Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:- Ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete ya ujenzi wa daraja la Kamsamba–Kilyamatundu bado haijatekelezwa tangu mwaka 2009. Je, ni upi mpango wa Serikali ya Awamu ya Tano kukamilisha ujenzi wa daraja hilo?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Hili swali la ujenzi wa daraja ninaliuliza leo ni mwaka wa saba mfululizo nikiwa ndani ya Bunge hili Tukufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada ambazo nimeanza kuziona ambazo zinaweza kuzaa matunda hivi karibuni, ni kwamba wametangaza tender tarehe 11.01.2017; sasa ninachotaka kujua ni kwamba, ili tupunguze maneno maneno mengi, je, Serikali itakamilisha lini utaratibu wa tenda ili ujenzi huo uanze? Wananchi wangu kule wameshachoka story hizi wanataka waone daraja likiwa limejengwa kwahiyo hicho ndiyo kitu cha kwanza, commitment ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili; ni kwamba palipokuwa na ahadi ya ujenzi wa daraja ilikuwa inaambatana na muendelezo wa ujenzi wa barabara ambayo Mheshimiwa Haonga alikuwa ameuliza katika swali la nyongeza kutokea pale Kamsamba mpaka Mlowo kilometa 166.
Sasa ninachohitaji kujua ni kwamba wakati wa awamu ya nne Waziri Mkuu alipokuwa analijibu hili swali alisema umeingizwa katika mradi wa MCC 3 lakini bahati mbaya wale watu wa Marekani wa MCC 3 walishajitoa katika kuhudumia miradi ya ndani ya nchi yetu. Sasa, je, Serikali ile miradi ambayo iliondolewa na MCC katika Serikali hii ya Awamu ya Tano itatekelezwa vipi ili kuhakikisha kwamba daraja linakamilika na liendane na ujenzi wa lami? Ahsante sana.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi Mheshimiwa Mbunge na ninaamini ni kwa niaba ya wananchi wake, wanahoji udogo udogo au utaratibu unaotumika, kwamba kasi yake kama ya konokono. Mimi nikuhakikishie, hii ni Serikali ya Awamu ya Tano, Serikali hii iko tofauti, Serikali hii imewaahidi wananchi sehemu mbalimbali na umeshaanza kuona sehemu mbalimbali magoli yanaanza kufungwa. Ninakuhakikishia na goli lako litafungwa, daraja na hizo barabara ninazoongelea kabla ya miaka hii mitano haijakwisha. Tuache utaratibu huu wa kitaalam ukamilike na nina uhakika kwa kuwa wameshaanza haitachukua muda kuikamilisha hii kazi ya usanifu na mimi mara baada ya hapo, kwa kuwa fedha tayari tunazo nitahakikisha nalisimamia hili eneo likamilike na hasa kwa sababu mwenzako, jirani yako; na mimi nawasifu sana ninyi Wabunge wawili, wewe na Mheshimiwa Ignas Aloyce Malocha. Ninawasifu sana kwa ushirikiano mnaotumia katika kuhakikisha Daraja la Momba linajengwa.Ni daraja linalohudumia watu, halina Silinde wala halina Ignas Malocha. Mheshimiwa Ignas Malocha anakuja ofisini, Silinde anauliza hapa, wote wanawalenga wananchi wa Momba pamoja na watu wa Kwela.
Mimi niwahakikishie, kazi hii tutaifanya kwa umakini na kama ambavyo tumekuwa tukiwaahidi tutaikamilisha kwa wakati muafaka kabla hiki kipindi chetu hakijaisha.

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:- Ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete ya ujenzi wa daraja la Kamsamba–Kilyamatundu bado haijatekelezwa tangu mwaka 2009. Je, ni upi mpango wa Serikali ya Awamu ya Tano kukamilisha ujenzi wa daraja hilo?

Supplementary Question 2

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa hali ya Momba ni sawa sawa na Moshi Vijijini, kwa sababu Rais wa Awamu ya Nne Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete aliahidi kujenga barabara ya Kibosho kwa Raphael kupitia central mpaka International School; na kazi hiyo ilianza lakini mkandarasi ameondoka site. Vilevile Rais wa Awamu ya Tano Mheshimiwa John Pombe Magufuli aliahidi kujenga barabara ya Mamboleo mpaka Uru Shimbwe kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nijue ni lini ahadi hizi zitatekelezwa?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Komu tuonane ili anipe taarifa za zaidi hasa ya huyo mkandarasi ambaye anasema ameondoka site. Njoo ili tuhakikishe huyo mkandarasi anarudi kwa sababu tulishatoa maelekezo wakandarasi wote ambao walikuwa wamesimama kwa sababu ya kutolipwa warudi site, sasa nashangaa leo naambiwa kuna mkandarasi huku tena kwenye barabara muhimu sana ya ndugu zangu kule wa Kilimanjaro. Hebu njoo ofisini tuongee kwa undani tulifanyie kazi na wataalam wetu wa Mikoa wa TANROADS au wa Halmashauri.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:- Ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete ya ujenzi wa daraja la Kamsamba–Kilyamatundu bado haijatekelezwa tangu mwaka 2009. Je, ni upi mpango wa Serikali ya Awamu ya Tano kukamilisha ujenzi wa daraja hilo?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti nikushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Daraja la Magala na barabara yetu ya Karatu - Mbulu - Haydom - Sibiti Mheshimiwa Waziri aliahidi kwamba itaanza upembuzi yakinifu, sasa swali, je, barabara hii iko kwenye hatua gani, upembuzi yakinifu na lini anafikiri kwamba itaanza ujenzi?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Massay, tulikubaliana kwamba twende site kwa sababu kuna mambo kama matatu ya msingi katika eneo lake. Mimi nimuombe, tutakapofika site tukaifanya kazi inayokusudiwa kuifanya baada ya hapo kama kutakuwa na maswali zaidi ndipo aulize, lakini kwa sasa nimhakikishie kwamba ahadi yangu ya kwenda site iko pale pale na tumekubaliana kipindi gani twende. Mimi naomba tuitumie fursa hiyo kushughulikia mambo makubwa yote matatu ikiwa ni pamoja na Daraja la Mto Ugala, barabara hiyo aliyoitaja Karatu - Mbulu - Haydom vilevile pamoja na wale watu wa Yaeda Chini ambao hawana mawasiliano ya simu.