Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- Baadhi ya watumishi wa DEPU mwaka 1999 – 2000 na Idara ya Uhamiaji hawajapandishwa vyeo mpaka sasa, licha ya kuwa na vigezo kama vya elimu na ngazi ya shahada huku wenzao wakiwa wamefikia vyeo vya Makamishna na Kamishna wasaidizi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia watumishi kupata haki yao ya vyeo stahiki kama ilivyo kwa wenzao waliopandishwa vyeo?

Supplementary Question 1

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, je, ni wangapi ambao walipandishwa vyeo ambao waliweza kujiendeleza kielimu toka mwaka 1999 na 2000 mpaka sasa na ni utaratibu upi ambao unatumika kupandisha vyeo kwa vijana wa uhamiaji? Kwa sababu mpaka sasa kuna vijana ambao wana vigezo na viwango vya elimu sawa na waliopandishwa vyeo miaka sita nyuma. Kutoka miaka sita mpaka sasa hivi hakuna hata kijana mmoja kwa upande wa Zanzibar ambaye amepandishwa cheo. Je, Mheshimiwa Waziri anaweza akatupa sababu ambazo zimepelekea miaka sita mpaka sasa hivi kuwe hakuna mtu ambaye ameweza kupandishwa cheo? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, si kwamba hakuna ambaye amepandishwa cheo. Wamepandishwa vyeo katika nafasi tofauti tofauti, kumbukumbu zinaonesha zaidi ya vijana 137 kwa gap lile alilolisemea la mwaka 1999 – 2000 walipandishwa vyeo katika nafasi tofauti tofauti.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu wale ambao amesema wa upande wa Zanzibar na lenyewe nitalifuatilia kwa undani wake ili niweze kuwasiliana na Mheshimiwa Mbunge. Kama alichosema ndicho, basi katika hatua zinazofuata tunakokwenda tutazingatia ushauri wa Mheshimiwa Mbunge ili kuhakikisha kwamba jambo linapoletwa na watetezi wa wananchi, Waheshimiwa Wabunge, wawakilishi wa wananchi; sisi Serikali tunalifanyia kazi kuhakikisha kwamba panakuwepo na haki ya watu wetu hao wanaofanya kazi vizuri. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- Baadhi ya watumishi wa DEPU mwaka 1999 – 2000 na Idara ya Uhamiaji hawajapandishwa vyeo mpaka sasa, licha ya kuwa na vigezo kama vya elimu na ngazi ya shahada huku wenzao wakiwa wamefikia vyeo vya Makamishna na Kamishna wasaidizi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia watumishi kupata haki yao ya vyeo stahiki kama ilivyo kwa wenzao waliopandishwa vyeo?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Askari Magereza wapo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na kwa kuwa Askari Magereza na wenyewe wanajiendeleza, wanapata shahada, wanapata elimu ya juu zaidi, lakini mishahara yao imekuwa ikibaki kuwa ile ile ambayo haitofautiani na askari wa kawaida aliye na cheti cha form four. Ukiangalia Jeshi la Polisi mtu mwenye shahada anapata sh. 860,000 lakini pia anapata posho ya ujuzi asilimia 15, kwa Askari Magereza wanalipwa sh. 400,000 wakikatwa inabaki 335,000.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua sasa ni lini Serikali itaona umuhimu wa kuwalipa Askari Magereza kulingana na ujuzi wao maana imekuwa ikiwaahidi kwamba itawaongezea mshahara kulingana na ujuzi wao, lakini mpaka leo bado. Ni lini sasa itakwenda kuwalipa Askari Magereza kulingana na ujuzi wao ili kuwapa motisha kama askari wengine?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Matiko hususan katika masuala mazima ya kupanga mishahara ya Askari Magereza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua katika kada mbalimbali si wote ambao wanapata mishahara ambayo inaendana na kazi zao. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Esther Matiko, tayari tumeshaanza zoezi la tathmini ya kazi na hata ninavyoongea hapa watu wangu wa Bodi ya Mishahara wako hapa Bunge, wameshaongea na Tume ya Huduma za Bunge, lakini vilevile wameshazunguka nchi nzima kuongea na kada mbalimbali. Ifikapo mwezi wa Pili zoezi hili litakuwa limekamilika na baada ya hapo tukae sasa kupanga uwiano wa kazi pamoja na uzito wa majukumu kwa kada moja baada ya nyingine tukitambua ugumu wao wa kazi pamoja na majukumu yao. Vile vile tutaweza kupanga pia miundo yao pamoja na madaraja yao katika ngazi za mshahara. Kwa hiyo, nimhakikishie zoezi hili litaweza kufanyika kwa Askari Magereza, lakini vilevile kwa watumishi wote wa umma kwa ujumla wake.

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- Baadhi ya watumishi wa DEPU mwaka 1999 – 2000 na Idara ya Uhamiaji hawajapandishwa vyeo mpaka sasa, licha ya kuwa na vigezo kama vya elimu na ngazi ya shahada huku wenzao wakiwa wamefikia vyeo vya Makamishna na Kamishna wasaidizi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia watumishi kupata haki yao ya vyeo stahiki kama ilivyo kwa wenzao waliopandishwa vyeo?

Supplementary Question 3

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na matatizo ya askari ambayo yameelezwa, lakini kuna matatizo yaliyoko kwa Askari wetu wa Kikosi cha Reli ambao huwa wanasindikiza hizi treni katika maeneo mbalimbali kama vile Mpanda, Kigoma na Mwanza. Sasa kuna utaratibu wa wao kulipwa allowance katika hizo kazi wanazofanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Askari wa Kikosi cha upande wa Kata ya Katumba na Ugala wana madai yao tangu mwaka 2013 mpaka sasa hawajalipwa. Sasa je, Waziri yuko tayari kuhakikisha kwamba Shirika la Reli linalipa mafao yao ili waondokane na tatizo la usumbufu kwa sababu imepelekea mpaka wamefungua kesi Mahakamani?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli yapo malalamiko ya madai mbalimbali ya askari yakiwemo hayo ya askari wale wanaofanya kazi upande wa TAZARA. Kilichokuwa kinafanyika ilikuwa ni uhakiki wa madai hayo na Wizara yangu tayari imeshawasiliana na Wizara ya Fedha ili punde ambapo uhakiki huo utakuwa umekamilika wa madai mbalimbali yakiwemo ya askari hao aliowataja Mheshimiwa Mbunge, malipo hayo yaweze kufanyika na kuweza kuondoa kero hiyo ambayo imekuwa ikijitokeza kwa askari wetu wanaofanya kazi nzuri.