Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPH O. MBILINYI aliuliza:- Kumekuwa na tabia za watu kupiga watu wengine hovyo kila siku, vipigo hivyo vinafikia kiasi cha utesaji (torture) kama ilivyotokea Mbeya Sekondari kwa walimu kumshambulia mwanafunzi au mtu kumtoa macho kama ilivyotokea huko Buguruni na maeneo mengine:- (a) Je, Serikali inaona mateso haya wanayopata Watanzania kutoka kwa Watanzania wenzao? (b) Je, Serikali inachukua hatua gani ili kuwalinda wananchi na vitendo hivi vya kikatili?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wanasema mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, napenda niipongeze Serikali kwa kukubali kwamba kuna tatizo la utesaji na torture kwa sababu siku hizi kumekuwa na utaratibu na utamaduni wa kukataa na kukanusha kila kitu. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa kukubali kwamba kuna tatizo la utesaji na torture. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali langu limejibiwa kwa wepesi na ujumla sana. Kwenye swali langu la msingi nili-cite kwa mfano, kinachoendelea kuhusu Mwalimu Msigwa na wenzake ambao walimfanyia torture au shambulio la kudhuru mwanafunzi wa Mbeya Sekondari ambapo mpaka leo hii wazazi wana hofu na watoto wao katika shule ile kiasi kwamba wanamsukuma Mbunge kutaka kujua ni nini hatma ya wale walimu kwa sababu maneno yamekuwa mengi. Mara wanasema amri kutoka juu imesema kwamba waachiwe na kadhalika...
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimejiuliza sana na juzi nimeuliza kwenye Kamati lakini Waziri wa Elimu anasema hana habari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi nimeuliza kwenye Kamati wanasema chuo kimeunda tume, chuo kinafanya uchunguzi wa jinai toka lini wakati suala hili liko wazi kwenye video ilienda viral wale walimu walitesa watoto tunawatetea walimu lakini wanapovunja sheria ni lazima hatua zichukuliwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka kujua ni nani aliyetoa amri kwamba wale walimu waachiwe wasichukuliwe hatua za kisheria kwa kosa la jinai walilofanya? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika Watanzania wanaowatesa wenzao ni pamoja na Polisi. Watanzania hawa Polisi, kwa mfano wakati wa Operesheni UKUTA ambayo tuliisitisha kwa maslahi ya Taifa, walikamata watu, waka-torture mfano Mtanzania Nyagali maarufu kama Mdude wa Mbozi ambaye mpaka leo hii amevunjwa miguu na hayuko sawasawa. Sasa Taifa hili limekuwa Taifa la disappearance watu wanapotea...
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nijue kwa nini isiundwe Tume ya Kimahakama kama ile aliyounda Mheshimiwa Kikwete ya kuchunguza Operesheni TOKOMEZA ili kuchunguza maovu haya yanayofanywa na Watanzania ambao wana uniform za kipolisi? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala la walimu ambao wamewanyanyasa wanafunzi kwenye shule ya Mbeya Day niseme ni mtambuka kwa hiyo hatua mbalimbali zinachukuliwa na mamlaka husika. Kwa upande wa Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Mashtaka DPP kuna hatua ambazo zinaendelea kuchukuliwa na pale ambapo ushahidi na uchunguzi utakapokamilika watafikishwa katika vyombo vya sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ni kuhusu kuundwa Tume ya UKUTA, kwanza tulishazungumza mapema kwamba mkusanyiko wowote ambao si halali hautaruhusiwa na hivyo Jeshi la Polisi litasimamia kuhakikisha kwamba linalinda usalama wa nchi hii kwa kuzuia mikusanyiko yoyote ambayo siyo halali. Kwa hiyo, kama ikiwa Jeshi la Polisi limetekeleza majukumu yake kuzuia mkusanyiko ambao si halali limefanya hivyo katika kutekeleza majukumu ya kawaida na tunawasihi wananchi pale wanapoelekezwa kutii sheria za nchi, basi watii sheria za nchi.

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH O. MBILINYI aliuliza:- Kumekuwa na tabia za watu kupiga watu wengine hovyo kila siku, vipigo hivyo vinafikia kiasi cha utesaji (torture) kama ilivyotokea Mbeya Sekondari kwa walimu kumshambulia mwanafunzi au mtu kumtoa macho kama ilivyotokea huko Buguruni na maeneo mengine:- (a) Je, Serikali inaona mateso haya wanayopata Watanzania kutoka kwa Watanzania wenzao? (b) Je, Serikali inachukua hatua gani ili kuwalinda wananchi na vitendo hivi vya kikatili?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa kumekuwa na tabia ya wananchi au vyombo vya ulinzi na usalama na wengine ambao wanakwenda kwenye mafunzo ambayo siyo halali kutesa raia wasiokuwa na hatia na kuwasababishia maumivu makali na hatimaye kupelekwa rumande bila kupatiwa huduma za kiafya. Je, Serikali hamuoni kama mnavunja haki za binadamu na utawala bora?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la Mheshimiwa Maryam Msabaha liko too general, nadhani si sahihi kusema Polisi kazi yao ni kutesa raia. Polisi wamekuwa wakifanya kazi ya kulinda raia na kazi hii imefanyika kwa mafanikio makubwa sana na ndiyo maana mpaka leo nchi yetu iko salama. Ningemwomba Mheshimiwa Maryam Msabaha kama ana tukio specific ambalo linamhusisha Polisi kwa kufanya tendo lolote ambalo limekwenda kinyume na sheria basi aliwasilishe ili hatua zichukuliwe.

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH O. MBILINYI aliuliza:- Kumekuwa na tabia za watu kupiga watu wengine hovyo kila siku, vipigo hivyo vinafikia kiasi cha utesaji (torture) kama ilivyotokea Mbeya Sekondari kwa walimu kumshambulia mwanafunzi au mtu kumtoa macho kama ilivyotokea huko Buguruni na maeneo mengine:- (a) Je, Serikali inaona mateso haya wanayopata Watanzania kutoka kwa Watanzania wenzao? (b) Je, Serikali inachukua hatua gani ili kuwalinda wananchi na vitendo hivi vya kikatili?

Supplementary Question 3

MHE FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mbali na kujitokeza watu ambao wanawanyanyasa binadamu wenzao kwa kuwapiga lakini kuna baadhi ya watu hususani kule Pemba wanachoma mashamba ya mikarafuu, wanawapiga watu na kuwachomea nyumba. Je, Serikali imechukua hatua gani ya kuwalipa fidia watu waliodhalilishwa kwa matukio kama hayo? Vilevile imewachukulia hatua gani wahalifu hao?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwepo na matatizo ya wananchi kujichukulia sheria mkononi na hili si tu kwenye mikarafuu lakini tumeshuhudia hata kwenye upande wa wakulima na wafugaji. Tamko letu kama Wizara na kama Serikali tunasema hakuna sababu yoyote ile inayotosha kuhalalisha mwananchi kuchukua sheria mkononi dhidi ya mwenzake iwe kwa kudhuru maisha yake ama kwa kudhuru mali zake. Yeyote atakayefanya hivyo tumesema atafika kwenye mkono wa sheria na wale ambao walishafanya hivyo tumesema wachukuliwe hatua ili iwe mfano na kwa wengine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeelekeza na Waheshimiwa Wabunge nawaomba kwenye hili tukubaliane, ili Serikali ionekane ipo na inatetea wale wanaoonewa tutachukua hatua kali kwa wale wanaofanya vitendo hivi vya kihalifu dhidi ya wenzao. Hii ndiyo itakuwa njia pekee ya kuweza kuhakikisha kwamba wananchi hawajichukulii sheria mkononi kwa sababu duniani kote sheria isipochukua mkondo wake ndipo wananchi huchukua sheria mkononi.