Je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 2
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika,
nakushukuru. Kwa kweli niendelee kusikitika kwamba Serikali inashindwa kuona barabara ambazo zinaweza zikaongeza chachu ya ukuaji wa uchumi kwenye nchi yetu kupitia utalii.
Mheshimiwa Spika, ningependa kujua ni lini Barabara ya Tarime – Nata kwa maana ya kwenda Mugumu itakamilika kwa kiwango cha lami? Mheshimiwa Naibu Waziri anatueleza
kwamba upembuzi yakinifu unakamilika 2018, watalii wengi wanaotoka Kenya wanapita Tarime wanaenda Serengeti, tukiboresha ile barabara kwa kiwango cha lami tutakwenda kukuza uchumi wetu kwa sababu watalii wengi watapita
kwa sababu barabara inapitika. Ni lini sasa Serikali itajicommit, isiseme leo itamaliza upembuzi yakinifu 2018, ione kuna uhitaji wa haraka sana wa kujenga barabara ya Tarime – Mugumu na iweze kumalizika ndani ya mwaka mmoja kama ikiwezekana tuweze kukuza uchumi wa nchi yetu? (Makofi)
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, katika ujenzi wa barabara tuna hatua tatu muhimu na hatua hizi ni lazima zikamilike. Hatua ya kwanza ni upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Baada ya Serikali kuiona barabara hii kwamba ina umuhimu na inaongeza mapato yetu katika utalii imeamua kuianza hiyo kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kazi hiyo itakamilika mwaka 2018.
Mheshimiwa Spika, baada ya kazi hiyo kukamilika,
hatua ya pili itakayofuata ni kutafuta fedha za ujenzi wa barabara hiyo. Huwezi ukajenga barabara bila fedha. Kwa hiyo, Serikali itatafuta fedha ili tuanze kujenga barabara hiyo.
Tukishapata fedha tutatangaza tumpate mkandarasi wa kuanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved