Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Kuna mahitaji makubwa ya umeme katika Jimbo la Singida Mjini hususani katika kata za pembezoni kama vile Kisaki, Mtama, Mtipa, Mwankoko, Uhamaka, Unyambwa, Unyamikombi na Unyianga. (a) Je, Serikali ina mpango gani kuvipatia umeme vijiji katika mwaka huu wa fedha? (b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutumia rasilimali ya nguvu ya upepo iliyopo Singida ili kuongeza nishati ya umeme?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kumshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Singida Mjini imejaaliwa kuwa na rasilimali ya vyanzo vya umeme kwa maana ya upepo na jua na yako makampuni tayari yamekwishajitokeza kwa ajili ya kuzalisha umeme huo. Sasa na sisi wananchi wa Jimbo la Singida Mjini tumejitokeza kwa maana ya kutoa maeneo yetu kwa ajili ya uzalishaji. Serikali sasa ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba umeme huo unazalishwa ili Singida Mjini iweze kupata viwanda vya kutosha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Singida Mjini kunapita umeme wa kilovoti 40 kuelekea Shinyanga na Namanga na wananchi tayari wametoa maeneo yao kwa ajili ya kupisha mradi huo na wako ambao wameshalipwa fidia na wengine hawajalipwa fidia. Serikali inatoa tamko gani sasa kuhakikisha kwamba wananchi wote wanalipwa fidia kwa ajili ya kupisha umeme huo? Ahsante sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa, Serikali ina mpango mahususi wa kuendeleza wawekezaji binafsi katika umeme mbadala hasa katika maeneo ya Singida ambako kuna umeme wa upepo. Hata hivyo, mkakati wa Serikali wa kwanza, Serikali imetenga kupitia mradi wake wa REA shilingi milioni 42 kwa ajili ya kuendeleza wawekezaji binafsi watakaofanya katika uzalishaji wa umeme pamoja na mambo ya miradi ya maji. Kwa hiyo, wananchi wa Singida watapata pesa hizi kupitia mradi wa REA ambapo watawezeshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mkakati mwingine badala ya kupitia mradi wake umeshafadhili sasa, nikizungumzia kwa nchi nzima miradi ya Lukonda kule Njombe pamoja na Ndoya kule Mbinga kama wajasiriamali wa Kitanzania ambao wanawezeshwa kupitia miradi ya Serikali, miradi ya REA. Kwa hiyo, miradi ya Serikali kupitia miradi ya REA kutoa mahususi kwa ajili ya kuendekeza wawekezaji. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Sima na kama kuna wawekezaji wengine kule Singida Mheshimiwa Sima basi walete wataalam wetu watashirikiana na watu wa REA ili waweze kushirikiana zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili kuhusiana na mkakati wa Serikali kulipa fidia kwenye Mradi wa backbone wa kilovoti 400. Kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Sima alivyoshirikiana na Serikali mpaka wananchi takriban 200 wakalipwa fidia awamu ya kwanza. Awamu ya pili nimhakikishie Mheshimiwa Sima, hivi sasa vijiji vyake 13 ambavyo vinaingia kwenye mradi ule vitalipwa fidia jumla ya shilingi milioni 722.7, malipo yataanza mwezi Februari mwaka huu na yatakamilika mwezi Machi na nimhakikishie kwamba vijiji vyake vya Misuna ambavyo vilipitiwa na umeme pamoja na Mtipa pamoja na Kisaki pia vitalipwa fidia kwa utaratibu huo.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Kuna mahitaji makubwa ya umeme katika Jimbo la Singida Mjini hususani katika kata za pembezoni kama vile Kisaki, Mtama, Mtipa, Mwankoko, Uhamaka, Unyambwa, Unyamikombi na Unyianga. (a) Je, Serikali ina mpango gani kuvipatia umeme vijiji katika mwaka huu wa fedha? (b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutumia rasilimali ya nguvu ya upepo iliyopo Singida ili kuongeza nishati ya umeme?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na pamoja na kazi nzuri ambayo Wizara hii inafanya, naomba niulize swali dogo tu la nyongeza. Niliwahi kuuliza hili swali kwamba kwa kuwa Wilaya ya Kilolo ndiyo wilaya pekee ambayo maji mengi yanayojaza Kihansi yanatoka kule ambayo ndiyo yanasaidia kupelekea kuleta umeme nchi hii. Je, Kilolo inanufaikaje sasa? Naomba kwa nafasi hii atueleze hapa wananchi wa Kilolo watanufaika vipi ili kuhakikisha wanapata umeme.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa eneo la Kilolo linatupatia maporomoko ya maji ambayo yanatusaidia sana kuingiza kwenye Gridi ya Taifa. Lakini wananchi wa Kilolo pamoja na hasa wananchi wa Kihesa Mgagao watanufaika sana na umeme huu na nitaje tu Mheshimiwa Mwamoto, hivi sasa katika Mkoa wa Iringa, REA Awamu ya Tatu imeshaingia na eneo mojawapo ambalo linapelekewa umeme ni pamoja na Kihesa Mgagao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wananchi wa Kilolo wataendelea kunufaika na miradi ya umeme.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Kuna mahitaji makubwa ya umeme katika Jimbo la Singida Mjini hususani katika kata za pembezoni kama vile Kisaki, Mtama, Mtipa, Mwankoko, Uhamaka, Unyambwa, Unyamikombi na Unyianga. (a) Je, Serikali ina mpango gani kuvipatia umeme vijiji katika mwaka huu wa fedha? (b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutumia rasilimali ya nguvu ya upepo iliyopo Singida ili kuongeza nishati ya umeme?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Jimbo la Tarime Mjini lina kata nane na kati ya kata nane, kata nne ziko pembezoni na hazina umeme kabisa na kata mbili zina umeme kwa asilimia chache. Ningependa kujua commitment ya Serikali ya kuhakikisha kwamba wananchi wa Jimbo la Tarime Mjini wanapata umeme kwa asilimia zaidi ya 90.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Esther, tumeshirikiana naye sana kwenye mradi wa REA Awamu ya Pili na ni kweli kuna kata nne na kata nyingine mbili ambazo hazijaguswa kabisa. Hata hivyo, nimhakikishie Mheshimiwa Esther kwamba Jimbo lako pamoja na Mkoa wa Mara tumeshaanza kutekeleza Mradi wa REA Awamu ya Tatu wa desification. Hapa ninapozungumza wiki ijayo mkandarasi ata-report kwake ili amwelekeze maeneo mahususi. Kwa hiyo, kata zake nne na zile tatu ambazo anazungumza Mheshimiwa Mbunge zitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA Awamu ya Tatu unaoanza mwezi wa Tatu na kuendelea.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Kuna mahitaji makubwa ya umeme katika Jimbo la Singida Mjini hususani katika kata za pembezoni kama vile Kisaki, Mtama, Mtipa, Mwankoko, Uhamaka, Unyambwa, Unyamikombi na Unyianga. (a) Je, Serikali ina mpango gani kuvipatia umeme vijiji katika mwaka huu wa fedha? (b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutumia rasilimali ya nguvu ya upepo iliyopo Singida ili kuongeza nishati ya umeme?

Supplementary Question 4

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri akijibu swali mojawapo hapa Bungeni kuhusu mradi wa umeme wa upepo Singida alisema kwamba Serikali inakamilisha mkataba na taratibu za kusaini kati ya Kampuni ya Wind East-Africa na kwamba mwezi Februari mradi huo utaanza. Naomba atusaidie, je, maneno yale ni kweli au bado? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichowaeleza ni kweli kwanza, lakini cha pili nifafanue tu kwamba mradi wa REA unaokwenda kuendelea umeshaanza na mpaka tarehe 31 mwezi Machi, wakandarasi watakuwa wameshaingia mikoa yote kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa REA unaoendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa upande wa umeme wa upepo kule Singida nimesema mradi wa Wind East-Africa pamoja na Geo Wind wanakamilisha taratibu za kimikataba na kufikia mwezi Juni ndiyo wataanza rasmi. Kwa wanaoanza Februari na mwezi Machi ni miradi ya REA na ile miradi ya upepo itaanza kuanzia mwezi Juni na kuendelea.