Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY F. OWENYA aliuliza:- Barabara ya Old Moshi - Kiboriloni - Kikarara - Tsuduni - Kidia yenye urefu wa kilometa10.8 ni muhimu kwa uchumi wa wakazi wa Kata ya Old Moshi Mashariki na Taifa kwa ujumla hasa ikizingatiwa kuwa ni njia mojawapo ya kupanda Mlima Kilimanjaro. Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kwa kuzingatia ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne?

Supplementary Question 1

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kwamba barabara hii inasimamiwa na Halmashauri ya Moshi, lakini kwa kuzingatia kwamba ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Mstaafu na aliyekuwa Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Magufuli, ambaye ni Rais kwa sasa, katika bajeti ya mwaka 2015 waliahidi kutoa shilingi milioni 810 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami, lakini mpaka sasa hivi wananchi wa Old Moshi na wa Kilimanjaro kwa ujumla wake hawajaona chochote kinachoendelea zaidi ya ahadi ya pesa ambazo ziko kwenye makaratasi tu.
Sasa tunataka kujua, watupe time frame, ni lini barabara hii itaanza na ni lini hii zabuni itapitishwa ili barabara ile iweze kujengwa kwa kiwango cha lami, ukizingatia barabara ile kule Tsuduni kuna vivutio vya utalii, kuna vipepeo, kuna waterfalls na kadhalika? Sasa Mheshimiwa Waziri atueleze ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami una hatua. Tunaanza na upembuzi yakinifu, baada ya hapo tunafuata usanifu wa kina na baadaye ndipo tunaingia kwenye ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Fidelis Owenya kwamba barabara hii kutokana na ahadi ambayo Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne aliiitoa tayari imeingizwa katika mchakato. Tumemaliza hatua ya kwanza ya upembuzi yakinifu, sasa hivi tunakaribia kumaliza hatua ya pili ya usanifu wa kina ambapo kilichobakia sasa ni kupata tu taarifa ya mwisho ya msanifu na baada ya hapo barabara hii itaanza kujengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, isitoshe, kama ambavyo nilivyosema katika jibu langu la nyongeza, Mheshimiwa Owenya barabara hii imeshatengewa fedha kwa mwaka huu wa fedha na bahati nzuri sasa hatua zile za mwanzo ambazo zilikuwa ni za lazima zikamilike kabla ya ujenzi kuanza sasa zinakaribia kukamilika. Nimhakikishie ahadi tutaitekeleza kama ilivyoahidiwa na viongozi wetu wakuu.

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. LUCY F. OWENYA aliuliza:- Barabara ya Old Moshi - Kiboriloni - Kikarara - Tsuduni - Kidia yenye urefu wa kilometa10.8 ni muhimu kwa uchumi wa wakazi wa Kata ya Old Moshi Mashariki na Taifa kwa ujumla hasa ikizingatiwa kuwa ni njia mojawapo ya kupanda Mlima Kilimanjaro. Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kwa kuzingatia ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne?

Supplementary Question 2

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza na swali langu napenda kulielekeza kwa Waziri, Wizara ya ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Swali langu linafanana sana na swali lililoulizwa hivi punde; ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Ziba kwenda Ikinga, Simbo mpaka Tabora na Ziba, Choma mpaka Shinyanga hasa ukizingatia hizi ni ahadi za Mheshimiwa Rais na huu ni mwaka wa 2017? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Seif Gulamali na wananchi wote wa Manonga na Wilaya ya Igunga kwa ujumla, kwamba ahadi zote ambazo viongozi wetu wamezitoa katika kipindi hiki cha miaka mitano tutazitekeleza. Lazima twende hatua kwa hatua, hatuwezi kutekeleza ahadi zote kwa mwaka mmoja wa fedha. Na nimhakikishie tu kwamba kabla ya kipindi hiki cha miaka mitano barabara hii tutakuwa tumeitendea haki kama ambavyo viongozi wetu wakubwa wa kitaifa walitolea ahadi.

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. LUCY F. OWENYA aliuliza:- Barabara ya Old Moshi - Kiboriloni - Kikarara - Tsuduni - Kidia yenye urefu wa kilometa10.8 ni muhimu kwa uchumi wa wakazi wa Kata ya Old Moshi Mashariki na Taifa kwa ujumla hasa ikizingatiwa kuwa ni njia mojawapo ya kupanda Mlima Kilimanjaro. Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kwa kuzingatia ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne?

Supplementary Question 3

MHE. PASCHAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Barabara ya kutoka Mji Mdogo wa Mlowo Wilaya ya Mbozi kuelekea Kamsamba ni barabara muhimu sana kwa kuwa inaunganisha Halmashauri ya Mbozi lakini pia na Halmashauri ya Momba. Pia barabara hii inaunganisha Mkoa mpya wa Songwe na Mkoa wa Rukwa na Katavi. Je, ni lini Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nadhani amewahisha swali hili kwa sababu anajua kuna swali lingine zuri kabisa la Mheshimiwa Silinde linakuja; lakini nimhakikishie tu kwamba kila ambapo Serikali hii imeahidi itatekeleza.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY F. OWENYA aliuliza:- Barabara ya Old Moshi - Kiboriloni - Kikarara - Tsuduni - Kidia yenye urefu wa kilometa10.8 ni muhimu kwa uchumi wa wakazi wa Kata ya Old Moshi Mashariki na Taifa kwa ujumla hasa ikizingatiwa kuwa ni njia mojawapo ya kupanda Mlima Kilimanjaro. Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kwa kuzingatia ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne?

Supplementary Question 4

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru sana. Kwa kuwa barabara inayokwenda katika mbuga za wanyama katika Mkoa wetu wa Iringa ni barabara ya kiuchumi pia na Serikali kwa mara ya mwisho nilipouliza swali hilo iliniambia kwamba inafanya upembuzi yakinifu.
Je, ni lini sasa Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara hiyo kwa sababu hii barabara tunategemea kwamba kama itakuwa imemalizika, uchumi wa Iringa kutumia utalii utaongezeka?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Ritta Kabati pamoja na Mheshimiwa Waziri wa Ardhi, walimchukua Waziri wangu wakaenda kuikagua barabara hii na nafahamu aliyowaahidi alipokuwa kule site.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nikuhakikishie, yale ambayo Waziri wangu aliwaelezeni kule site ni lazima tutayatekeleza.