Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti, Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana pa kwenda:- Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo hilo.

Supplementary Question 1

MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru
Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake. Kwa kuwa, Wizara ya Maliasili imelitelekeza
hili eneo kwa muda mrefu na hili eneo limekuwa ni eneo hatarishi na lipo katikati
ya makazi ya watu, watu wamekuwa wakipita hapo wanavamiwa na wengine
wameumizwa. Je, Wizara haioni sasa umefikia wakati muafaka kulirudisha hili
eneo Manispaa ya Ilala ili liweze kutumika kwa maendeleo ya Watanzania wote.
(Makofi)
Swali la pili; Jimbo la Segerea lina wakazi wengi lakini ndio Jimbo mpaka
sasa hivi halina kituo cha afya, halina soko, halina viwanda vidogovidogo
ambavyo wananchi au vijana wanaweza wakajiendeleza. Je, Wizara ya Maliasili
haioni kwamba umefika wakati ilirudishe hili eneo kwa wananchi wa Jimbo la
Segerea ili sisi tuweze kujenga kituo cha afya na mimi Mbunge wa Jimbo la Segerea nitatoa milioni 50 katika Mfuko wa Mbunge ili tuweze kuanzisha kujenga
kituo cha afya.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu
swali lake la kwanza Wizara haijatelekeza eneo la Msitu wa Kinyerezi na badala
yake miongoni mwa maeneo ambayo tayari yana maboya kwenye mipaka na
ambayo yana mabango na usimamizi wake unaendelea kwa kufuata mipaka
hiyo niliyoitaja ambayo imeshawekwa alama kama nilivyotangulia kusema eneo
la msitu huu ni mojawapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema eneo hili ni la hekta 4.4 tu.
Eneo la hekta 4.4 ni dogo sana, tunapata changamoto kubwa sana kama Taifa
ya kwamba Miji inaonekana kama vile ili uone mahali kuna mji ni sawasawa
kwamba panatakiwa pawe mahali palipo wazi kabisa hapatakiwi kuwa na miti
hata kidogo. Hii ni dhana ambayo tunapaswa kuondokana nayo twende katika
mwelekeo ambao Miji yetu itakuwa pamoja na majengo na vitu vingine
unavyoweza kuviona kama miundombinu, misitu iwe ni sehemu mojawapo. Tuwe
na miti, bustani ndiyo tunaweza kuwa na miji ambayo itakuwa endelevu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili la mahitaji ya eneo;
nimesema kwenye swali la msingi, Ilala ina eneo kubwa bado kwa mujibu wa
sensa iliyopo ina jumla ya hekta 21,000. Kwa hiyo, hakuna uhaba wa ardhi, tuna
changamoto ya matumizi bora ya ardhi. Haya mambo mawili ni tofauti. Kukosa
ardhi au kuwa na uhaba wa ardhi na kukosa mbinu za matumizi bora ya ardhi ni
mambo mawili tofauti.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu narudia tena Mheshimiwa
Mbunge kwa kushirikiana na Baraza la Madiwani na Halmashauri ya Wilaya
inayohusika, waende wakakae wajaribu kuangalia Ilala kwa ukubwa wake na
eneo lake lote, miundombinu iliyopo na fursa zingine zilizopo za matumizi ya
ardhi, wafanye mpango bora wa matumizi ya ardhi ili waweze kupata maeneo
ya kuweza kujenga miundombinu aliyoizungumzia.

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti, Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana pa kwenda:- Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo hilo.

Supplementary Question 2

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Wakati
likijibiwa swali juu ya Msitu wa Nyuki, Serikali imeeleza kwamba inakusudia
kuendeleza msitu huu kuwa sehemu ya vivutio vya utalii Dar es Salaam. Kwa
miaka mingi Serikali imekuwa ikitoa ahadi juu ya kuugeuza msitu wa akiba wa
Pande (Pande Forest Reserve) kuwa kivutio cha utalii, ikafikia hatua mpaka
Serikali ikatangaza tenda.
Sasa kama msitu huu mpaka leo haujakamilika kuwa kivutio cha utalii ni
miujiza gani ambayo Serikali inayo ili kuharakisha kwamba haya mapori ya Dar es
Salaam yageuzwe kuwa sehemu za utalii na kuingiza kipato kwa Dar es Salaam
badala ya kuyaacha kama yalivyo na hatimaye kugeuka kuwa misitu ya mauaji
kama ilivyokuwa pori la akiba la Mabwepande.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza
nimpongeze kwa mtazamo ambao ni chanya wa kwamba, kwanza
anakubaliana na dhana nzima ya matumizi bora ya maeneo ya misitu;
hapingani na dhana nzima ya Serikali kuhusiana na kuifanya misitu iwe ni
rasilimali ambayo inaweza kutumika kwa ajili ya maslahi ya jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kwamba kuna ucheleweshaji
kama ambavyo amesema; nataka nimtoe wasiwasi kwamba historia ni nzuri,
inatukumbusha tulipotoka, mahali tulipo na inatuwezesha kuona kule ambako
tunakwenda.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka Mheshimiwa Mnyika akubaliane tu na
rai yangu kwamba tumetoka huko tulikotoka, mipango imekuwepo lakini sasa
awamu hii mipango hii ninayoizungumza ni uhakika na kwamba nataka anipe
muda wa mwaka mmoja tu, halafu aweze kuona katika eneo hili tunafanya nini.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti, Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana pa kwenda:- Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo hilo.

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa
kunipa nafasi. matatizo yaliyopo huko Segerea yapo pia katika Jimbo langu la
Manyoni Magharibi katika Halmashauri ya Itigi kuna msitu unaitwa Chaya Open
Area, ni kitalu cha uwindaji ambacho muda mrefu hakina Mwekezaji. Sasa
Serikali inataka kuondoa wananchi ambao wamekaa pale kwa ajili ya kulima na
wanafuga vizuri sana. Je, Serikali inaweza ikaona umuhimu wa wananchi wale
kuendelea kutumia Chaya Open Area ambapo ni eneo ambalo halina kabisa
faida kwa ajili ya uwindaji?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika,
anazungumzia eneo la Chaya na anatoa maoni kwamba pengine Serikali ilitoe
sasa eneo hili kwa ajili ya matumizi ya kibinadamu kwa wananchi wa eneo hilo
na wanaozunguka eneo hilo. Tumejibu swali hili mara nyingi kama Serikali
kwamba tunayo changamoto kama Taifa ya kwamba katika maeneo kadhaa
wananchi wamepata au wameonekana kuwa na uhitaji wa maeneo kwa ajili ya
matumizi ya kibinadamu yakiwemo makazi, kilimo pamoja na ufugaji. Kama
Serikali tumekwishasema kwamba jambo hili linatakiwa lishughulikiwe kisayansi na
kitaalam. Huwezi kuzungumzia juu ya uhaba wa ardhi juujuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa wakati huu tunavyoendelea tayari Serikali
imekwishaunda Kamati ya Kitaifa inayohusisha Wizara nne ambayo inapita katika
maeneo yote ya nchi hii kuangalia kwa uhalisia kabisa wapi kweli kuna uhaba
wa ardhi na wapi kweli ardhi tungeweza kuitumia kwa namna bora zaidi. Kamati
hii itasaidia baadaye Serikali iweze kuja kusema kwamba eneo hili ni kweli
linaweza likabadilishwa matumizi na eneo lingine liendelee kubakia kutumika
kwa namna ambayo sote tutakubaliana tukiwa tunaongozwa na Serikali
kwamba matumizi hayo ya hivi sasa ni matumizi ambayo yana tija zaidi kwa
Taifa.