Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:- Katika Jimbo zima la Mlimba kuna kituo kimoja tu cha polisi cha Mngeta jambo linalofanya hali ya usalama kwa wananchi kuwa duni. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya polisi katika Jimbo la Mlimba?

Supplementary Question 1

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu ya kunakili kila swali anapoulizwa majibu yake ndiyo haya haya kwa hiyo ana-copy na ku-paste. Sasa kwa taarifa yako Waziri wa Mambo ya Ndani tarehe 5 Februari, 2017 alifanya ziara katika Jimbo la Mlimba na kuona hali halisi tete ilivyokuwa kule vituo vya polisi vimebandikwa pale TAZARA kwa hiyo hali ni mbaya zaidi ya kiusalama na akatoa ahadi kwenye mkutano wa hadhara baada ya kuona hali ni tete kwamba mwaka huu sisi tutafute kiwanja na kiwanja kimeshatafutwa karibuni ekari 80 kwa matumizi ya umma na sasa tulete ili iingie kwenye bajeti, nakushangaa unajibu swali huwasiliani na Waziri wako.
Sasa je, kwa ahadi aliyotoa Waziri wako tarehe 05 Februari, 2017 Serikali sasa iko tayari kuingiza kwenye mpango wa bajeti ya mwaka 2017/2018 ili Wananchi wa Mlimba wapate kituo cha polisi?
Kwa kuwa ndani ya Jimbo la Mlimba inafanana kabisa na Jimbo ya Kilombero, katika Makao Makuu ya Wilaya Ifakara, kituo cha polisi cha Wilaya kiko kwenye kituo cha maliasili na wakati wa mvua maji yanajaa askari wanaogelea kama bata. Ni lini sasa Serikali itapeleka pesa katika Mpango wa Bajeti wa mwaka 2017/2018 kuhakikisha wanajenga kituo cha Wilaya ya Polisi Ifakara maeneo ya Kibaoni ambapo kiwanja kimeshapatikana?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nimhakikishie Mheshimiwa Susan kwamba hakuna kupingana wala kugongana kokote kati ya mimi na Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, alichokifanya ndiyo tunakifanya ndiyo msimamo wetu. Alifanya ziara Mlimba na hivi juzi tu nimerudi kufanya ziara katika mikoa minne na nataka nikupe mfano ambao nimeuona katika Mkoa wa Mbeya kwenye Jimbo la Mbeya Vijijini ambapo Mbunge wake Mheshimiwa Oran amehamasisha wananchi kuweza kutafuta kiwanja, kuchangia fedha za awali za ujenzi na tukaahidi kama ambavyo Mheshimiwa Waziri alivyokuahidi wewe kwamba tutaangalia kama ambavyo jibu langu la msingi nimejibu pale ambapo fedha zitapatikana tuweze kuingiza katika bajeti kwa ajili ya kumalizia nguvu hizo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi niseme tu kwamba Mheshimiwa Waziri alikuja na aliunga mkono jitihada hizo na naendelea kutoa wito tu kwa Waheshimiwa Wabunge wengine wote, wale ambao wataonakuna haja ya kufanya hivyo, kuongeza jitihada za Serikali kama ulivyotambua tuna upungufu mkubwa sana wa vituo katika nchi nzima. Wilaya, Tarafa na Kata tuna upungufu wa vituo 65 katika wilaya 65 nchi nzima. Kwa hiyo tatizo ni kubwa katika maeneo mengi nchini.
Kwa hiyo, tunaomba Mheshimiwa Susan usivunjike moyo, wewe endelea hivyo hivyo kuhamasisha wananchi, wachangishe na Mheshimiwa Waziri ahadi yake iko pale pale kwamba fedha zitakapopatikana tutachangia nguvu hizo.

Name

Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:- Katika Jimbo zima la Mlimba kuna kituo kimoja tu cha polisi cha Mngeta jambo linalofanya hali ya usalama kwa wananchi kuwa duni. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya polisi katika Jimbo la Mlimba?

Supplementary Question 2

MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa wananchi wa tarafa ya Chipanga Wilaya ya Bahi, kwa takribani miaka 15 iliyopita waliamua kuchanga wao wenyewe na kujenga kituo cha polisi na wakakikamilisha kwa thamani ya wakati huo shilingi milioni 40.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimehangaika sana, nimempeleka Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani wakati huo alikuwa Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha akakiona kituo akashangaa kwa nini hakifunguliwi, nikampeleka Mheshimiwa Naibu Waziri Silima wakati huo akakiona kituo akaona kwanini hakifunguliwi, lakini pia nimemuandikia sasa barua Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Mheshimiwa Naibu Waziri lakini mpaka leo kituo kile hakijafunguliwa.
Sasa nilikuwa nataka kujua hapa leo ama Serikali inatoa kauli ya kufungua kituo cha polisi kile mara moja au itoe kauli ya kutokifungua sisi na wananchi wa tarafa ya Chipanga tukifanyie kazi nyingine? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Badwel pamoja na wananchi wake kwa jitihada hizo lakini nimhakikishie kwamba hili jambo aliwahi kulizungumza mimi sikuwa na hakika na taarifa kwamba mpaka leo bado kituo hicho hakijafunguliwa. Lakini Mheshimiwa Badwel nataka nikuahidi kwamba tukitoka hapa tukae, tufuatilie tuone lini tutafungua kituo hiki ili wananchi waendelee kupata moyo na wsivunjike moyo wa maeneo mengine na Jimbo lako kwa ujumla wake.

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:- Katika Jimbo zima la Mlimba kuna kituo kimoja tu cha polisi cha Mngeta jambo linalofanya hali ya usalama kwa wananchi kuwa duni. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya polisi katika Jimbo la Mlimba?

Supplementary Question 3

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jengo la Polisi la kituo cha Kingeja ni bovu, chakavu, linavuja na jengo hili Serikali walinyang’anya kutoka kwa hao wanaitwa Wakoloni. Kwa bahati mbaya sana wamenyang’anya kutoka kwa hawa wanaitwa wakoloni wakawa wameshindwa kueliendeleza na linahatarisha maisha ya polisi na Naibu Waziri amefika kituo cha Polisi cha Kingeja huku akiwa na ahadi lukuki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka utuambie leo Mheshimiwa Waziri, una mikakati gani ya ziada kuhakikisha kwamba kituo cha polisi cha Kingeja ambacho mlinyang’anya kwa wakoloni, jengo lile sasa hivi linapatiwa ukarabati wa hali ya juu ili polisi wale wasipate madhara yoyote? Nashukuru.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, anachokizungumza Mheshimiwa Masoud ni sahihi, binafsi nilifanya ziara katika Jimbo hilo la Mtambile na nilikitembelea hiki kituo, kwa kweli hiki kituo kiko katika hali mbaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nataka nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba hatujakaa kimya wala hatujadharau. Tunatambua changamoto kubwa ya ubovu wa kile kituo kama ambavyo vituo vingine vingi katika nchi yetu na kama ambavyo nimezungumza mwanzo kwamba pale ambapo tutapata fedha za ujenzi na ukarabati wa vituo hivyo tutafanya hivyo haraka sana.