Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- Sera ya Elimu inasema mlinganyo wa vyoo kwa wanafunzi wa kike uwe choo kimoja kwa wasichana 20 na choo kimoja kwa wavulana 25:- Je, utekelezaji wa Sera hiyo kwenye eneo hili ukoje?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu haya yaliyotolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto wa kike wanahitaji faragha na hasa wanapokuwa katika siku zao. Kwa hali hii iliyopo hivi sasa ni tatizo kubwa kwa watoto wa kike. Je, Serikali inachukua hatua gani za dharura kuhakikisha kwamba angalau tunawapatia unafuu watoto wa kike na hasa ukizingatia kwamba shule nyingi pia hazina maji kwa mtoto huyu wa kike inakuwa ni vigumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; je uwiano huu wa 52 kwa 54 na 23 kwa 25 kwa shule za sekondari umezingatia kwa kiasi gani hali ya watoto wenye mahitaji maalum, watoto wenye ulemavu ambao wanalazimika kutambaa katika kinyesi cha watoto wenzao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwa sababu ni changamoto kweli hasa watoto wetu wa kike kuna wakati fulani wanataka faragha ya hali ya juu kuwawezesha kusoma katika mazingira rafiki na hili ndiyo maana nimesema kwamba katika yale matundu ambayo tunayajenga 8,991 kwa shule za msingi na yale 1942 kwa shule za Sekondari kipaumbele ni matundu ya vyoo vya kike.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tuna mradi wa MMES II ambao katika shule za sekondari tunajenga takriban matundu yasiyopungua 9,345. Katika haya maelekezo yetu ni kuhakikisha hasa katika shule za sekondari tunaweka nguvu kubwa tuweze kuondoa kabisa tatizo hasa la vyoo vya kike, kwa kujua kwamba, hili jambo ni muhimu sana kwa ajili ya utulivu wa watoto wetu hasa wa kike wanapokuwa katika yale mazingira ambapo hakuna namna lazima wapate mazingira yenye staha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika suala la walemavu ni kweli, katika kipindi cha nyuma kilichopita kwa muda mrefu tulikuwa hatuna kipaumbele cha kutosha katika ujenzi wa miundombinu yetu hasa katika maeneo ya walemavu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Amina Molel, katika vyoo vyetu vya sasa vyote vinavyojengwa suala la vyoo kwa watu wenye mahitaji maalum ni kipaumbele chetu cha msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa katika maeneo mbalimbali tunakopita na jana nilikuwa katika shule moja ya Chang‟ombe „B‟, tunaenda kujenga karibuni vyoo 20 lakini kipaumbele tumesema katika ujenzi ule ramani zote zinaelekeza watu wenye mahitaji maalum hasa walemavu ili kuhakikisha ujenzi wote unaofanyika sasa hivi uweze kuligusa kundi hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Amina Molel nimhakikishie kundi ambalo analiwakilisha vema humu Bungeni, tutahakikisha tunalipa nguvu ya kutosha na kuhakikisha kwamba haki zao zinapatikana kwa muda wote katika kipindi cha utawala huu.

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- Sera ya Elimu inasema mlinganyo wa vyoo kwa wanafunzi wa kike uwe choo kimoja kwa wasichana 20 na choo kimoja kwa wavulana 25:- Je, utekelezaji wa Sera hiyo kwenye eneo hili ukoje?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana. Nami naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, hili tatizo la matundu ya choo hasa shule ambazo ziko pembezoni, shule za vijijini siyo rafiki sana na watoto wa kike pamoja na wanafunzi kwa ujumla. Ni lini Serikali itahakikisha tatizo hili la matundu ya choo linakwisha mara moja?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la dada yangu Maryam Msabaha Mwanajeshi kutoka kambi ya Bulombora kule Mkoani Kagera kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema awali kwamba mpango mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunatatua tatizo la vyoo kama Mheshimiwa Molel alivyoanza na swali hili. Nilipopita maeneo mbalimbali kwa mfano takriban wiki moja na nusu nilikuwa katika Wilaya ya Kakonko, Buhigwe na maeneo mengine kule, nilipita katika maeneo hayo nikikagua hata baadhi ya miundombinu ya vyoo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tuna kila sababu, ndiyo maana tuna mpango mkakati mpana sana. Tumetenga fedha karibu bilioni 12, lengo kubwa ni investment katika kuondoa kero hii. Naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, Serikali kwa umoja wake lakini vilevile na wadau mbalimbali niwashukuru sana, katika kipindi hiki tumeweza kushirikiana vema kwa sababu baada ya kuondoa ajenda ya tatizo la madawati, sasa hivi Serikali na wadau mbalimbali tumejielekeza katika vyoo na vyumba vya madarasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, imani yangu ni kwamba ndani ya muda mfupi tutaona mazingira makubwa sana yamebadilika katika sekta ya elimu katika Jamhuri yetu ya Muungano wa Tanzania.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- Sera ya Elimu inasema mlinganyo wa vyoo kwa wanafunzi wa kike uwe choo kimoja kwa wasichana 20 na choo kimoja kwa wavulana 25:- Je, utekelezaji wa Sera hiyo kwenye eneo hili ukoje?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwaa Mwenyekiti, nakushukuru. Tatizo la vyoo katika shule zetu za msingi linafanana na tatizo la nyumba za Walimu kwa shule zetu na tatizo hili sasa hivi kama limeachiwa Halmashauri ndiyo watatue tatizo hili, lakini kwa mapato ya Halmashauri nina uhakika mkubwa kwamba tatizo hilo haliwezi kupatiwa ufumbuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumuuliza Naibu Waziri kwamba Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo hili katika kipindi kifupi kijacho?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niweke wazi kwamba Serikali kwa sasa imejipanga vema. Imejipanga vema kwanza hata ukiangalia mchakato wa bajeti ya mwaka huu tumemaliza madawati, lakini tumetenga takriban bilioni 13 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba katika shule za msingi na bilioni 11 katika shule za sekondari. Tukishirikiana TAMISEMI na wenzetu wa TEA jambo hili tumekuwa na mkakati mpana sana, lengo siyo nyumba za Walimu peke yake, bali ni madarasa, nyumba za Walimu, maabara na kufanya mpango kabambe wa ukarabati wa shule kongwe. Mwaka huu peke yake, shule kongwe 33, kila shule tunaipatia bilioni moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo letu, Watanzania waone kwamba, Serikali ya Awamu ya Tano, ina lengo la kuweka msukumo wa mbele katika kuboresha elimu yetu ya Tanzania.