Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza:- Ulevi wa kupita kiasi hasa wa pombe za kienyeji umekuwa na athari kubwa za kiafya na kiakili kwa Watanzania wenye tabia ya ulevi wa kukithiri:- Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na tatizo hilo hasa ikizingatiwa kuwa Sheria ya Vileo ya mwaka 1969 ni ya zamani sana kiasi kwamba inawezekana kabisa haikidhi mabadiliko ya hali halisi ya vileo kwa wakati huu.

Supplementary Question 1

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na
majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, bado nina swali moja la nyongeza
ambalo linahusiana na hawa watoto wadogo chini ya umri wa miaka 18 kutumia
huu ulevi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile nilisema sheria hii ya mwaka 1969 ni ya
muda mrefu sasa ni lini Serikali itaweza kujipanga na kuleta ili tuweze kufanyia
marekebisho sheria hii ili tuwabane na hawa watoto wadogo walio chini ya umri
wa miaka 18 kutumia ulevi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBUWAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli. Sasa hivi kuna tabia kwenye baadhi ya Mikoa,
utakuta watoto wadogo asubuhi au wakati wa weekend wananyweshwa pombe. Jambo hili kwanza kimsingi ni ukiukwaji wa haki za kibinadamu kwanza
na haki za watoto ambapo mtoto mdogo anatakiwa kuendelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba tuchukue huu ushauri kwa
sababu sheria hii ni ya muda mrefu sana na kutokana na maoni ya wadau
mbalimbali tutaangalia jinsi gani tutafanya turekebishe, lengo kubwa ni
kuhakikisha kwamba Taifa letu linakuwa Taifa imara kwa sababu lazima tuwalee
hawa watoto kwa kizazi kijacho.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba tuchukue ushauri.
Itakapoonekana pale ina haja, basi wadau mbalimbali wataleta maoni yao na
sisi Wabunge ni miongoni mwa wadau wa kutengeneza hizo sheria. Kwa hiyo, hili
nadhani tutalifanyia kazi vema tuweze kulifanikisha.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza:- Ulevi wa kupita kiasi hasa wa pombe za kienyeji umekuwa na athari kubwa za kiafya na kiakili kwa Watanzania wenye tabia ya ulevi wa kukithiri:- Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na tatizo hilo hasa ikizingatiwa kuwa Sheria ya Vileo ya mwaka 1969 ni ya zamani sana kiasi kwamba inawezekana kabisa haikidhi mabadiliko ya hali halisi ya vileo kwa wakati huu.

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa
kuwa katika swali la msingi linazungumzia pombe za kienyeji na pombe za
kienyeji katika Taifa letu ni nyingi ikiwemo mbege, kimpumu, ulanzi na pombe
nyinginezo. Ni lini sasa hawa watu wa viwango vya kuandika kilevi kilichoko
kwenye pombe ikiwemo TBS wataingia katika maeneo husika ili kuweza kujua
kwamba ni kiwango gani cha ulevi kinachoruhusiwa katika pombe za kienyeji?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBUWAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna pombe mbalimbali. Kuna mbege, kuna
ulanzi na nyinginezo, bahati mbaya pombe hizi hazijawekwa katika viwango
stahiki na ndiyo maana maeneo mengine utakuta kuna kesi mbalimbali
zimejitokeza. Baadhi ya watu saa nyingine wamekunywa pombe, pombe ile
imewadhuru na matukio haya tumeona kwamba yametokea maeneo
mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naamini kwa sababu sasa hivi tuna Wizara
ambayo inafanya kazi vizuri zaidi na hususan suala zima la viwanda na naamini
wenzetu sasa wa TBS watachukua jukumu lao katika maeneo mbalimbali
kuhakikisha ni jinsi gani tunafanya kurekebisha utaratibu mzuri hasa katika hivi
vikundi vidogovidogo vinavyojihusisha na pombe za kienyeji, lengo kubwa ni
kumlinda Mtanzania anywe kitu kinachoridhisha maisha yake lakini na afya yake
ya msingi vilevile.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza:- Ulevi wa kupita kiasi hasa wa pombe za kienyeji umekuwa na athari kubwa za kiafya na kiakili kwa Watanzania wenye tabia ya ulevi wa kukithiri:- Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na tatizo hilo hasa ikizingatiwa kuwa Sheria ya Vileo ya mwaka 1969 ni ya zamani sana kiasi kwamba inawezekana kabisa haikidhi mabadiliko ya hali halisi ya vileo kwa wakati huu.

Supplementary Question 3

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru
sana. Kwa kuwa, ulevi wa pombe hizi za kienyeji sasa hivi kumekuwa na
ongezeko la matumizi makubwa sana ya pombe aina ya viroba ambavyo
vifungashio vyake na bei yake imekuwa ni nafuu sana ambapo imepelekea hata
watoto wa shule wanaweza kumudu kati ya shilingi 300 mpaka 500 kuzinunua.
Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kupiga marufuku pombe za viroba ili
kunusuru Taifa hili?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika,
kinachofanyika sasa ni utaratibu, lakini ukweli ulio wazi ni kwamba viroba
vitapigwa marufuku na tutaanzisha packaging ya pombe kali kwenye ujazo
ambao itakuwa ni vigumu kwa mtu kuficha. Watoto wa shule kwa sababu ni
rahisi wanaweza kuficha. Tutaweka kwenye chupa ya glass, ujazo utakuwa
mkubwa kiasi kwamba mtoto ashindwe kununua lakini hata dereva wa daladala
ashindwe kuficha. Ni suala la muda na Waziri wa Mambo ya Mazingira
alizungumzia jana.

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza:- Ulevi wa kupita kiasi hasa wa pombe za kienyeji umekuwa na athari kubwa za kiafya na kiakili kwa Watanzania wenye tabia ya ulevi wa kukithiri:- Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na tatizo hilo hasa ikizingatiwa kuwa Sheria ya Vileo ya mwaka 1969 ni ya zamani sana kiasi kwamba inawezekana kabisa haikidhi mabadiliko ya hali halisi ya vileo kwa wakati huu.

Supplementary Question 4

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.
Sehemu ya swali langu imeshajibiwa lakini naomba niulize. Kwa kuwa sasa hizi
pombe zinatumiwa sana na watu wengi, ni kwa nini Serikali sasa isifikirie kujenga
kiwanda cha kuzisafisha na kuziwekea viwango kama Uganda wanavyofanya
na kile kinywaji cha „Uganda Waragi‟?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya
Serikali ni kuweka mazingira ya uwezeshaji, wanaowekeza ni Sekta Binafsi.
Nichukue fursa hii shangazi, tujasirie kusudi tuweze kukusanya ile konyagi ya
nyumbani, tuiweke kwenye ubora tuweze kuuza. Kila mtu atafute fursa kwake
kusudi aweze kuboresha vile vinywaji ambavyo havina viwango viingie kwenye
viwango, tupate pesa, tutengeneze ajira lakini mwisho wa siku tulipe kodi.