Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Kituo cha afya kilichopo Laela kinategemewa na Kata za Lusaka, Kasanzama, Laela, Mnokola, Miangalua na Kaoze; kutokana na kupanuka kwa kasi kwa mji huo na ongezeko la watu wanaohudumiwa katika kituo hicho, kimesababisha upungufu wa dawa, wataalamu na vifaa tiba. (a) Je, ni lini Serikali itakipa kituo hicho hadhi ya Hospitali ya Wilaya? (b) Je, ni lini kituo hicho kitapatiwa gari la wagonjwa? (c) Je, ni lini Serikali itapeleka wataalam wa kutosha, vifaa tiba na dawa za kutosha katika kituo hicho?

Supplementary Question 1

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ina vituo vya afya vitano ambavyo havina magari ambavyo ni Laela, Kayengeza, Msanadamungano, Mpuwi na Milepa, na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga imejitahidi sana katika kuweka bajeti kwa mwaka 2013/2014, 2014/2015 ili kukabiliana na adha hii lakini Serikali haijatoa fedha ili halmashauri iweze kununua magari hayo. Sasa Serikali inaithibitishiaje halmashauri kwamba ikitenga fedha inaweza kuipatia ili iweze kununua magari kukabiliana na tatizo hilo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri amezungumzia tatizo la msongamano wa wingi wa wagonjwa katika Kituo cha Afya Laela, na amezungumzia utatuzi wa tatizo hilo kwa mpango wa muda mrefu, wakati kwa sasa tatizo hilo ndiyo lipo na ni kubwa sana kutokana na wingi wa watu na kupanuka kwa mji mdogo. Nataka Serikali inieleze, kwa sasa inafanyaje mpango wa dharura ili kuokoa wananchi wanaosongamana katika kituo cha afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mchakato wa bajeti unaokuja, naomba ninyi anzeni tu ule mchakato wa awali wa kuhakikisha kwamba mnatenga ile bajeti halafu sisi tutasimamia jinsi gani katika Bajeti ya mwaka 2017/2018 hilo gari liweze kupatikana, yaliyopita si ndweli tugange yajayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msongamano wa sasa tulionao katika hospitali, nakumbuka Mheshimiwa Mbunge tulikuwa pamoja pale katika eneo lako. Kwanza wasiofahamu jimbo la Mheshimiwa Malocha, liko kama mbalamwezi hivi ambao mwezi mchanga, ambayo kuna watu wengine wanatoka maeneo ya Pembe mbali sana kuja katika Hospitali ya Sumbawanga. Kwa hiyo, mwenyewe nime-verify lile tatizo, ni tatizo la msingi na hili naomba nimwelekeze RAS wetu wa Mkoa wa Rukwa kwamba aangalie jinsi gani kwanza kama mpango wa haraka kuhakikisha eneo hili linapata angalau huduma katika sekta ya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ni kweli, wananchi wa Mheshimiwa Malocha pale wakitoka kule Pembe mpaka kufika hapa kama mgonjwa anaweza akafariki. Kwa hiyo, naomba nikwambie ofisi yetu itawasiliana na ofisi ya mkoa pale tuangalie mipango mikakati ya haraka kuwasaidia wananchi wa eneo lako ilimradi waweze kupata huduma ya afya kama ilivyokusudiwa na Watanzania wengine.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:- Kituo cha afya kilichopo Laela kinategemewa na Kata za Lusaka, Kasanzama, Laela, Mnokola, Miangalua na Kaoze; kutokana na kupanuka kwa kasi kwa mji huo na ongezeko la watu wanaohudumiwa katika kituo hicho, kimesababisha upungufu wa dawa, wataalamu na vifaa tiba. (a) Je, ni lini Serikali itakipa kituo hicho hadhi ya Hospitali ya Wilaya? (b) Je, ni lini kituo hicho kitapatiwa gari la wagonjwa? (c) Je, ni lini Serikali itapeleka wataalam wa kutosha, vifaa tiba na dawa za kutosha katika kituo hicho?

Supplementary Question 2

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Kwa kuwa swali la msingi hapa ni kituo cha afya; na kwenye Jimbo la Vunjo, Kata ya Marangu Magharibi yenye vijiji saba haina kituo cha afya wala zahanati hata moja, na mpaka sasa Mbunge kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji cha Kitowo na Kiraracha tumeweza kufanikisha shilingi milioni 20, na KINAPA wanatupatia shilingi milioni 53 na tunategemea kujenga kwa shilingi milioni 200, commitment ya Serikali itatoa mchango gani ili Kata ya Marangu Magharibi, hasa Kijiji cha Kiraracha waweze kupata huduma ya afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niwapongeze kwa ile initial stage ya wananchi wako, mmefanya resource mobilization pale mmeweza kupata karibu shilingi milioni hiyo ishirini na kwa ajili ya jambo hilo, nililizungumza katika vipindi mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesema kwanza tumefanya tathmini ya nguvu za wananchi katika maeneo mbalimbali, kuna maboma mengi sana yamejengwa lakini yamefika katikati hayajakamilishwa, ndiyo maana tumewaagiza Wakurugenzi wote wa maeneo mbalimbali kuangalia zile juhudi ambazo wamefanya katika eneo lao, ili mradi katika bajeti hii ya mwaka wa fedha inayokuja tuhakikishe kwamba ajenda ya kwanza ni kukamilisha maboma na maeneo yote. Tukifanya hivi yale maboma ambayo yapo katika stage mbalimbali tutakuwa tumesaidia sana kuwapa support wananchi, lakini hali kadhalika tutakuwa tumejenga vituo vingi vya afya na zahanati tutapunguza tatizo la afya katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo nikushukuru katika hilo. Serikali commitment yetu ni kwamba tumeshafanya hilo zoezi liko katika ground linaendelea na katika mchakato wa bajeti hiyo ni priority yetu katika mpango wa fedha wa mwaka 2017/2018.