Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY aliuliza:- Wavuvi kutoka Ukanda wa Uvuvi wa Kisiwa cha Unguja na wale wa Ukanda wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani wamekuwa wakifanya uvuvi kwenye maeneo yanayoingiliana, lakini hivi punde wavuvi wa Unguja wameanza kusumbuliwa na kuwekewa vikwazo vya kuvua maeneo ya Tanzania Bara:- (a) Je, kwa nini wavuvi hao wasumbuliwe na kuwekewa vikwazo? (b) Je, wavuvi hao hawana haki ya kuvua maeneo hayo? (c) Je, ni kwa nini Serikali isiwaelimishe juu ya wanachotakiwa kufanya au wasichotakiwa kufanya?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Waziri ametuambia hapa kwamba kuna sharia zinazosimamia suala hili lakini sijui kama ana taarifa kwamba watu hupigwa na kunyang’anywa mali zao na lini jambo hili litakoma ili sheria ifuate mkondo na siyo kunyang’anywa mali zao na kupigwa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Waziri amesema kwamba kuna elimu inatolewa juu ya watu hawa wa Dago ambapo kwa Wazanzibar ni jambo asili na la muda mrefu tu kutoka Bara kuja Unguja kama vile watu wanavyotoka hapa kwenda Dago Zanzibar. Je, Waziri anajua kwamba hiyo elimu anayoisema haijaenea kiasi cha kutosha ndiyo sababu ya sokomoko linalotokea katika eneo la wavuvi hawa?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa kwamba watu hupigwa na kunyang’anywa mali zao hazijafika rasmi Wizarani. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba pale tutakapopata taarifa hizi tutachukua hatua stahiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nimueleze kwamba nafahamu kuna changamoto nyingi zinatokea katika Kambi za Dago hasa maeneo ya Mafia, kuna changamoto nyingi ambazo zimeripotiwa. Wizara yangu ina mkakati na mimi mwenyewe nimepanga kwamba mara nitokapo kwenye Bunge hili nitaelekea Mafia kwa sababu mbali na alichosema Mheshimiwa Mbunge tayari Wabunge wengi wa ukanda huo na hasa wanaotoka maeneo ya Mafia wameleta changamoto nyingi ambazo zipo, nitaendelea kufahamu changamoto zilizopo kule ili kuweza kuzipatia suluhu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nitumie fursa hii kupitia Bunge hili kuwasihi wananchi kwamba utaratibu wa Dago ni utaratibu mzuri lakini ni mzuri tu kama unafuatwa. Kama wavuvi wakiwa wanatoka eneo moja kwenda lingine bila kufuata taratibu ni vigumu sana Serikali kutoa msaada wowote. Kwa hiyo, ni vizuri tufuate taratibu na sheria zilizopo ili kuondoa vurugu ambazo zinatokea kwenye Dago.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la nyongeza la pili lilitaka nijibu kama kuna elimu inatolewa Zanzibar. Nimweleze Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa taarifa tulizonazo sisi ni kwamba elimu hiyo inatolewa kote na mara nyingi inatolewa kwenye halmashauri anapokwenda kuvua mvuvi siyo kule anapotoka. Kwa hiyo, tunaendelea kusisitiza kwamba kama kuna upungufu katika elimu inayotolewa, tutaendelea kuwasiliana na mamlaka husika kuhakikisha kwamba elimu hii inatolewa kwa wavuvi wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY aliuliza:- Wavuvi kutoka Ukanda wa Uvuvi wa Kisiwa cha Unguja na wale wa Ukanda wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani wamekuwa wakifanya uvuvi kwenye maeneo yanayoingiliana, lakini hivi punde wavuvi wa Unguja wameanza kusumbuliwa na kuwekewa vikwazo vya kuvua maeneo ya Tanzania Bara:- (a) Je, kwa nini wavuvi hao wasumbuliwe na kuwekewa vikwazo? (b) Je, wavuvi hao hawana haki ya kuvua maeneo hayo? (c) Je, ni kwa nini Serikali isiwaelimishe juu ya wanachotakiwa kufanya au wasichotakiwa kufanya?

Supplementary Question 2

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa sekta ya uvuvi ni muhimu sana katika kukuza uchumi wa Taifa na ni sekta oevu kwa kupata mapato ya Taifa pia kuweza kuwapatia vijana wetu ajira. Serikali imeshafanyia kazi kiasi gani Taarifa ya Chenge One kuhusu sekta hii ya uvuvi hasa wa bahari kuu ambapo Serikali itapata mapato, wawekezaji wataweza kushirikiana na wawekezaji wa ndani ili Taifa letu liweze kujikwamua katika hali ambayo ipo na rasilimali tunayo? (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli naungana naye kwamba sekta ya uvuvi ni sekta ambayo inategemewa sana na Watanzania wengi. Ni sekta ambayo inawaajiri Watanzania 4,000,000, kuna operators mbalimbali wanaofika 400,000 wanaojihususha na shughuli za uvuvi, kwa hiyo ni sekta muhimu sana. Vile vile nikubaliane naye kwamba potential iliyopo ni kubwa na kuna fursa kubwa sana ya kuweza kufanya hili eneo liweze kuchangia zaidi katika maendeleo ya Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kumekuwa na mapendekezo mengi ya namna ya kuboresha ufanisi wa sekta hii ikiwa ni pamoja na ripoti aliyosema ya Chenge One ambayo pamoja na mambo mengine ilipendekeza ni namna gani tunaweza tukapanua wigo wa fursa za uvuvi kwa kutumia bahari kuu. Katika kutekeleza ushauri huu, Wizara ipo katika mpango wa kuchukua hatua mbalimbali ili kuhakikisha kwamba tunaweza kuanza kunufaika na rasilimali iliyopo katika bahari kuu. Kwa kuanzia, tupo kwenye mkakati wa kuanzisha fishing port. Tunataka tuanzishe bahari ya uvuvi ambayo pamoja na mambo mengine itakuwa rahisi kuratibu namna uvuvi unavyofanywa katika bahari kuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kama nilivyokwishasema hata katika Bunge hili tumeshakutana na Waheshimiwa Wabunge wanaotoka maeneo ya uvuvi na leo hii tena mchana tunakutana. Tunaendelea kupokea mawazo ya Waheshimiwa Wabunge ili tuone namna ya kuboresha sekta hii muhimu katika Taifa letu.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY aliuliza:- Wavuvi kutoka Ukanda wa Uvuvi wa Kisiwa cha Unguja na wale wa Ukanda wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani wamekuwa wakifanya uvuvi kwenye maeneo yanayoingiliana, lakini hivi punde wavuvi wa Unguja wameanza kusumbuliwa na kuwekewa vikwazo vya kuvua maeneo ya Tanzania Bara:- (a) Je, kwa nini wavuvi hao wasumbuliwe na kuwekewa vikwazo? (b) Je, wavuvi hao hawana haki ya kuvua maeneo hayo? (c) Je, ni kwa nini Serikali isiwaelimishe juu ya wanachotakiwa kufanya au wasichotakiwa kufanya?

Supplementary Question 3

MWENYEKITI: Mheshimiwa Dkt. Ndugulile na wa mwisho jirani yako Mheshimiwa Keissy.
MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Kigamboni lina jamii kubwa sana ya wavuvi lakini sekta hii ina changomoto kubwa sana. Wavuvi wana leseni za chombo, wana leseni za baharia, wana leseni ya aina ya samaki wanayovua lakini wavuvi hawa hawa wakitoka Dar es Salaam wakiingia Mafia kuna leseni nyingine ambayo wanatakiwa kukata. Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya mapitio ya mzigo wa leseni ili kuondoa hizi kero kwa ajili ya wavuvi hawa? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. Faustine Mbunge wa Kigamboni kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia sana suala la wavuvi, nakumbuka alishakuja ofisini mara kadhaa. Niseme tu kwamba Wizara na Serikali kwa ujumla inayaangalia maeneo yanayolalamikiwa katika kazi zinazowapatia Watanzania kipato hasahasa yanayohusu makato mengi yanayokwenda kwa mtu anapofanya shughuli yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, amelisemea hili la leseni nyingi na nilipokutana na Wabunge wanaotokea maeneo ya uvuvi upande wa Kanda ya Ziwa walisema hata mtu akitoka Nyamagana akiingia Ilemela anatakiwa atoe leseni nyingine. Lingine wavuvi ni Watanzania na maji ni ya Tanzania lakini leseni inatolewa kwa dola na lenyewe tumepokea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na Wabunge kwamba vikao hivi tunavyofanya vya kukutana nao ni kwa ajili ya kuandaa mpango maalum ambao utatoa majawabu ya kudumu ya malalamiko hayo ambayo Wabunge wameyaleta kwa niaba ya wananchi wao. Kwa hiyo, tutalifanyia kazi na tutatoa tamko ambalo litakomesha yale ambayo yanawakwaza wavuvi, wafugaji pamoja na wakulima.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY aliuliza:- Wavuvi kutoka Ukanda wa Uvuvi wa Kisiwa cha Unguja na wale wa Ukanda wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani wamekuwa wakifanya uvuvi kwenye maeneo yanayoingiliana, lakini hivi punde wavuvi wa Unguja wameanza kusumbuliwa na kuwekewa vikwazo vya kuvua maeneo ya Tanzania Bara:- (a) Je, kwa nini wavuvi hao wasumbuliwe na kuwekewa vikwazo? (b) Je, wavuvi hao hawana haki ya kuvua maeneo hayo? (c) Je, ni kwa nini Serikali isiwaelimishe juu ya wanachotakiwa kufanya au wasichotakiwa kufanya?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY M. KEISSY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mwambao wa Ziwa Tanganyika wavuvi wengi wanatoka DRC-Congo. Cha ajabu wanakata leseni kwa bei kama mvuvi mwenyeji wa Ziwa Tanganyika. Je, ni lini Serikali itachukua hatua ili wavuvi kutoka nchi za jirani walipie leseni kama inavyotakiwa?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Keissy kwa sababu amekuwa akifuatilia kwa karibu sana changamoto mbalimbali za uvuvi na hasa katika maeneo ya Jimbo lake. Tumepata taarifa kwamba kuna wavuvi wanaotoka nchi za jirani wanavua katika maziwa yetu. Kwa vyovyote vile, hii ni kinyume na sheria. Tunaomba Waheshimiwa Wabunge taarifa kama hizi tuendelee kuzipata. Tukitoka hapa mimi mwenyewe nitachukua hatua za makusudi za kufuatilia ili tuweze kujua nani amehusika, tuwajue Maafisa wa Halmashauri wanaotoa leseni kwa watu hao ili kuweza kuchukua hatua stahiki.