Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Neema William Mgaya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itahakikisha wakulima wanapata pembejeo za kilimo kama mbolea kwa wakati kwa kuwa tatizo hilo limekuwa sugu?
Supplementary Question 1
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri. Kwa kuwa hatuna muda nitauliza swali moja tu la nyongeza na swali langu liko hivi. Kwa kuwa, kumekuwa na mlolongo mrefu wa upatikanaji wa pembejeo za kilimo kwa wakulima.
Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kutafuta njia mbadala ili kufupisha mlolongo huo?
Name
William Tate Olenasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngorongoro
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Serikali iko kwenye mpango tayari wa kupitia mfumo wa kutoa pembejeo ili kuleta mfumo ambao utaleta ufanisi zaidi katika ugawaji wa pembejeo ambao sisi tunaamini kwamba siyo tu kwamba, utarahisisha upatikanaji wa pembejeo kwa wakati, lakini vilevile kwa bei nafuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni kama mnavyofahamu tumekutana na Wabunge wote wanaotoka maeneo wanayolima mazao muhimu ili kupata mawazo yao ya namna ya kuboresha mfumo huu. Nawaahidi kwamba, katika bajeti inayokuja, Serikali inakuja na mapendekezo ya mpango mpya kabisa ambao utaondoa hii kero na changamoto, ili isiwepo tena. Nashukuru sana.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved