Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Issa Ali Abbas Mangungu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbagala
Primary Question
MHE. ISSA A. MANGUNGU aliuliza:- Riba kubwa katika benki zetu nchini imekuwa kikwazo kikubwa kwa wanawake na vijana kupata mikopo. (a) Je, Serikali ipo tayari kuandaa utaratibu maalum wa riba elekezi itakayowawezesha wanawake na vijana kupata mikopo benki kwa riba nafuu ili waweze kujikwamua kiuchumi? (b) Je, Serikali itakuwa tayari kuziagiza benki za biashara kulegeza masharti ya dhamana kwa vijana na wanawake ambayo yanarefusha mchakato wa upatikanaji wa mikopo?
Supplementary Question 1
MHE. ISSA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini swali langu la msingi niliuliza ni utaratibu gani mtaweza kuwasaidia makundi maalum ya wanwake na vijana ili waweze kupata mikopo kwa riba nafuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili nilitaka kuuliza, kwa kuwa kuna ugumu na sheria zinazoibana Serikali kusimamia riba hizi. Ni lini sasa Serikali itatusaidia kutimiza ile ahadi ya shilingi milioni 50 kila kijiji na mtaa ili tuweze kuwasaidia wananchi wetu na kinamama wa Tanzania?
Name
Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Kondoa
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi; kwa mujibu wa Sheria Benki Kuu haiwezi kutoa maelekezo ya kuleta riba elekezi ili kuweza kusimamia mabenki haya yaweze kufanya vizuri katika soko letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusu shilingi milioni 50 kama ambavyo Serikali imekuwa ikisema; tunaendelea kuandaa utaratibu na kwenye bajeti yetu ya fedha ya mwaka 2016/2017 tumetenga bajeti hii na tutaweza kuitekeleza kabla ya mwaka huu wa fedha haujaisha.
Name
Sophia Hebron Mwakagenda
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ISSA A. MANGUNGU aliuliza:- Riba kubwa katika benki zetu nchini imekuwa kikwazo kikubwa kwa wanawake na vijana kupata mikopo. (a) Je, Serikali ipo tayari kuandaa utaratibu maalum wa riba elekezi itakayowawezesha wanawake na vijana kupata mikopo benki kwa riba nafuu ili waweze kujikwamua kiuchumi? (b) Je, Serikali itakuwa tayari kuziagiza benki za biashara kulegeza masharti ya dhamana kwa vijana na wanawake ambayo yanarefusha mchakato wa upatikanaji wa mikopo?
Supplementary Question 2
MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa jibu la msingi la Mheshimiwa anasema Benki Kuu haiwezi kuingilia kutoa bei elekezi, tunawezaje kusaidia Benki ya Wanawake iweze kutoa riba ndogo kwa kupata ushauri kutoka kwenye Wizara yake?
Name
Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Kondoa
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema mwanzo, kwa mujibu wa sheria Benki Kuu haiwezi kutoa hiyo riba elekezi na napenda niseme kwamba riba hizi zilizopo ni kwa mujibu wa Sera ya Riba ya mwaka 1992. Kwa hiyo, lazima tuendane na sera tuliyoipitisha humu Bungeni ili kuweza kuhakikisha kwamba sekta ya fedha inafanya vizuri ndani ya uchumi wetu na kwa Benki ya Wanawake naamini Mheshimiwa Waziri wa Afya anaweza kulisimamia hili na kuweza kutoa riba ambayo ni nzuri, lakini hawezi kukiuka misingi ile iliyowekwa na Sera ya Riba ya mwaka 1992.
Name
Anatropia Lwehikila Theonest
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ISSA A. MANGUNGU aliuliza:- Riba kubwa katika benki zetu nchini imekuwa kikwazo kikubwa kwa wanawake na vijana kupata mikopo. (a) Je, Serikali ipo tayari kuandaa utaratibu maalum wa riba elekezi itakayowawezesha wanawake na vijana kupata mikopo benki kwa riba nafuu ili waweze kujikwamua kiuchumi? (b) Je, Serikali itakuwa tayari kuziagiza benki za biashara kulegeza masharti ya dhamana kwa vijana na wanawake ambayo yanarefusha mchakato wa upatikanaji wa mikopo?
Supplementary Question 3
MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia leseni za kufanya biashara katika Manisapa mbalimbali zinatolewa baada ya kupatikana kwa tax clearance, lakini ukweli ni kwamba sio biashara zote hasa biashara ndogo zinahitaji wakati mwingine tax clearance, haioni ni wakati muafaka kuweka categories za biashara ambazo wanaweza kupewa leseni bila hata tax clearance badala ya kinachofanyika sasa?
Name
Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Kondoa
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza hili ni swali la kutoa leseni ambalo ni swali jipya ambalo tumeondoka katika riba, kwa hiyo naomba niseme tu tuna viwango ili kuweza kutoa leseni katika biashara zote zinazoendeshwa ndani ya nchi yetu. Kwa hiyo, kama hawajafikia ndani ya kiwango kile kinachohitajika mfanyabiashara huyo wala hatozwi na wala hapewi leseni lakini akishavuka yale malengo ya biashara yake tayari anatakiwa apewe leseni na tunasimamia kama moja ya njia za kukusanya mapato yetu.
Name
Issaay Zacharia Paulo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbulu Mjini
Primary Question
MHE. ISSA A. MANGUNGU aliuliza:- Riba kubwa katika benki zetu nchini imekuwa kikwazo kikubwa kwa wanawake na vijana kupata mikopo. (a) Je, Serikali ipo tayari kuandaa utaratibu maalum wa riba elekezi itakayowawezesha wanawake na vijana kupata mikopo benki kwa riba nafuu ili waweze kujikwamua kiuchumi? (b) Je, Serikali itakuwa tayari kuziagiza benki za biashara kulegeza masharti ya dhamana kwa vijana na wanawake ambayo yanarefusha mchakato wa upatikanaji wa mikopo?
Supplementary Question 4
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Pamoja na mafanikio makubwa ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuwezesha elimu bure, upatikanaji wa madawati na pia watumishi hewa kuondolewa, naomba kufahamu, kwa sasa Watanzania wengi hasa akinamama katika SACCOS zao wamekuwa na hamu kubwa ya kufanya biashara. Je, Serikali inachukua hatua gani kuwezesha SACCOS za akinamama katika halmashauri zote zipate hela za kutosha?
Name
Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Kondoa
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ikumbukwe kwamba sote humu ndani Waheshimiwa Wabunge sisi ni Wajumbe katika Mabaraza yetu ya Halmashauri, hivyo tunatoa asilimia tano katika mapato ya halmashauri na hayo ni katika kuimarisha vikundi vyetu vya VICOBA pamoja na SACCOS zilizopo ndani ya halmashauri zetu. Nitoe wito tu kwa Waheshimiwa Wabunge, tusimamie kwa ufasaha asilimia hizo tano za mapato ndani ya Halmashauri zetu ili ziweze kuwafikia wananchi wetu hasa akina mama na vijana ili kuweza kuinua uchumi wao.