Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE.VEDASTUS M. MANYINYI aliuliza:- Baada ya Serikali kutoa tamko la elimu bure wananchi wamekuwa wagumu sana kutoa michango mbalimbali ya kuboresha elimu. Je, Serikali ina mikakati gani ya kumaliza tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa na vyumba vya maabara katika shule za msingi na sekondari?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani ilijigamba kwamba itatoa elimu bure na utekelezaji wa elimu bure kwa mujibu wa watafiti wa haki elimu inahitaji takribani shilingi bilioni 700 kwa mwaka mmoja wa fedha. Na hali ilivyo sasa hivi, fedha mnazopeleka ni kidogo tu za fidia ya ada.
Je, mko tayari sasa kuwaambia Watanzania mmeshindwa kutekeleza elimu bure ili Watanzania wachangie suala la elimu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Watanzania wanafahamu. Wakati hatuna programu ya elimu bure, vijana wengi walikuwa wanakosa hata hii elimu ya msingi, wengine walikuwa wanatishwa vitumbua kwenda kuuza barabarani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi juzi nilipita kule katika Mkoa wa Kagera, nilipofika pale Nyakanazi, shule ambayo mwaka huu ime-register wanafunzi wengi zaidi ya wanafunzi 800 wa shule ya msingi peke yake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitendo cha kutoa elimu bure hii kusaidia mitihani, gharama za ada, hata suala zima la posho, ni jambo kubwa sana. Mimi naamini ndio maana kwa rekodi mwaka huu inatuonesha vijana wengi sasa hivi wanaripoti shule za seondari ukilinganisha na kipindi cha mwanzo, kwa sababu mwanzo wazazi walikuwa wanashindwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kikubwa zaidi naomba tuamini kwamba Serikali katika jambo hili imeleta ukombozi mkubwa. Na hili niseme kwa vile Serikali tumejipanga na hili nimelisema sehemu mbalimbali, changamoto yetu inatufanya tunataka tuseme lazima private schools sasa si muda mrefu zitatakiwa zijipange vizuri, kwa sababu tunaenda kwa kasi kubwa ya ajabu. Huku tunakokwenda tutakwenda kupata mafanikio makubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, imani yangu Watanzania wote tutaungana pamoja, hii nchi yote ni ya kwetu, Watanzania wote ni wa kwetu na watoto ni wa kwetu tusaidiane kuhakikisha Tanzania inafika mahali salama katika suala zima la utoaji wa elimu.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE.VEDASTUS M. MANYINYI aliuliza:- Baada ya Serikali kutoa tamko la elimu bure wananchi wamekuwa wagumu sana kutoa michango mbalimbali ya kuboresha elimu. Je, Serikali ina mikakati gani ya kumaliza tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa na vyumba vya maabara katika shule za msingi na sekondari?

Supplementary Question 2

MHE.VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, na ameendelea kusema hapa kwamba hii michango tunahitaji kuendelea kuwahamasisha wananchi ili waweze kuchangia. Lakini ukiangalia kwa mapungufu tuliyokuwanayo kwa maana ya madawati, vyumba vya madarasa pamoja na maabara; ni mapungufu makubwa sana na kwa sababu wananchi wengi wanaamini kwamba michango ni hiari kama alivyosema Naibu Waziri, hatuoni kama tutashindwa kutekeleza azma yetu ya kuhakikisha kwamba wanafunzi wote wanaweza kupata elimu bora kwa sababu wanafunzi wengi wataendelea kukosa vyumba vya madarasa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tunatambua kwamba wazazi pamoja na shughuli kubwa wanazozifanya pamoja na kujenga hostel, lakini bado ukiangalia wale wanafunzi wa kike zile gharama zote za kuwasomesha kwenye zile hostel bado ni gharama za wazazi. Ni kwa nini Serikali isikubali kugharimia hizo gharama za hostel baada ya kuwa hizi hostel zimejengwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mathayo kwa sababu katika rekodi pale juzi juzi ameweza kushiriki utoaji wa mifuko 200 ya cement kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika eneo lake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefika pale Musoma Mjini, nimeweza kutembelea nimeona kazi kubwa anayofanya. Kwa hiyo, imani yangu kwa ile kazi unayoifanya na nadhani mnataka mjenge takribani vyumba karibuni 200 vinatakiwa vikamilike ndani ya mwezi Machi, naomba tuwaunge mkono kwa sababu mnafanya kazi njema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa kusema kwa mkakati huu tutashindwa, naomba nikuhakikishie ndio maana mwaka huu tunakamilisha vyumba vingi kwa kutenga karibu shilingi bilioni 29, na ndugu zangu Wabunge naomba niwaambie huku site tunakotoka sasa hivi ukienda huko utakuta kazi kubwa sana ya ujenzi wa madarasa inaendelea. Naamini katika muda huu ambao tuko hapa Bungeni, Mbunge mwingine akirudi katika site kwake atakuta kwamba kuna madarasa mengine katika eneo lake hata alikuwa hajatarajia yameshakamilika. Hii yote ni juhudi ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba niwahakikishie Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tutajitahidi kuhakikisha azma ya Serikali kuwapatia wananchi wake elimu bora inafanikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala zima la zile hostel zilizojengwa changamoto ni kubwa sana, katika suala la vijana hasa watoto wetu wa kike kwamba ikiwezekana kwamba zile hostel zilizojengwa Serikali igharamie. Naomba niseme hili ni wazo ngoja tutalifanyia kazi, kwa sababu kugharamia hostel zote Tanzania ni bajeti kubwa sana na hizi zimejengwa makusudi ni hostel za kata ziko katika maeneo yetu. Lengo ni mtoto anaenda shuleni na kurudi lakini kwa sababu changamoto ya uzito kwa wanafunzi ni vyema tujenge hostel nasema tuendelee na mpango huu wa sasa pale Serikali kwa kushirkiana na wadau mbalimbali itakavyoona kwamba nini tufanye, lengo ni kuboresha wananchi katika kata zetu tutafanya hivyo kwa kadri inavyowezekana.