Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. ENG.ATASHASTA J.NDITIYE aliuliza:- Nchi yetu bado ina upungufu mkubwa sana wa sukari na kwa kuwa Wilayani Kibondo kuna ardhi oevu kwenye Bonde la Mto Malagarasi na Lupungu ipatayo ekari 52,000 na wananchi wako tayari kutoa ushirikiano kwa matumizi ya ardhi hiyo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kutafuta mwekezaji wa kiwanda cha sukari katika eneo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. ATASHASTA J.NDITIYE: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru sana, jina langu ni Atashasta Justus Nditiye au Engineer Nditiye inatosha. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wawekezaji wazawa Green Field Plantations walianza mchakato wa kufuatilia eneo hilo toka mwezi wa pili mwaka jana na tuliwapa ushirikiano namshukuru sana Mkuu wa Wilaya pamoja na wananchi wa Jimbo la Muhambwe, lakini ilipofika mwezi wa nane ameondoka mpaka sasa hivi ninapoongea hajarudi. Tunadhani ni muhimu sana tupate mwekezaji competitor kwa ajili ya ku-speed up suala la yeye kuja kufanya shughuli za uwekezaji kama tunavyotarajia ili wananchi wasije wakakata tamaa. Ni lini Serikali inafikiria kutafuta mwekezaji mwingine ikiwezekana hata wa kutoka nje ili kuweza kuwekeza katika Kiwanda cha sukari? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika kuelekea kwenye sera ya viwanda katika nchi yetu tuna wabunifu wengi sana na katika Wilaya yetu ya Kibondo kwa mfano, kuna kijana amebuni magodoro yanayotumia mifuko ya plastic na kila alipojaribu kuwasiliana na COSTECH kwa ajili ya ushauri wamekuwa hawampi ushirikiano wa kutosha. Ni lini Serikali inajipanga kuwaongezea uwezo COSTECH ili wanapopata maswali kutoka kwa wabunifu wadogo wadogo waweze kuwatembelea na kuwapa ushauri? Ahsante.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepata taarifa kwamba hapa mwekezaji aliondoka na hajarejea na kama alivyosema Serikali yetu ya Awamu ya Tano ni Serikali ya viwanda. Tutamleta mwekezaji mwingine kama alivyosema na siyo mmoja bali wawili, watatu kuongeza competition na ufanisi hilo nimelichukua na Serikali inalifanyia kazi, watakuja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ubunifu na COSTECH; kwanza nikiri kwamba huyo mwanafunzi na nimwambie Mheshimiwa Mbunge mwanafunzi huyo ni mwanafunzi wangu niliyemfundisha Masters Chuo Kikuu Mzumbe. Namfahamu na tulimfundisha na sasa anaendelea na ubunifu huo na COSTECH pamoja na Chuo Kikuu Mzumbe tumepanga kumuendeleza mwanafunzi huyo pamoja na wabunifu wote wanaoibuka ndani ya Nchi yetu.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. ENG.ATASHASTA J.NDITIYE aliuliza:- Nchi yetu bado ina upungufu mkubwa sana wa sukari na kwa kuwa Wilayani Kibondo kuna ardhi oevu kwenye Bonde la Mto Malagarasi na Lupungu ipatayo ekari 52,000 na wananchi wako tayari kutoa ushirikiano kwa matumizi ya ardhi hiyo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kutafuta mwekezaji wa kiwanda cha sukari katika eneo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Niongezee kwa hoja ya msingi iliyozungumzwa. Mwekezaji huyo katika Bonde la Malagarasi aliyeko Muhambwe pia yuko mwekezaji mwingine anaitwa Kigoma Sugar yuko Bonde la Malagarasi upande wa Wilaya ya Kasulu. Wote hawa inaonekana wameshindwa na kama sisi Kasulu tunataka ardhi yetu ekari 100,000 tumnyang‟anye sasa tuweze kutafuta mwekezaji mwingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilikuwa naomba basi juhudi hizo za kutafuta mwekezaji zifanyike kote Muhambwe na Wilaya ya Kasulu kwa sababu wote wako kwenye Bonde hilo la Malagarasi. Kwa hiyo, swali langu ni kuomba tu Serikali wawekezaji wote hao wa zamani wameshindwa, hawapo.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme siyo kwa Wilaya ya Muhambwe na Kasulu tu, niseme kwa Wilaya zote na maeneo yote ya uwekezaji na hasa uwekezaji kwa ajili ya kilimo cha miwa pamoja na viwanda vya sukari. Naomba tupatiwe taarifa ili Serikali tuchukue hatua mara moja kama walipewa ardhi basi naamini Waziri wa Ardhi yupo makini tutaichukua ardhi hiyo na kumpa mwekezaji mwingine.
Kwa hiyo, niombe Waheshimiwa Wabunge tupate taarifa ya wawekezaji wote wanaonekana ni wababaishaji na wameshindwa kufanya kazi, tushirikiane na Tanzania ya viwanda inawezekana.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. ENG.ATASHASTA J.NDITIYE aliuliza:- Nchi yetu bado ina upungufu mkubwa sana wa sukari na kwa kuwa Wilayani Kibondo kuna ardhi oevu kwenye Bonde la Mto Malagarasi na Lupungu ipatayo ekari 52,000 na wananchi wako tayari kutoa ushirikiano kwa matumizi ya ardhi hiyo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kutafuta mwekezaji wa kiwanda cha sukari katika eneo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri. Pamoja na Tanzania kwamba tuna maeneo mengi mazuri kwa ajili ya kilimo cha miwa na viwanda tulivyonavyo vya sukari na pamoja na mbwembwe nyingi za Serikali ya Awamu ya Tano iliyonazo kukuza uchumi, lakini bado bei ya sukari katika nchi yetu ni kubwa sana na uwezo wa wananchi wetu ni mdogo. Je, ni lini Serikali itaangalia sasa uwezekano wa kupunguza bei ya sukari ili ifikie angalau pale tulipokuwa na tatizo la sukari wananchi wetu waweze kumudu kununua sukari?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikanushe Serikali ya Awamu ya Tano siyo ya kibabaishaji tunafanya kazi na kama alivyosema Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa tathmini ya mwezi Januari viwanda vyetu vya ndani vimeshazalisha asilimia 86 ya uhitaji wa sukari ndani ya nchi yetu, kwa hiyo, ninauhakika kwa demand na supply nguvu hii tayari tukishaweza kuzalisha asilimia mia moja bei ya sukari itashuka. Tukumbuke tu Waheshimiwa Wabunge nchi hii ni huru na inafuata soko huria, hatuwezi kuingilia hilo na turuhusu sasa Viwanda vyetu viweze kuzalisha asilimia mia moja na bei ya sukari itashuka na wananchi wetu watafurahia Serikali yetu ya Awamu ya Tano utendaji wake.