Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali kupitia Benki ya Dunia ilianzisha mradi wa maji katika Miji ya Haydom, Masieda, Tumati Arri na Bwawa la Dongobesh lakini mpaka sasa mradi huo haujakamilika baada ya fedha kusitishwa:- Je, Serikali imejipangaje kumaliza miradi hii ili wananchi wapate maji?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa miradi hii haijakamilika na wananchi sasa hivi wanapata adha ya kutopata maji hasa katika miji niliyoisema na vijiji vyake, je, Serikali itahakikisha vipi leo hii itapeleka pesa kule ili wananchi wapate maji?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kutokana na adha ya maji katika maeneo yetu, yuko mwananchi mmoja amechimba maji na kuyapata katika Mji wa Hydom. Je, kwa nini Serikali isiweze kupata maji katika maeneo yale na kuweka hela nyingi namna hii? Waziri yuko tayari kufuatana na mimi akaone jinsi ambavyo wananchi wanapata adha katika mji wa Hydom na maeneo mengine ya Mbulu Vijini? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Massay yeye mwenyewe tayari anafahamu kwamba Serikali ya Awamu ya Tano inafanya juhudi kubwa sana kukusanya pesa. Sasa hivi pesa zimeanza kupatikana kwa hiyo wakati wowote ule fedha zitaanza kutumwa kwenda kukamilisha miradi ambayo haijakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyozungumza katika maswali yaliyopita kwamba tumekuwa na miradi ya maji 1,855, miradi 1,143 tayari imeshakamilika na iliyobaki ni 454 ambayo tunatarajia tuipatie pesa ili iweze kukamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, muuliza swali amedai kwamba kuna mwananchi ambaye amepata maji lakini haku-specify kwamba huyo mtu aliyapata hayo maji kwa shilingi ngapi? Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kuna miradi inayoendelea katika wilaya yake. Kuna Mradi wa Tumati, Hasha, Mungay, Hydom, Moringa na Dongobesh. Miradi hii ikikamilika, naimani kabisa kwamba matatizo ya maji katika eneo lake yatakuwa yamekwisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwa kibali cha Mheshimiwa Spika, nitakuwa tayari kufuatana naye ili kwenda kuona tatizo lilivyo kwenye Jimbo lake.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali kupitia Benki ya Dunia ilianzisha mradi wa maji katika Miji ya Haydom, Masieda, Tumati Arri na Bwawa la Dongobesh lakini mpaka sasa mradi huo haujakamilika baada ya fedha kusitishwa:- Je, Serikali imejipangaje kumaliza miradi hii ili wananchi wapate maji?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa matatizo ya maji yaliyoko Hydom yanafanana kabisa na matatizo ya maji yaliyoko katika Mkoa wangu wa Arusha hasa Longido na Monduli. Kwa kuwa Monduli walikuwa na mabwawa matatu ambayo yamepasuka na sasa hivi wananchi wa Monduli wana tabu kubwa sana ya maji, wana-share maji na mifugo. Kwa kuwa kuna maji yanamwagika Engaruka na Mto wa Mbu, je, Serikali haioni umuhimu wa kuwasaidia wananchi hawa wa Monduli kwa kuyatumia maji yale kuliko yanavyomwagika bure? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru ametupa taarifa kuna mabwawa ambayo yamepasuka katika Jimbo la Mbulu. Naomba kuchukua nafasi hii kuagiza Mkoa wa Arusha wakatembelee eneo hilo na waipe taarifa Wizara ili hatua mahsusi ziweze kuchukuliwa.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali kupitia Benki ya Dunia ilianzisha mradi wa maji katika Miji ya Haydom, Masieda, Tumati Arri na Bwawa la Dongobesh lakini mpaka sasa mradi huo haujakamilika baada ya fedha kusitishwa:- Je, Serikali imejipangaje kumaliza miradi hii ili wananchi wapate maji?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo ambalo lipo kwenye maeneo mengi katika nchi yetu ni miradi ya maji ambayo Serikali ilianzisha kushindwa kutekelezwa. Jimboni kwangu kuna miradi ya maji katika Kijiji cha Majalila na Igagala na imeanza kufanyiwa kazi na imefikia asilimia 70. Sasa hivi miundombinu ya miradi ile imeanza kuharibika kwa sababu ya ukosefu wa fedha. Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia ile miradi ambayo kimsingi ingewasaidia wananchi kwenye maeneo hayo?

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ipo miradi mingi, tuna miradi zaidi ya 508 ambapo katika awamu ya kwanza ya programu haijakamilika. Hivi sasa ipo katika hatua mbalimbali, ipo kwenye asilimia 99 na mengine 60. Sasa hivi tumeingia awamu ya pili ya programu lakini lazima kwanza tukamilishe ile miradi ambayo ipo mbioni kukamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi fedha zimeshaanza kupatikana kwa ajili ya kuwalipa wakandarasi ambao walikuwa katika hatua mbalimbali na maeneo mengine walikuwa yamesimama, kwa hiyo, tunawalipa ili kusudi wakamilishe miradi hiyo. Nilihakikishie Bunge lako kwamba Serikali itakwenda kukamilisha miradi yote ili wananchi wetu waweze kupata maji kama ilivyokusudiwa.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Serikali kupitia Benki ya Dunia ilianzisha mradi wa maji katika Miji ya Haydom, Masieda, Tumati Arri na Bwawa la Dongobesh lakini mpaka sasa mradi huo haujakamilika baada ya fedha kusitishwa:- Je, Serikali imejipangaje kumaliza miradi hii ili wananchi wapate maji?

Supplementary Question 4

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona na kunipa nafasi. Napenda kumuuliza swali la nyongeza Mheshimiwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upo mradi wa umwagiliajii wa Bonde la Bigombo ambao ulianza 2012 na ulitakiwa kukamilika 2013, ulifadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika chini ya ASDP, mpaka sasa mradi huo haujakamilika. Mradi huu ilikuwa ni tegemeo kwa wananchi wa Jimbo la Ngara hususani wananchi wa Kata ya Rulenge, Keza na Nyakisasa kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji. Ni lini sasa mradi huu utaweza kukamilika?

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, jana nilisema kwamba miradi yote ya umwagiliaji inasimamiwa na Tume ya Umwagiliaji. Nikasema katika bajeti ya mwaka huu wa 2015/2016, tumepanga fedha kiasi cha shilingi bilioni 53 katika kuendeleza sekta hii ya umwagiliaji. Miradi hii ilikuwa imeanzishwa chini ya programu ya ASDP ambapo wafadhili ni African Development Bank na mingi ilikuwa haijakamilika. Kwa sababu tumeunda Tume, tutakwenda kufuatilia tuone tunaweza kukamilisha kwa namna gani mradi ambao tayari ulikuwa umeshaanza.