Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU aliuliza:- Walimu wamekuwa wakiidai Serikali stahiki zao mbalimbali na tatizo hili la kutowalipa kwa muda muafaka limekuwa likijirudia rudia:- (a) Je, walimu wanadai stahiki zipi na kwa kiasi gani? (b) Je, Serikali imejipangaje kutatua tatizo hilo na kulimaliza kabisa?

Supplementary Question 1

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka nenda, miaka rudi tofauti na kada nyingine za watumishi, kero imekuwa madeni ya walimu, madeni ya walimu. Leo hii mnatuambia kwamba madeni ya walimu yamefikia takribani shilingi bilioni 34 plus. Walimu hawa wanaidai Serikali wengine kama matibabu, likizo, kwa miaka zaidi ya mmoja hadi miwili. Walimu waliopandishwa mishahara miezi 12 iliyopita hadi leo hawajalipwa huo mshahara wanausikia harufu tu. Walimu wengine wamestaafu zaidi ya miezi sita hawajapata mafao yao.
Ningependa kujua kwa kuwa sasa hivi Serikali mnasema mmeshahakiki ni lini, na mnipe tarehe na mwezi hawa walimu watakuwa wamelipwa haya madeni kwa sababu wamechoka kila siku madeni ya walimu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuna walimu waliosimamia mitihani mwaka 2015. Leo hii tunazungumza mwaka 2017, kwa nini hadi leo hawajalipwa na ni lini Serikali itakuwa imewalipa hiyo stahili yao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema awali, kwanza tuweke kumbukumbu vizuri. Katika kada ambayo Serikali katika njia moja ua nyingine imekuwa ikishiriki vizuri sana katika ulipaji wa madeni ni kada ya walimu. Ukiangalia miaka mitatu mfululizo, trend ya malipo ya madeni ya walimu ambayo tulikuwa tumezungumza hapa katika Bunge kila wakati, kwa kweli Serikali inajitahidi sana. Na ndio maana katika kipindi cha sasa hata ukiangalia katika mwezi wa 11 uliopita huu kuna baadhi ya madeni ya walimu especially katika baadhi ya Wilaya, Halmashauri, kwa mfano kuna Temeke na Halmashauri zingine kulikuwa na outstanding deni karibuni ya shilingi bilioni moja nayo ililipwa vilevile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio maana katika ulipaji wa madeni mapya mengine; ndio maana Serikali ilikuwa inafanya zoezi zima la uhakiki. Na bahati nzuri, ofisi yetu ya TAMISEMI pamoja na Ofisi ya Hazina ndio ilishiriki, na jambo hili sasa hivi limekamilika. Na ndio maana nimesema hapa siwezi kutoa deadline ni lini, deni hilo litalipwa lakini kwa sababu mchakato wa uhakika umekamilika, hili deni la shilingi bilioni 26 ninaamini sasa hazina si muda mrefu mchakato wa malipo utaanza kuanza.
Naomba Mheshimiwa Mbunge, najua uko makini katika hili lakini amini Serikali yako kwa vile zoezi la uhakiki ambalo lilikuwa ni changamoto limekamilika basi walimu hawa si muda mrefu wataweza kulipwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala zima la deni la kusimamia mitihani na ndio maana nilisema deni hili lilikuwa ni miongoni mwa madeni haya ambayo yaliyohakikiwa ambayo takribani ilikuwa ni shilingi bilioni sita.
Naomba tuondoe hofu walimu wangu katika mchakato wa sasa walimu hawa wote wataendelea kulipwa ili mradi kila mtu haki yake iweze kulipwa, na Serikali haitosita kuhakikisha inawahudumia vyema walimu wake kwa sababu italeta tija kubwa sana katika sekta ya elimu.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU aliuliza:- Walimu wamekuwa wakiidai Serikali stahiki zao mbalimbali na tatizo hili la kutowalipa kwa muda muafaka limekuwa likijirudia rudia:- (a) Je, walimu wanadai stahiki zipi na kwa kiasi gani? (b) Je, Serikali imejipangaje kutatua tatizo hilo na kulimaliza kabisa?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa kuna watumishi ambao walipandishwa daraja kama alivyosema muuliza swali wa kwanza, na kupokea mshahara mpya mwaka jana; na kisha hiyo mishahara ikasitishwa na sasa hivi watumishi hawa ambao ni walimu na watumishi wa afya kuna baadhi yao wameshastaafu, na wengine wanatarajia kustaafu miezi ijayo hii.
Je, Serikali itatumia hesabu gani katika ku-calculate, itatumia mshahara upi? Ule wa zamani au mshahara mpya katika kukokotoa kile kiinua mgongo cha mwisho? Ahsante sana.

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kwa watumishi ambao walikuwa wameingia katika utumishi wa umma, halafu baadaye wakaambiwa warudi nyumbani, tumeshawarudisha watumishi 421 na kwa sasa tayari wameshalipwa takribani watumishi 379, 42 tumewarudishia waajiri wao ili waweze kukamilisha baadhi ya taratibu za ajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hoja yake ya pili kwamba unakuta wengine wameshastaafu, lakini ni kiwango gani kitatumika katika kukokotoa mafao yao? Nipende tu kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge na wote wanaosikiliza, kwa wale ambao wanastaafu wanapewa kipaumbele miezi miwili kabla ya tarehe ya kustaafu mishahara yao inarekebishwa na watakuwa wamepata katika cheo stahiki ili waweze kutokuathirika na mafao.

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU aliuliza:- Walimu wamekuwa wakiidai Serikali stahiki zao mbalimbali na tatizo hili la kutowalipa kwa muda muafaka limekuwa likijirudia rudia:- (a) Je, walimu wanadai stahiki zipi na kwa kiasi gani? (b) Je, Serikali imejipangaje kutatua tatizo hilo na kulimaliza kabisa?

Supplementary Question 3

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nina swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, madai ya walimu yasiyo ya mshahara ni pamoja na deni la walimu kwa Serikali juu ya posho na kufundishia yaani teaching allowance ambayo ni ahadi ya Serikali tangu mwaka 2012 ambayo ilitolewa kule Mtwara siku ya Walimu Duniani.
Je, Serikali ina mkakati gani wa ziada kuweza kuwalipa na kuwapatia fedha zao walimu hawa deni wanalolidai, posho la kufundishia yaani teaching allowance kwa haraka inavyowezekana?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA YA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, kwa hali ya sasa tunachokifanya ni kuhakikisha kwa kadri iwezekano kusaidia sekta ya elimu. Ndio maana kabla sijajibu hili swali sasa hivi ukiangalia Serikali yetu kwa kazi kubwa waliyoifanya sasa hivi, mwanzo ukiangalia Walimu Wakuu, hata Waratibu wa Elimu mwanzo walikuwa hawalipwi hizi allowances.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Serikali hivi sasa toka mwaka jana kuanzia Waratibu wa Elimu, Wakuu wa Shule za Msingi na Wakuu wa Shule za Sekondari hivi sasa wote wanalipwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kama kuna madeni mengine yoyote Serikali iko katika michakato mbalimbali kuyalipa madeni haya yote. Naomba niwahakikishie ndugu zangu Wabunge kwamba Serikali yetu jukumu letu kubwa ambalo tunalilenga sasa hivi, kwa sababu tunataka kuhakikisha ubora wa elimu lazima madeni haya yote yatalipwa na kama nilivyosema madeni yote ambayo yamehakikiwa kupitia Hazina yatalipwa madeni hayo. Tunataka walimu wetu wawe na morali ya kufanya kazi katika mazingira yao ya kazi.