Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Jimbo la Mtera katika kijiji cha Mvumi Misheni aliahidi kutujengea barabara ya lami kutoka Mlowa barabarani hadi Mvumi Misheni kwenye Hospital Teule ya Wilaya ya Chamwino. Pia Rais wa Awamu ya Tano katika kampeni zake alipofika Mvumi Misheni alisisitiza kuwa barabara hiyo itajengwa haraka iwezekanavyo. Je, ujenzi huo utaanza lini?

Supplementary Question 1

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake. Hata hivyo napenda niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, punde wakati akijibu maswali leo asubuhi, amesema barabara ili ijengwe kwa kiwango cha lami inapitia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina; na kwa muda aliouonyesha ni kama vile kila kitendo kinachukua zaidi ya miaka miwili.
Je, kwa miaka iliyobaki kabla hata ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina haujaanza kufanyika, Waziri anawahakikishiaje wananchi wa Jimbo la Mtera kwamba barabara hiyo itakamilika mwaka 2020?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema barabara hiyo itaendelea kujengwa kwa kiwango cha changarawe na sasa hivi barabara hiyo bahati nzuri inajengwa. Je, Naibu Waziri yuko tayari kuongozana na mimi ili akaone hicho kiwango cha changarawe anachokisema kwamba kinajengwa badala ya kiwango cha changarawe naona wanajenga kwa kiwango cha tope, yuko tayari twende tukaone site? Ahsante

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Lusinde kwa kazi kubwa anayofanya ya kuwatetea wananchi wa Mtera.
Mimi nimhakikishie, Serikali hii iko pamoja naye na hicho anachokidhania kwamba inachukua zaidi ya miaka minne kufanya hizi kazi mbili, kwanza hii barabara siyo ndefu sana kwa hiyo, haitaweza kuchukua miaka minne. Ni barabara fupi na tunaweza tukaingia kwenye hatua ya design and build, kwa maana ya unafanya yote kwa wakati mmoja. Nikuhakikishie tu ahadi yetu kwenye hilo tutaitekeleza kwanza hii barabara ni ndogo sana. Siamini kama wewe unafahamu ni barabara fupi inayohitaji gharama siyo kubwa sana kwa hiyo, tutaikamilisha kwa wakati kabla ya kipindi hiki cha miaka mitano hakijaisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, kwa kweli naomba kwa heshima kabisa ikiwezekana hata leo jioni hebu twende tukalione hili ili tuweze kulishughulikia kwa haraka. Kama ni kweli ni tope siyo sahihi kabisa.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Jimbo la Mtera katika kijiji cha Mvumi Misheni aliahidi kutujengea barabara ya lami kutoka Mlowa barabarani hadi Mvumi Misheni kwenye Hospital Teule ya Wilaya ya Chamwino. Pia Rais wa Awamu ya Tano katika kampeni zake alipofika Mvumi Misheni alisisitiza kuwa barabara hiyo itajengwa haraka iwezekanavyo. Je, ujenzi huo utaanza lini?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba nichukue nafasi hii kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri hayakugusa ahadi ya Mheshimiwa Rais aliyoitoa katika barabara ya Mji wa Mbulu na ahadi hiyo iliwagusa wananchi wa Mji wa Mbulu wakati wa uchaguzi. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anatuambia nini kuhusu utekelezaji wa ahadi hii ambayo imesahaulika, hadi sasa mwaka mmoja umeisha baada ya uchaguzi?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii hatujaisahau. Tulichokifanya katika mwaka wa kwanza ni kutekeleza barabara zile ambazo wakandarasi walikuwa wameondoka site kwa kutolipwa madeni yao, na unaona kwamba sasa hivi tumefanya kazi kubwa sana na barabara nyingi zinaanza kukamilika baada ya kulipa madeni ambayo walikuwa wanayadai. Nimhakikishie, kuanzia bajeti ijayo, tunaanza sasa, kwanza kukamilisha zile barabara zilizobakia za nyuma ili tusiwe tunadaiwa daiwa riba pamoja na usumbufu, lakini vilevile tuanze sasa kwa kiwango chochote tutakachoweza kwa mwaka ujao wa fedha barabara zile mpya tulizoziahidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie katika safari yangu ambayo Mheshimiwa Massay tumekubaliana tutafika mpaka Mbulu na ninadhani nitalala Mbulu Mjini ili tuliangalie hilo kwa undani pamoja na hayo matatizo matatu makubwa ambayo nimeyaongea kabla.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Jimbo la Mtera katika kijiji cha Mvumi Misheni aliahidi kutujengea barabara ya lami kutoka Mlowa barabarani hadi Mvumi Misheni kwenye Hospital Teule ya Wilaya ya Chamwino. Pia Rais wa Awamu ya Tano katika kampeni zake alipofika Mvumi Misheni alisisitiza kuwa barabara hiyo itajengwa haraka iwezekanavyo. Je, ujenzi huo utaanza lini?

Supplementary Question 3

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shida ya barabara ya Jimbo la Mtera inafanana sana na shida ya barabara ya Jimbo la Ukonga. Barabara ya kutoka Banana - Kitunda - Kivule - Msongora ni barabara ambayo imeahidiwa kwa miaka ishiri ambapo Mheshimiwa Rais wa sasa alikuwa Waziri kwenye eneo hilo aliahidi na haikutekelezwa, miaka kumi ya Mheshimiwa Kikwete iliahidiwa haikutekelezwa. Kwenye bajeti ya mwaka jana ilionyesha kuwa TANROADS wanasaida kujenga angalau kilometa 3.2.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapozungumza hapa walishaenda wakafanya survey wakapata na mkandarasi yupo anasubiri. Shida iliyopo ni kwamba fedha hazipo na ieleweke tu kwamba barabara hii ndiyo inayohudumia Kata ya Kitunda, Kata ya Mzinga, Kata ya Kivule, Kata ya Msongora na mojawapo ya shida ya barabara hii imeleta madhara makubwa kwa sababu shule zilizoongoza kwa kufanya vibaya, shule ya msingi Kitonga ipo eneo hili na shida mojawapo ya watoto wale kufeli ni kwamba wanatoka mjini kati, wanaenda kule hakuna usafiri wanatembea kwa miguu, kwa hiyo wanatega shule na wamefeli ndiyo maana wakaomba walimu wasiadhibiwe kwa sababu hii.
Sasa naomba nimuulize Mhesimiwa Naibu Waziri ni lini baabara hii itaweza kutengenezwa kwa kiwango cha lami au hata changarawe ili magari yatoke Banana mpaka Msongora – Kitonga, walimu na watumishi wengine, wanafunzi waende shuleni kwa uhakika kupunguza shida iliyopo sasa? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waitara anafahamu kwamba tatizo hili aliliwasilisha kwangu vilevile kupitia kwa Afisa Elimu Sekondari ambaye naye alilalamika sana kuhusiana na kufeli shule zake, kuwa za mwisho katika Mkoa wa Dar es Salaam; na alisema kwamba mchango mmojawapo ni matatizo ya hii barabara na wanafunzi wanapangiwa kule mbali kwa sababu shule za karibu huwa zinajaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimuhakikishie, Serikali imelichukua hili, tutalishughulikia ili turekebishe haya. Naomba unipe fursa niwasiliane na TANROADS Mkoa wa Pwani nipate taarifa zao za karibuni maana yake nilishawaambia kuhusu hili tatizo baada ya kupata hiyo taarifa kutoka kwa Afisa Elimu wa Sekondari wa Wilaya ya Ilala, na baada ya kujua sasa alifanya nini baada ya malalamiko yale nitakuja nikuambie hatua ipi tunaichukua.

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE aliuliza:- Rais wa Awamu ya Nne alipotembelea Jimbo la Mtera katika kijiji cha Mvumi Misheni aliahidi kutujengea barabara ya lami kutoka Mlowa barabarani hadi Mvumi Misheni kwenye Hospital Teule ya Wilaya ya Chamwino. Pia Rais wa Awamu ya Tano katika kampeni zake alipofika Mvumi Misheni alisisitiza kuwa barabara hiyo itajengwa haraka iwezekanavyo. Je, ujenzi huo utaanza lini?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru kwa kunipa nafasi nilulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kutoka Mtwara hadi Newala – Masasi kipande cha kutoka Mtwara hadi Nnivata tender ilishatangazwa, na kwa mujibu wa maelezo ya Meneja TANROADS Mtwara ni kwamba mkataba ulisainiwa tarehe 16 Januari, lakini ukimuuliza Waziri anasema hajui, Naibu Waziri hajui na wengine wanakwambia mara mkataba uko kwa Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali. Sasa nilitaka kujua mkataba umesainiwa au haujasainiwa na inachukua muda gani kujua ndani ya ofisi hiyo hiyo inamchukua Waziri muda gani kupata taarifa?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Ghasia na kupitia kwake na wananchi wake wa Mtwara Vijijini kwamba Serikali kama ambavyo imepanga kwenye bajeti ya kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami katika mwaka huu wa fedha itatekeleza ahadi hiyo na tofauti ambayo ameieleza kati ya tunachokifahamu sisi na anachoambiwa na TANROADS Mkoa kule kimetokana na sintofahamu iliyotokea kwa mkandarasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kila kitu kukamilika na document kuwa tayari kusainiwa kuna kipengele ambacho ilibidi Mwanasheria Mkuu wa Serikali akikamilishe kukiangalia na kukiweka sawa kabla mkataba haujasainiwa.
Kwa hiyo, ninavyofahamu mimi na kwa namna Mheshimiwa Waziri wangu alivyonieleza na namna nilivyoambiwa na TANROADS pamoja na Katibu Mkuu mkataba huu utasainiwa muda wowote katika wiki hii kwa sababu Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu namshukuru ametusaida kulitatua lile tatizo ambalo lilikuwa linatusumbua, kwa hiyo mkataba utasainiwa muda wowote kati ya wiki hii na wiki ijayo. Kikubwa na cha msingi fedha tumetenga, tuko tayari kuanza ujenzi, process za kumpata mkandarasi wa kujenga tayari sasa zimefikia mwisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naomba Mheshimiwa Ghasia pamoja na mengi anayotushauri kwenye hili atuvumilie kidogo, lakini kubwa ni kwamba zile fedha tulizozitenga shilingi bilioni 21 zitatumika katika mwaka wa fedha kuanza ujenzi.