Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Kata za Mtambula, Idunda, Maduma, Kiyowela na Idete ili wananchi waweze kufaidika na huduma hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri lakini nina maswali mawili tu ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; katika upelekaji wa umeme vijijini, REA wanapeleka kwa kufuata barabara na kwenye centres, lakini unaweza ukaona kwamba kwenye shule za msingi, sekondari, vituo vya afya na zahanati kule umeme haupelekwi. Sasa Naibu Waziri naomba anihakikishie wananchi wa Jimbo la Mufindi Kusini kwenye maeneo haya niliyotaja kama watapewa umeme?
Mheshimiwa Mwenyekiti la pili, namuomba Naibu Waziri, kwa majibu haya aliyoeleza vizuri, kwa programu ya awamu ya tatu ambayo inaanza, je, utakuja lini Mufindi ukafanya mkutano angalau hata mmoja kuongea na wale wananchi?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kuwajulisha Waheshimiwa Wabunge na wananchi kwa ujumla kwamba mradi kabambe wa REA Awamu ya Tatu utapeleka umeme katika maeneo yote ya taasisi ikiwemo shule za msingi, sekondari, hospitali na katika taasisi nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Mheshimiwa Kigola, jimbo lako la Mufindi Kusini, maeneo yote niliyoyataja ikiwemo pia katika vijiji vyako vya Mbaramaziwa, Tambarang‟ombe kwenda mpaka Tengereo mpaka kule Kilowelo vitapelekewa umeme kwenye taasisi nilizozitaja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu suala lake la pili, kwamba ni lini sasa tutatembelea katika maeneo yale? Nimhakikishie Mheshimiwa Kigola; kwanza kabisa nikupongeze umeshaanza kuchimba visima kwa ajili ya kuhitaji umeme. Napongeza sana kwenye Kitongoji chako cha Msumbiji umeshaanza kujenga, lakini pale Idambaravumo pia umeshaanza kujenga na pia unatarajia kupeleka umeme pale Kilowelo centre, na pia kwenye vijiji vyako vingi sana ikiwemo kama nilivyosema pale Kisaula tutakupelekea mashine ya umeme, lakini pia kwenye vijiji vyako vingine mbali na vijiji na Kitongoji cha Msumbiji na pale Changarawe kwa Mheshimiwa Kigola kwa vijiji vyako 47 vilivyobaki vyote vitapata umeme wa uhakika.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Kata za Mtambula, Idunda, Maduma, Kiyowela na Idete ili wananchi waweze kufaidika na huduma hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante. Kwa kuwa tatizo linalowakabili wananchi wa Mufindi Kusini linafanana sana na wananchi wa Jimbo la Nzega Mjini; nilitaka kusikia kauli ya Waziri, katika kata ya Migua, jimbo la Nzega Mjini, Kata za Mwanzoli, Mbogwe, maeneo ya Bulunde pamoja na Kashishi yote haya yalikuwa yapekelewe umeme kwa miradi ya MCC na miradi hii imefutwa. Je, Naibu Waziri anasema kauli gani kuwaambia wananchi wa jimbo la Nzega wa maeneo haya juu ya upatikanaji wa uhakika wa umeme katika maneo niliyoyataja? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nipende tu kusema wazi kwamba miradi yote iliyokuwa chini ya MCC ambayo haikuendelea sasa itapelekewa umeme kwa bajeti ambayo tumeipitisha kupitia mradi wa REA wa Awamu ya Tatu ikiwemo pamoja na vijiji kwa Mheshimiwa Bashe alivyovitaja kwenye jimbo lake. Lakini niseme tu, kijiji cha Kashishi tulishaanza kufanyia survey lakini pia vijiji vya Mbogwe na vingine vya karibu tulishaanza kuvifanyia survey na vyote vitapelekewa umeme kwenye kipindi hiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Bunge lako mimi nitatembelea kwa Mheshimiwa Kigola mara tukimaliza Bunge, pia nitatembelea kwa Mheshimiwa Bashe na maeneo mengine kuhakikisha maeneo yote yanapata umeme.