Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATUMA H. TOUFIQ aliuliza:- Ujenzi wa Maternity Complex katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma ulianza tangu mwaka 2009 ambapo majengo hayo yana uwezo wa kuweka vitanda 180, lakini hadi leo jengo hilo halijakamilika kutokana na Serikali kuamua kuimarisha huduma ya afya ya mama na mtoto kwa kuzingatia vipaumbele vya Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa (BRN). Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati wa kutekeleza Matokeo Makubwa Sasa kwa kuiangalia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma kwa jicho la pekee kwa kuipatia fedha ili jengo hilo likamilike haraka ili kuwaondolea adha kubwa wanayopata akinamama wakati wa uzazi?

Supplementary Question 1

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ni kwamba hadi sasa hivi katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma pesa ambayo imeidhinishwa mwaka 2014/2015 haijatolewa na pia ya 2015/2016 haijatolewa:-
(i) Je, ni lini pesa hizi zitatolewa ili kukamilisha ujenzi huo?
(ii)Je, Serikali haioni kwamba inaingia gharama za ziada inapochelewesha miradi na kuathiri mipango ya wale wakandarasi? Ahsante.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni lini Serikali itakuwa tayari kutoa pesa hizo, jibu kwa ufupi ni kwamba pesa hizo kwa kuwa zipo kwenye bajeti, zitatolewa pindi Serikali itakapopata pesa za kutosha na ambazo zitakuwa tayari kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu variation ambayo inatokana na kuchelewa kwa miradi, kwa bahati mbaya sana kuna gharama nyingine haziepukiki kutokana na uwezo mdogo wa kiuchumi wa nchi yetu. Nia thabiti ipo na utekelezaji utafanyika tu pale ambapo tutaweza kuwa na fedha hizo. Kwa bahati mbaya sana kama tutakuwa tumeshaingia gharama hatutakuwa na namna ya kuzikwepa kwa kuwa ndiyo hali halisi ya uchumi wetu.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATUMA H. TOUFIQ aliuliza:- Ujenzi wa Maternity Complex katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma ulianza tangu mwaka 2009 ambapo majengo hayo yana uwezo wa kuweka vitanda 180, lakini hadi leo jengo hilo halijakamilika kutokana na Serikali kuamua kuimarisha huduma ya afya ya mama na mtoto kwa kuzingatia vipaumbele vya Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa (BRN). Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati wa kutekeleza Matokeo Makubwa Sasa kwa kuiangalia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma kwa jicho la pekee kwa kuipatia fedha ili jengo hilo likamilike haraka ili kuwaondolea adha kubwa wanayopata akinamama wakati wa uzazi?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTER A BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Dodoma ilijengwa mwaka 1923 na ilipojengwa ilikuwa na wakazi wasiozidi elfu hamsini lakini kwa sasa Dodoma ina wakazi takribani laki sita na majengo yako vilevile wala hayajaongezeka. Bima ya Afya waliamua kujenga jengo kwa ajili ya kupunguza wingi wa watu katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma ambalo lina miaka mingi halijakamilika, limekabidhiwa lakini hakuna samani ndani yake.
MWENYEKITI: Uliza swali sasa.
MHE. FELISTER A. BURA: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuishawishi Bima ya Afya ambayo ipo chini ya Wizara yake kuleta samani na kukamilisha jengo lile ili lianze kutumika kwa wagonjwa wa Dodoma?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Bura kwa swali lake la nyongeza. Sisi hatuna shida na kuishawishi taasisi ya NHIF kuwakopesha Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, lakini ukweli utabaki palepale, narudia tena ukweli utabaki palepale kwamba hospitali hizi za mikoa zipo chini ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Naomba Waheshimiwa Wabunge tunapohudhuria vikao vya RCC tuikumbuke sekta ya afya kwa kushawishi bajeti maalum za mikoa na hata bajeti za kawaida za mikoa kwa kiasi kikubwa zielekezwe kwenye kuboresha hospitali zetu ikiwa ni pamoja na utanuzi wa majengo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia suala la mikopo NHIF ni suala la kibiashara zaidi. Kama hospitali husika ina makusanyo na vigezo vinavyotosha kuwezesha kupata pesa kwa mkopo kutoka NHIF basi uongozi wa hospitali husika utafanya mazungumzo ya kibiashara ambayo yana faida kwa pande zote mbili baina ya wao wenyewe. Hili wala siyo suala la sisi kama Wizara kwenda kuishawishi NHIF kwa sababu mambo haya yanahusu fedha na fedha zinataratibu zake.

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. FATUMA H. TOUFIQ aliuliza:- Ujenzi wa Maternity Complex katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma ulianza tangu mwaka 2009 ambapo majengo hayo yana uwezo wa kuweka vitanda 180, lakini hadi leo jengo hilo halijakamilika kutokana na Serikali kuamua kuimarisha huduma ya afya ya mama na mtoto kwa kuzingatia vipaumbele vya Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa (BRN). Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati wa kutekeleza Matokeo Makubwa Sasa kwa kuiangalia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma kwa jicho la pekee kwa kuipatia fedha ili jengo hilo likamilike haraka ili kuwaondolea adha kubwa wanayopata akinamama wakati wa uzazi?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH N. MAFTAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Naomba niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kwa muda mrefu Serikali ilikuwa na mpango wa kuhakikisha inatoa huduma za afya bure kwa wazee, lakini kumekuwa na mkakati na utaratibu wa kutoa bima ama kadi za matibabu kwa wazee ambazo zina mipaka. Kwa mfano, mzee wa Mtwara Mjini akienda Mtwara Vijijini kule hana nafasi ya kutibiwa japokuwa ana zile kadi. Je, Serikali ina mkakati gani sasa hivi wa kuondoa mipaka ya kadi za matibabu za wazee? (Makofi)

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa kuuliza swali hili la muhimu sana. Takribani mwezi mmoja umepita Mheshimiwa Waziri wa Afya alinipa jukumu la kutengeneza Kikosi Kazi ambacho kitawashirikisha wadau mbalimbali kwenye Mfuko wa Afya kwa Umma (CHF) na Bima ya Afya kwa ujumla wake. Kikosi Kazi kimeshakaa na tumepanga mpango kazi wa namna mpya ya kuboresha huduma za afya kutokana na kadi ya CHF.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo tutakayoyafanya ni pamoja na kuweka utaratibu mzuri wa cross subsidization, dhana unayoisema Mheshimiwa inaitwa cross subsidization. Pia tutashughulikia suala la portability ya kadi kwa maana ya kutoka kwenye level moja kwenda kwenye level nyingine kwa maana ya kutoka kwenye level pengine ya wilaya kwenda kwenye level ya rufaa ya mkoa ama kutoka wilaya moja kwenda wilaya nyingine ama kutoka zahanati kwenda kituo cha afya, hiyo inaitwa portability ya hiyo kadi. Hili ni jambo mojawapo ambalo tunalifanyia kazi na tutaliwekea mkakati mahususi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, ni lazima kutakuwa na ongezeko la uchangiaji kwa sababu unapotoka level ya chini kwenda level ya juu gharama za huduma pia zinaongezeka. Tutakapoleta mpango huu tutawashirikisha Wajumbe wa Kamati yetu na Wabunge wote kwa ujumla ili kwa pamoja twende kuwahamasisha wananchi wakubaliane na mpango huu mzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango huu utakuja sambamba na kutafuta namna bora zaidi kwa kulekule kwenye halmashauri kutenga fedha mahsusi kwa ajili ya kulipia Bima ya Afya kwa wazee ili waweze kupewa Kadi za Bima za Afya bure kama ambavyo sera inasema. Kwa maana ya kwamba ni lazima tuwabane walionacho ili tuweze kuwahudumia ambao hawana uwezo wakujihudumia, hiyo ndiyo mikakati ya Serikali. (Makofi)