Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:- Mradi wa Masoko Group Water Scheme umeshughulikiwa kidogo na miundombinu tayari imeshaharibika. Je, ni lini mradi huu utamaliziwa?

Supplementary Question 1

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na
majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naipongeza Serikali kwa jinsi
ambavyo wameushughulikia mradi huu wa masoko na miradi mingine iliyo ndani
ya Wilaya ya Rungwe. Nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza; kwa kuwa,
mradi huu wa maji umechukua muda mrefu na Mkandarasi aliyekuwa amepewa kazi hiyo Osaka, baada ya kutangazwa tenda ya mara ya pili anaondolewa.
Tungependa kufahamu ni sababu gani zimesababisha Mkandarasi huyu wa
mara ya kwanza ashindwane na Halmashauri?
Swali la pili; kwa kuwa, miradi hii ya maji ni ya thamani kubwa, zaidi ya
bilioni tano tungependa tumwombe Mheshimiwa Naibu Waziri aweze
kuitembelea hii miradi pamoja na ya Mwakaleli One pamoja na Kapondelo
ikiwemo na hii ya Masoko. Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika,
ameuliza sababu zilizofanya Mkandarasi asimamishwe kuendelea na kazi,
sababu ziko kimkataba. Kwa hiyo, sababu za kimkataba hatuwezi kuzijadili sisi
Waheshimiwa Wabunge, lakini la kuelewa tu ni kwamba, alishindwa ku-perform
vile ilivyokuwa imetakiwa kimkataba ndiyo maana Halmashauri kwa kutumia
vifungu vya mkataba ikamsimamisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nimpongeze Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Rungwe. Kwa mara ya kwanza ameleta bajeti ya miaka mitano na nimefurahi
sana. Ameweka mpango wa miaka mitano na bajeti inayotakiwa akaweka na
kifungu cha matengenezo ya miradi atakayokuwa ameitekeleza ili kuhakikisha
kwamba miradi tunayojenga basi inakuwa ni ya kudumu na mabomba
yanaendelea kutoa maji mwaka mzima.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:- Mradi wa Masoko Group Water Scheme umeshughulikiwa kidogo na miundombinu tayari imeshaharibika. Je, ni lini mradi huu utamaliziwa?

Supplementary Question 2

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa
kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu
Waziri, nauliza swali ambalo kama ilivyo Rungwe ule mradi wa Masoko, Tabora
Mjini ule mradi wa Ziwa Victoria, kuna vijiji ambavyo niliviorodhesha kwenye swali
Na. 57 lililojibiwa hapa Bungeni ambavyo ni Vijiji vya Itetemla, Uyui, Ntalikwa,
Kabila, Mtendeni, Itonjanda na baadhi ya maeneo ambayo ni ya Kata za Tumbi.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji hivi na hizi Kata havijaorodheshwa kwenye
huu mradi wa Ziwa Victoria na vina shida sana ya maji. Sijui vitapitiwa lini na
mradi huu wa Ziwa Victoria? Naomba swali langu lipatiwe majibu. Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika,
kwanza kabisa Tabora Mjini kuna mradi mkubwa wa maji ambao umekamilika
kutoka bwawa la Igombe na kwamba maji yanayozalishwa ni lita milioni 30 kwa
siku wakati mahitaji ni lita milioni 24. Kwa hiyo, kwa maana ya Tabora Mjini tayari
imeshakamilisha huduma maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia tupo na mradi ambao sasa hivi upo kwenye
zabuni ambao utatoa maji kutoka Ziwa Victoria kupeleka Nzega, Tabora na Igunga. Kwa hiyo, nina hakika kabisa kwamba sasa Tabora itakuwa na maji
mengi na ndiyo maana tunataka hayo maji yakishafika tuyaelekeze yaende
mpaka eneo la Sikonge. Kwa hiyo, Vijiji vyote Mheshimiwa Mbunge ambavyo
havina maji nje ya Manispaa ya Tabora kupitia mradi huo tutakuwa na maji ya
uhakika kuhakikisha sasa kata na vijiji vyote vinapata maji ikiwemo na sehemu ya
eneo la Uyui.

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:- Mradi wa Masoko Group Water Scheme umeshughulikiwa kidogo na miundombinu tayari imeshaharibika. Je, ni lini mradi huu utamaliziwa?

Supplementary Question 3

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Katika
Mkoa wa Katavi kumekuwa na changamoto kubwa ya miradi ya maji kuendelea
kusuasua kwisha. Je, ni lini sasa Serikali itasema mikakati ya kujenga hii miradi ili
iishe kwa wakati, kwa sababu pesa nyingi zimekuwa zikitumika mfano, kwenye
Kata ya Ugala ambako kuna mradi mpaka sasa ni miezi sita, mradi umesimama.
Sasa, ni lini Serikali itamaliza kujenga hii miundombinu ya umwagiliaji.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika,
kwanza kabisa Mkoa wa Katavi, eneo la Mpanda linahitaji lita milioni 11 kwa siku,
lakini sasa hivi maji yanayozalishwa ni lita milioni 3.5. Tayari tumeshakamilisha
mradi wa Ikolongo na wananchi wanaendelea kupata huduma; lakini tuna
miradi miwili ambayo tunasaini mwezi huu kwa ajili ya kuleta maji Mji wa
Mpanda. Kwa upande wa eneo la Ugala kwanza lina bwawa moja kubwa
ambalo linaweza kuhudumia ule Mji wa Ugala. Sasa hivi kupitia kwenye
Halmashauri tunayo miradi ambayo inaendelea kuhakikisha kwamba wananchi
wa Ugala wanapata huduma ya maji.