Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasmine Tiisekwa Bunga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Vyuo Vikuu

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Chuo Kikuu cha Mzumbe ni chuo kikongwe chenye historia tangu mwaka 1953 kipindi cha ukoloni na mwaka 1972 kupandishwa hadhi kuwa Chuo cha Uongozi wa Maendeleo (IDM) kikiwa na miundombinu ya kukidhi wanafunzi wasiozidi 1,000. Kwa sasa chuo hiki kina jumla ya wanafunzi 11,282 ambapo idadi hii ni sawa na ongezeko la 874.3% wakati hali ya majengo na miundombinu kwa kiasi kikubwa bado ni ile ile ya mwaka 1972:- Je, ni lini sasa Serikali itaanza kujenga miundombinu mipya ikiwemo madarasa, mabweni, ofisi za Wahadhiri, jengo la utawala na kadhalika ili kukidhi mahitaji ya ongezeko kubwa la wanafunzi na Wahadhiri waliopo na watakaokuja na kukifanya chuo hiki chenye historia kubwa kiwe na taswira ya chuo cha kisasa na hadhi ya kimataifa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukarabati unahitaji fedha za kutosha na Chuo Kikuu cha Mzumbe kwa muda mrefu kina madai halali sana kutoka Serikalini ambapo chuo kinaidai Serikali kama vile fedha za ada kutoka Bodi ya Mikopo. Fedha hizi zingeletwa mapema zingeweza kusaidia kufanya ukarabati. Je, ni lini sasa Serikali itaweza kulipa madeni haya ili Chuo Kikuu cha Mzumbe kiweze kufanya marekebisho haya madogo madogo na kukifanya chuo hiki kiweze kuwa na muonekano mzuri kuliko ilivyo sasa hivi?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kama ambavyo amezungumza Mheshimiwa Mbunge Dkt. Jasmine ni kweli kuna umuhimu mkubwa sana wa kufanya marekebisho katika chuo hiki, lakini pia katika suala la ada kuna wakati tulikuwa tumeagiza vyuo vyote kufanya uhakiki hasa kwa wale wanafunzi ambao walikuwa hawastahili kupata mikopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, Mheshimiwa Waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mheshimiwa Profesa Joyce Ndalichako, alishatoa maagizo kwamba Bodi ya Mikopo ipeleke fedha hizo wakati uhakiki ukiwa unaendelea ili wasikwamishe shughuli zinazoendelea. Kwa hiyo, naamini muda wowote ule hizo fedha watakuwa wamezipata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Serikali imedhamiria kuona kwamba vyuo vyote vikuu vinaongezewa fedha ili kuongeza udahili unaostahili kwa wanafunzi ili kwenda kusoma kwenye chuo binafsi iwe ni hiyari zaidi ya mwanafunzi kuliko kuwa ni sababu ya kukosa nafasi katika vyuo vyetu vya Serikali. Kwa hiyo, naamini mpango huu ukikamilika hali itazidi kuwa nzuri zaidi kwa vyuo vyote ikiwepo Mzumbe.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Chuo Kikuu cha Mzumbe ni chuo kikongwe chenye historia tangu mwaka 1953 kipindi cha ukoloni na mwaka 1972 kupandishwa hadhi kuwa Chuo cha Uongozi wa Maendeleo (IDM) kikiwa na miundombinu ya kukidhi wanafunzi wasiozidi 1,000. Kwa sasa chuo hiki kina jumla ya wanafunzi 11,282 ambapo idadi hii ni sawa na ongezeko la 874.3% wakati hali ya majengo na miundombinu kwa kiasi kikubwa bado ni ile ile ya mwaka 1972:- Je, ni lini sasa Serikali itaanza kujenga miundombinu mipya ikiwemo madarasa, mabweni, ofisi za Wahadhiri, jengo la utawala na kadhalika ili kukidhi mahitaji ya ongezeko kubwa la wanafunzi na Wahadhiri waliopo na watakaokuja na kukifanya chuo hiki chenye historia kubwa kiwe na taswira ya chuo cha kisasa na hadhi ya kimataifa?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN J. A. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Katika siku hizi za karibuni, Tanzania tumepata sifa kubwa sana ya kuwa na chuo kikubwa sana Afrika Mashariki na Kati, Chuo Kikuu cha Dodoma; na chuo hiki kinaweza kuchukua takribani wanafunzi 40,000. Kwa mshangao mkubwa sana, leo Serikali ya Chama cha Mapinduzi imeamua kufanya Chuo Kikuu cha Dodoma kuwa sehemu ya majengo ya Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua, Serikali kwa kuleta utaratibu wa kubadili au wa kuchanganya wanafunzi na majengo ya Serikali (Wizara), maana yake ni kwamba tunachukua wanafunzi wetu kuwapekeleka kwenye simba. Nataka kujua huu ndiyo utaratibu wa kuhamia Dodoma kwa maana ya kubadilisha miundombinu ya elimu kuwa Ofisi za Serikali? Naomba majibu.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kumfahamisha Mheshimiwa Suzan Lyimo kwamba pamoja na hayo aliyoyazungumza, ukweli ni kwamba chuo maana yake siyo majengo peke yake. Chuo maana yake ni majengo, Walimu pamoja na vitendea kazi vingine vya kufundisha na kufundishia. Kwa hali hiyo Chuo cha UDOM kilipojengwa kilijiwekea utaratibu wa namna gani kitakuwa kinakua sambamba na majengo. Kwa hiyo, kwa taasisi au Wizara kuhamia katika majengo haya ni kwa vile ni suala la muda mfupi na kwa sababu majengo hayo yalitokana na…
Kulingana na utaratibu na mipango yake ya kukua yalikuwa kwa sasa hayatumiki. Wizara zinatafutiwa maeneo yake ya kujenga, CDA wakishakamilisha kuleta viwanja hivyo, kila Wizara itakuwa na majengo yake katika eneo lake.
Kwa hiyo, niwaombe tu kwamba suala la kuhamia Dodoma, sisi kwetu tunaona ni suala lenye tija na litaongeza ufanisi mkubwa hasa kwa wananchi wetu kwa sababu sasa watakuwa wanapata huduma kiurahisi zaidi, ikizingatiwa kwamba Dodoma hata foleni hakuna na ni Makao Makuu ya nchi. Kwa hiyo, sisi Wizara tumejipanga na tutahakikisha kwamba tutahamia kwenye maeneo yetu muda ukifika.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri aliyoyatoa hapa ndani ya Bunge. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, naomba niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge kwamba nia ya Serikali katika kukiendeleza Chuo cha Dodoma ilijidhihirisha kutokana na nia njema ya Chama cha Mapinduzi kutoa ukumbi wake na kubadilisha matumizi kutoka kwenye matumizi ya Chama kuwa Chuo Kikuu cha Watanzania wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hatua hiyo hiyo ya nia njema ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi, tunaendelea na mpango wa Taifa wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya kuhamishia Serikali Dodoma. Naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge Majengo yatakayotumika na Serikali ni majengo ambayo Serikali ya Chama cha Mapinduzi ilishayajenga na yakawa mengi. Kwa sababu majengo yale ni mengi na yamejengwa na Serikali hii, badala ya kuyaacha yaharibike bila kutumika, yatatumika na baadhi ya Wizara za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, majengo yale hayaingiliani na shughuli zozote za elimu pale UDOM. Nawahakikishia Watanzania wote, nazipongeza Wizara hizo kwa kuyalinda kwa kuyatumia majengo hayo.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Chuo Kikuu cha Mzumbe ni chuo kikongwe chenye historia tangu mwaka 1953 kipindi cha ukoloni na mwaka 1972 kupandishwa hadhi kuwa Chuo cha Uongozi wa Maendeleo (IDM) kikiwa na miundombinu ya kukidhi wanafunzi wasiozidi 1,000. Kwa sasa chuo hiki kina jumla ya wanafunzi 11,282 ambapo idadi hii ni sawa na ongezeko la 874.3% wakati hali ya majengo na miundombinu kwa kiasi kikubwa bado ni ile ile ya mwaka 1972:- Je, ni lini sasa Serikali itaanza kujenga miundombinu mipya ikiwemo madarasa, mabweni, ofisi za Wahadhiri, jengo la utawala na kadhalika ili kukidhi mahitaji ya ongezeko kubwa la wanafunzi na Wahadhiri waliopo na watakaokuja na kukifanya chuo hiki chenye historia kubwa kiwe na taswira ya chuo cha kisasa na hadhi ya kimataifa?

Supplementary Question 3

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwanza, naishukuru Wizara ya Elimu iliweza kutoa fedha kwa ajili ya ukarabati wa Chuo cha Ualimu pale Korogwe ambapo kilileta wanachuo karibu 800 na kitu kwa ajili ya mafunzo pale. Hata hivyo, naiomba Serikali, kwa kuwa chuo kile kina maktaba ndogo na sisi wananchi tumeweza kujenga maktaba kubwa ambayo ingeweza kuwasaidia wanachuo ambao ni wengi sasa pale chuoni, pamoja na wananchi wa Korogwe kwa ujumla: Je, Serikali itakuwa tayari kutupa fedha ili tuweze kukamilisha lile jengo la maktaba?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Chatanda kwa kufuatilia masuala ya kielimu na Mheshimiwa Mbunge anapofanya jitihada kama hizo sisi Serikali tunao wajibu wa kusaidia. Kwa hiyo, tutachukua hilo jukumu la kusaidiana nao kuhakikisha maktaba hiyo inakamilika vizuri.

Name

Suleiman Ahmed Saddiq

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:- Chuo Kikuu cha Mzumbe ni chuo kikongwe chenye historia tangu mwaka 1953 kipindi cha ukoloni na mwaka 1972 kupandishwa hadhi kuwa Chuo cha Uongozi wa Maendeleo (IDM) kikiwa na miundombinu ya kukidhi wanafunzi wasiozidi 1,000. Kwa sasa chuo hiki kina jumla ya wanafunzi 11,282 ambapo idadi hii ni sawa na ongezeko la 874.3% wakati hali ya majengo na miundombinu kwa kiasi kikubwa bado ni ile ile ya mwaka 1972:- Je, ni lini sasa Serikali itaanza kujenga miundombinu mipya ikiwemo madarasa, mabweni, ofisi za Wahadhiri, jengo la utawala na kadhalika ili kukidhi mahitaji ya ongezeko kubwa la wanafunzi na Wahadhiri waliopo na watakaokuja na kukifanya chuo hiki chenye historia kubwa kiwe na taswira ya chuo cha kisasa na hadhi ya kimataifa?

Supplementary Question 4

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi, nami naomba niulize swali dogo la nyongeza kuhusu Chuo Kikuu cha Mzumbe. Kwa kuwa Serikali inaongeza wanafunzi kila mwaka; na kwa kuwa kuna ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipokuja Mzumbe kwamba Serikali itatoa fedha kwa ajili ya Ofisi za Walimu na nyumba za wafanyakazi; na kwa kuwa ahadi hiyo hadi leo haijatekelezwa.
Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne pamoja na kuongeza nyumba za watumishi pale main campus Mzumbe?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo ilielezwa hapo awali, niseme tu kwamba katika Vyuo Vikuu ambavyo vina kipaumbele katika uongezaji wa miundombinu kwa mwaka huu unaokuja wa fedha 2017/2018 ni pamoja na Chuo Kikuu cha Mzumbe. Kwa hiyo, naomba ajue hilo.