Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- Wakazi wanaoishi katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro wamekatazwa kulima kwenye maeneo wanayoishi kwa mujibu wa sheria hali iliyochangia wakazi wengi katika eneo hilo ambao ni wafugaji kukabiliwa na njaa pamoja na umaskini mkubwa wa kipato:- Je, ni lini Serikali itarekebisha Sheria ya Mamlaka ya Hifadhi (Ngorongoro Conservation Area Act), 1959 Revised Edition, 2002) ili wananchi wa maeneo haya wapate maeneo kwa ajili ya shughuli zao za kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika,
nakushukuru na nashukuru pia kwa majibu kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa majibu ya
Mheshimiwa Waziri ni kwamba Serikali iko mbioni kufanya marekebisho ya sheria hii. Napenda kufahamu ni lini sasa Serikali itafanya marekebisho haya na kutenga eneo mahsusi
kwa ajili ya wakazi wanaoishi katika eneo hili la Bonde la Ngorongoro ili waweze kujihusisha na kilimo kwa sababu sio mazao yote yanayoharibu mazingira?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa
ukosefu wa maji kwa mifugo hususan msongamano ndani ya eneo dogo na kuharibu mazingira na kwa kuwa hifadhi hii bado ina maeneo ambayo yanaweza kutengwa kwa ajili
ya mifugo iweze kupata maji na Mheshimiwa Waziri Mkuu alishaiagiza Wizara hii kuhakikisha kwamba inatenga maeneo hayo ili wafugaji waweze kupata maeneo hayo kwa ajili ya
kunyweshea mifugo yao. Je, ni lini Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro itaweka maeneo haya maji na wananchi wanaoishi katika Bonde hili la Hifadhi ya Ngorongoro waweze kunywesha mifugo yao katika maeneo hayo na siyo kwenda kuharibu mazingira kama ambavyo sasa wanavyodaiwa
kufanya?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, katika swali lake la kwanza anataka kujua ni lini mabadiliko ya sheria kama ambavyo tumejibu katika swali la msingi yanafanyika? Mchakato wa mabadiliko ya sheria
unatanguliwa na shughuli kadhaa za kitaalam ambapo kutokana na shughuli hizo za kitaalam ndipo mapendekezo ya mabadiliko ya sheria yanapelekwa katika hatua mbalimbali za Serikali ili hatimaye mabadiliko ya sheria yale yaweze kuwa na tija kwa sababu yatakuwa yana-input ya kitalaam.
Mheshimiwa Spika, hivi ninavyozungumza, katika
kipindi cha wiki moja kikosi maalum cha watu wanaotakiwa kufanya sensa kama jambo la kwanza kabisa la kulifanya ili kujua ukweli wa hali halisi ya Ngorongoro kitaanza kazi. Kazi ambayo itafanyika kwa muda wiki moja. Hii inatokana na ukweli kwamba mwaka 1959 wakati Ngorongoro inatengwa kama eneo la hifadhi kulikuwa na jumla ya wakazi 8000 ndani ya eneo lile. Kufikia mwaka 2013 tayari kulikuwa na wakazi jumla ya 87,851, hii ni takribani wastani wa ongezeko la wakazi 1500 kila mwaka.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, changamoto hii ni
kubwa na hivyo hata mabadiliko ya sheria yanatakiwayaangalie uhalisia ambao utakuwa ni uhalisia wa kisayansi. Kwa hiyo, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, ndani ya kipindi cha mwaka wa fedha ujao tutakuwa tumeanza na kukamilisha utaratibu wa mabadiliko ya sheria
inayohusika.
Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili
anazungumzia juu ya suala la ukosefu wa maji na ambalo lina maagizo mahsusi kutoka kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Ni kweli, kulikuwa na maagizo ambayo yalikuwa yanataka kutatua changamoto ya maji katika kipindi cha mpito wakati ambapo tunasubiri mabadiliko yale ya sheria ambayo yataweka misingi ambayo itakuwa ni ya kudumu.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mpito suala la maji kwa ajili ya mifugo linashughulikiwa kwa kujenga mabwawa katika maeneo ambayo yanaonekana kwamba uwepo wa mabwawa katika maeneo hayo utatatua changamoto ya mahitaji ya maji kwa mifugo. Mamlaka ya
Hifadhi ya Ngorongoro imetenga fedha katika bajeti hii na Waheshimiwa Wabunge mkiipitisha, basi tunaweza kutatua tatizo hili kwa namna ambayo itakuwa ni toshelezi. Kwa hiyo,
namuomba Mheshimiwa Mbunge afanye subira, asubiri Bajeti ya Serikali, bajeti ya Wizara hii itakapopita, hasa kwa upande ule wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro tutakuwa tumeweza kuweka tengeo la kuweza kutekeleza agizo
la Mheshimiwa Waziri Mkuu ipasavyo.

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- Wakazi wanaoishi katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro wamekatazwa kulima kwenye maeneo wanayoishi kwa mujibu wa sheria hali iliyochangia wakazi wengi katika eneo hilo ambao ni wafugaji kukabiliwa na njaa pamoja na umaskini mkubwa wa kipato:- Je, ni lini Serikali itarekebisha Sheria ya Mamlaka ya Hifadhi (Ngorongoro Conservation Area Act), 1959 Revised Edition, 2002) ili wananchi wa maeneo haya wapate maeneo kwa ajili ya shughuli zao za kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Spika,
nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuuliza swali moja tu la nyongeza. Tatizo la Hifadhi ya Ngorongoro linafanana sana na lile tatizo la Hifadhi ya Swagaswaga ambalo linaunganisha Wilaya za Kondoa na Chemba. Kumekuwa
na matatizo watu wengi wamezuiwa kulima na
nilishakwenda mimi na Mheshimiwa Naibu Waziri katika eneo hilo na akatoa maagizo kwamba, ufanyike utaratibu wa kuweka mipaka upya, lakini jambo hili halijafanyika hadi sasa. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kuweka mipaka ili
wananchi wa Lahoda, Kisande, Iyoli pamoja na Handa waweze kuondokana na tatizo hili?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa hii. Ni kweli nilifanya ziara katika eneo hili ambalo linahusika na hifadhi yetu ya Swagaswaga na niliambata na Mheshimiwa Mbunge na ni kweli niliacha maagizo kama anavyosema. Pia siyo tu agizo, tuliendelea na utaratibu ule wa kuunda kikosi kazi ambacho kilihusisha Wizara nne na ambacho kimekuwa kikiendelea na kazi yake
kwa muda wa miezi michache iliyopita. Sasa hivi kamati ile imeshaandaa mapendekezo ya awali ambayo yamekabidhiwa tayari kwa Kamati ya Makatibu Wakuu, baada ya pale yanaenda kukabidhiwa kwa Baraza la Mawaziri, baadaye kwenye ngazi za juu, ili tuweze kupata
mwelekeo zaidi wa kwamba nini kifanyike ili kuweza kukamilisha utaratibu wa kuweka mipaka.
Mheshimiwa Spika, lakini kwa maana ya maeneo yale ambayo hayana migogoro kabisa, suala la uwekaji wa mipaka limekuwa likiendelea na hifadhi kadhaa tayari zimeshakamilisha utaratibu huo. Mheshimiwa Mbunge akiniona baada ya hapa tutaweza kuangalia kwenye orodha kama eneo lake limepangiwa lini kukamilisha utaratibu wa
kuweza kuweka mipaka.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- Wakazi wanaoishi katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro wamekatazwa kulima kwenye maeneo wanayoishi kwa mujibu wa sheria hali iliyochangia wakazi wengi katika eneo hilo ambao ni wafugaji kukabiliwa na njaa pamoja na umaskini mkubwa wa kipato:- Je, ni lini Serikali itarekebisha Sheria ya Mamlaka ya Hifadhi (Ngorongoro Conservation Area Act), 1959 Revised Edition, 2002) ili wananchi wa maeneo haya wapate maeneo kwa ajili ya shughuli zao za kilimo na ufugaji?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro wamekuwa wakikumbwa na changamoto kubwa sana kwa sababu wanaishi katika eneo la hifadhi. Hata hivyo kumekuwa na ahadi nyingi za Serikali
za kumaliza hiyo changamoto lakini hakuna mafanikio na mpaka leo wananchi wale wanaishi tu kwa matumaini. Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba wamekataza mifugo isiingie crater lakini kuna changamoto ya upatikanaji wa maji. Kumeshawahi kutengwa takribani shilingi bilioni tano na zimetumika, wamejenga ranchi kwa ajili ya kuhifadhi mifugo isiingie crater na haitumiki. Je, ni kwa nini ranchi imejengwa kwa gharama kubwa halafu haitumiki mpaka sasa?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, changamoto za Hifadhi ya Ngorongoro ni kubwa na nyingi. Hata hivyo, napenda ieleweke kwamba katika kusimamia uhifadhi ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro jambo hili sisi wote kwa pamoja tunatakiwa tuzingatie ukweli kwamba maslahi ya mtu mmoja mmoja yatazingatiwa, maslahi ya makundi yatazingatiwa lakini mwisho wa siku maslahi ya Taifa yanayotokana na kuhifadhi eneo lile ndiyo
yatakayopewa kipaumbele.
Mheshimiwa Spika, ni kweli, hapa na pale katika
kipindi chote cha uwepo wa sheria hii tunayoizungumzia ya mwaka 1959 mengi yametokea. Yako yale ambayo Serikali ilisema itatekeleza, tumetekeleza kikamilifu, yako yale ambayo bado Serikali inaendelea kuyatekeleza, lakini tumesema msingi wa kuweza kushughulikia tatizo hili vizuri na kikamilifu ni kufanya marekebisho ya sheria. Kwa sababu kufanya kitu chochote kile nje ya sheria kwa ajili tu ya kutaka
kujibu hoja za makundi au za mtu mmoja mmoja ni jambo ambalo halitaweza kutufanya tukafanikiwa.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nashauri Mheshimiwa Mbunge na wadau wengine wote na Taifa kwa ujumla tufanye subira. Tusubiri mabadiliko ya sheria ambayo yataweka misingi sasa ya kuweza kutatua changamoto hizi
kwa namna ambayo itakuwa ni endelevu.