Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kusambaza maji katika Kata za Kasamwa, Shiloleli, Bulela, Nyarugusu, Bukeli na maeneo mengine ya Wilaya ya Geita na Mkoa wa Geita kwa ujumla?

Supplementary Question 1

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, katika jibu la Mheshimiwa Naibu Waziri suala zima la miundombinu; Mheshimiwa Rais alivyokuwa na ziara Mkoani Geita alitoa ahadi kwa wananchi wa Kasamwa kwa ajili ya kuwachangia pesa kujenga bwawa au lambo kama tunavyoweza kuliita. Lakini kazi iliyofanyika ni chini kabisa ya viwango na maji yale ni machafu, wananchi hawawezi kuyatumia. Na katika majibu yako pia katika hizi pesa ambazo zimetajwa hapa tumepata taarifa katika Kamati zetu kwamba Serikali haina pesa ya kutoa kwa ajili ya miradi ya maji katika sehemu nyingi hapa nchini.
Sasa naomba Serikali itoe tamko kwa wananchi ambao wana wasikiliza leo kwamba Serikali hii ina mkakati gani wa kuhakikishia wananchi kwamba wanapata maji safi na salama ambao wananchi wengi ambao ni wanyonge shida yao ni maji na sio bombardier? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali pili Mheshimiwa Rais Magufuli aliweza kutoa ahadi kwa wananchi wa Geita kuweza kuwapatia magwangala, lakini katika eneo la Nyarugusu ni kati ya maeneo ambayo yameathirika sana kutokana na uchenjuaji wa dhahabu na wananchi katika maeneo hayo hawana maji salama kutokana kwamba vyanzo vingi vimeathiriwa na mercury.
Serikali inatoa tamko gani kwamba pamoja na shughuli za magwangala ambazo Rais amezitoa kwamba wananchi wa Geita watapata maji salama ili waweze kuendelea na maisha yao? Ahsante

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema kwamba Mheshimiwa Rais ametoa ahadi pale, lakini kazi inaendelea chini ya kiwango. Naomba nikuhakikishie kwamba tarehe 27/08 nilikuwa katika Mkoa wa Geita na nilifanya harambee kubwa pale tulipata karibuni 1.4 billion kwa ajili ya madawati katika Mkoa wa Geita. Hata hivyo, katika sekta ya maji kwa sababu ni kipaumbele changu, nilitembelea maeneo mbalimbali ikiwepo Chato na mradi mwingine nikazindua lakini na mradi mwingine ambao ulikuwa watu wamefanya mambo ya ovyo na kuunda kamati. Na hivi sasa tutaenda kuchukua hatua stahiki kwa wale watu wote waliokiuka utaratibu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nikwambie ni commitment ya Serikali kama sehemu ambayo umefanya ubadhirifu na mambo ya hovyo tutaenda kuyasimamia. Nikwambie kama kamati sasa hivi timu niliyounda tayari taarifa ipo mezani kwangu tunaenda kuchukua hatua stahiki kwa ajili ya wananchi. Kuna mradi mmoja wa Changolongo ambao umefanyika mambo ya ovyo, watu hawakufanya mambo sawasawa hata hiyo tunaenda ku-cross check. Lengo letu ni kwa wananchi wa Mkoa wa Geita na Mikoa na mingine waweze kupata huduma ya maji na hatutokuwa na masihara hata kidogo kwa watu ambao wanachezea kwa makusudi nguvu yoyote ya Serikali inayopelekwa halafu watu wakafanye mambo ya ovyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwambie commitment yetu ipo hapo na Mkoa wa Geita tunaenda kuchukua hatua, lakini naomba niwaombe radhi sana kwa wale watu ambao hata wakiwa ndugu zenu tukiwachukulia hatua tunaacha sasa naomba tusileteane vi-memo tunaenda kuwachukulia hatua watu waliokiuka taratibu za manunuzi katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili; suala la kwamba kuna mercury wananchi wa Nyarugusu wanahakikishiwa vipi? Ni kwamba ni commitment ya Serikali na ndio maana hata nilipofika kule niliwaambia wataalam wetu wajiongeze. Haiwezekani Mkoa wa Geita ambao kuna Ziwa Victoria kila sehemu unakoenda unakuta maji wananchi wanakosa fursa ya maji. Tukawaambia kwamba waje na mpango jinsi gani tutafanya Mkoa mzima wa Geita kutumia fursa ya Ziwa Victoria badala ya kuchimba borehole, tupate vyanzo vya maji mbadala kutumia Ziwa Victoria na hili niliwaagiza watalaam wetu na hilo wanalifanyia kazi. Na nimewaambia nataka tulione katika mpango wa bajeti wa mwaka huu wa fedha unaokuja, lengo kubwa wananchi wapate fursa ya maji katika maeneo yao.