Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Ni Sera ya Taifa kuwa na Chuo cha Ufundi katika kila Wilaya:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha Ufundi katika Wilaya ya Geita?

Supplementary Question 1

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nianze kushukuru kwa ajili ya majibu, vilevile maandalizi ya ujenzi wa hiki Chuo cha VETA, Mkoa wa Geita ni wa muda mrefu, ni tangu awamu iliyopita, lakini mpaka sasa ujenzi haujaanza. Ningependa kujua Mheshimiwa Waziri amesema utaanza hivi mapema, ni lini? Je, ni katika mpango wa mwaka huu wa 2016/2017?
Swali la pili, kwa kuwa tunaelekea kwenye viwanda, Awamu ya Tano ni awamu ya viwanda na vijana wetu hasa katika Mkoa wa Geita na Wilaya ya Geita hawana ujuzi kabisa, Serikali inasemaje kuanzisha program maalum kupitia SIDO, kwamba vijana wetu sasa waanze kuelimishwa ili viwanda vikianza waweze kuajiriwa?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kumshukuru kwa shukrani alizotupa. Pili, nikubaliane naye kwamba mchakato huu umeanza muda mrefu, hata hivyo tunapozungumzia kuanza kwa ujenzi, nina maana ni hatua zote zinazohusika ili kuwezesha ujenzi huu. Kama ambavyo tumekuwa tukizungumza hapo awali, chuo hiki kinategemewa kujenga kwa fedha za mkopo kutoka ADB, kwa hiyo, kuna taratibu ambazo lazima zifuatwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza la muhimu ilikuwa ni kupata hati na kiwanja ambacho kiko mahali pazuri ambapo wanachuo wengi watapenda kwenda hapa na pia itakuwa rahisi kufikika kazi hiyo imekamilika, sasa hivi tunaendelea na hatua za kumpata mshauri elekezi, tunaamini hatua hizi hazitakuwa na utata mkubwa kwa sababu ziko wazi na zinakwenda kwa taratibu zilizopo tukishakamilisha ndipo tukakapoanza ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili kuhusiana na tatizo la upungufu wa wataalam hasa katika azma ya kwenda uchumi wa viwanda. Ni kweli kabisa vijana wetu wengi wanamaliza darasa la saba, form four na vyuo, wanahitaji ujuzi. Kupitia ziara hiyo niliweza kutembelea maeneo mbalimbali vikiwemo Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi ambavyo navyo vinaonekana kuwa na mchango mkubwa katika kutoa mafunzo haya ya ufundi. Wizara tumeshajipanga kuona kwamba vyuo hivyo vinakarabatiwa na kuongezewa vifaa ili vijana wengi zaidi waweze kunufaika.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Ni Sera ya Taifa kuwa na Chuo cha Ufundi katika kila Wilaya:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha Ufundi katika Wilaya ya Geita?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Matatizo yaliyopo kwenye hii Wilaya ya Busanda yanafanana kabisa na yale yaliyoko katika Wilaya ya Liwale. Wilaya ya Liwale hatuna Chuo cha Ufundi, je, ni lini Serikali itatujengea Chuo cha Ufundi Wilayani Liwale?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Liwale wanahitaji chuo, lakini kwa bajeti ya mwaka huu Liwale haimo katika vyuo vitakavyojengwa. Ninachoshauri kwa sasa ,wale wanafunzi wote wanaohitaji kupata mafunzo haya ya ufundi waende pale katika vyuo vyetu ambavyo viko tayari na chuo ambacho kina uwezo wa kuchukua wanafunzi wengi pale Mtwara na watapata mafunzo yanayostahili.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Ni Sera ya Taifa kuwa na Chuo cha Ufundi katika kila Wilaya:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha Ufundi katika Wilaya ya Geita?

Supplementary Question 3

MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa, tatizo la ukosefu wa Chuo cha Ufundi katika Wilaya ya Geita inafanana kabisa na Wilaya yangu ya Pangani. Je, ni lini Serikali itahakikisha kwamba inatujengea Chuo cha Ufundi kwa sababu vijana wa Pangani wanashindwa kunufaika na rasilimali zilizopo katika Wilaya yangu ya Pangani?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ilivyo kwa Wilaya nyingi, ambazo zina uhitaji mkubwa wa kuhitaji kupata vyuo hivi vya VETA, niseme tu kwamba, tayari bajeti ya mwaka huu Waheshimiwa Wabunge wote mnayo na vyuo vitakavyotekelezwa vimo. Kwa hiyo, kama Wilaya yoyote ile imo katika orodha ya vyuo vinavyoanza kutekelezwa, basi ajue kwamba tupo katika kutekeleza mpango huo na kama haipo basi tunaendelea na michakato ya kupata ardhi ili na vyenyewe viweze kuwa katika mpango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tumegundua kwamba kwa muda mrefu fedha ambazo zimekuwa zikitengwa kwa ajili ya vyuo imekuwa ni kidogo, mwaka huu baada ya kutembelea na kuona huu uhitaji mkubwa tulichojifunza ni kuongeza maeneo hayo ya bajeti katika vyuo vyetu hasa hivi vyuo vya ufundi vya Wilaya.

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:- Ni Sera ya Taifa kuwa na Chuo cha Ufundi katika kila Wilaya:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha Ufundi katika Wilaya ya Geita?

Supplementary Question 4

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na swali langu ni hivi, wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne, darasa la saba kwenye nchi hii na hata wanaomaliza kidato cha sita na wakashindwa kuendelea ni wengi mno na Serikali yenu hii imesema inataka kujenga viwanda, japo ni viwanda vya akina Bhakresa na tunajua tunahitaji ma-technician wengi sana kwenda kufanya kazi kwenye viwanda, makampuni na hata migodi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri hebu atuambie ni lini kwa mipango yenu nchi nzima hii kutakuwepo na vyuo kwenye Wilaya, kwa sababu siyo kila siku tunasimama hapa tunauliza kwamba swali hili linafanana na la kwangu, lini mnataka muwe mmefikisha vyuo angalau kwenye Wilaya au tuvipeleke kwenye Kata kama shule za sekondari?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo amezungumzia katika suala lake, maudhui yake ya msingi kwamba kuna tatizo kubwa la mahitaji ya vijana kubakisha ujuzi. Ujuzi unapatikana katika staili za aina mbalimbali, mojawapo ni hiyo ya kuwa na vyuo maalum ikiwemo Vyuo vya Ufundi pamoja na Vyuo hivi vya Maendeleo ya Wananchi, pia tunavyo Vyuo Vikuu, ambavyo vyote vinatoa mafunzo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwa kutambua mahitaji haya yalivyo mengi, kuna vijana wengine pamoja na watu wazima ambao siku zote wamekuwa wakifanya shughuli za ufundi, lakini wamekuwa hawatambuliwi. Tayari kwa kutambua hilo tunao mpango wa kutambua wale ambao wana ujuzi ambao hawakupitia katika maeneo rasmi na hiyo tukishawatambua wanapewa mafunzo ya ziada ya ujasiriamali na kuwawezesha kutambulika.
Vilevile kupitia mpango ambao ni wa kuwezesha vijana katika mafunzo mbalimbali ya ufundi, hivi juzi tarehe 28 nimezindua tena mpango wa pili wa kuwezesha vijana mbalimbali ambao wataweza kupata mafunzo, yakawezesha kujiajiri na kuwezesha kuhudumia hivi viwanda vidogovidogo kama ambavyo Mheshimiwa Waziri wa Viwanda jana alivyoeleza ili waweze kufanya shughuli zao. Mpango huo utanufaisha vijana zaidi ya 22,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kwa staili mbalimbali ambazo tunatumia tutaweza kuwafikia vijana wengi zaidi na kwa muda mfupi zaidi.