Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:- Kumekuwa na uuzaji holela wa vifaa hatarishi barabarani kama vile visu, mapanga na kadhalika. Je, Serikali ina mkakati gani wa kukomesha biashara hii ambayo ni hatari kwa usalama wa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, katika jibu lake la msingi amesema kwamba, pindi biashara hii itakapoendelea, Serikali itachukua hatua zinazostahili. Sasa biashara hii ipo inaendelea na hasa katika Majiji makubwa kama Dar es Salaam na ni hatarishi kwa sababu mtu anakuja anajifanya kama anakuuzia kisu, mimi mwenyewe ni muathirika, pindi akikuona umeshika kitu anajifanya kama anakuuzia kisu lakini anakuamuru utoe kile kitu ulichokishika. Sasa naomba tamko la Serikali kwa habari ya biashara hii. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuliona hilo. Kama ilivyo kwa uhalifu mwingine, Serikali inapiga vita uhalifu wa aina yoyote na nitoe rai kwa mtu yeyote ambaye atakutana na mambo ya aina hiyo na yeyote aliye karibu na mtu anayepatwa na jambo hilo, tushirikiane kuhakikisha kwamba tunakomesha uhalifu wa aina hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi litakuwa bega kwa bega na litakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba wale wote wanaotumia vibaya mazingira hayo watafikishwa katika mkono wa sheria ili kuweza kukomesha uhalifu wa aina hiyo.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:- Kumekuwa na uuzaji holela wa vifaa hatarishi barabarani kama vile visu, mapanga na kadhalika. Je, Serikali ina mkakati gani wa kukomesha biashara hii ambayo ni hatari kwa usalama wa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona ili niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa askari hawa ambao wanatekeleza kufanya nchi hii iwe na amani kuhakikisha wahalifu wanakuwa hawafanyi vizuri wako katika Jimbo langu la Itigi na wanakaa katika nyumba ya railway ambayo ni mbovu sana. Kituo kile kiko katika nyumba za railway; Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaboreshea Kituo cha Polisi na Mheshimiwa Waziri anajua kabisa kituo kile ni kibovu na hakifai na wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi wamejitahidi kwa nguvu zao wameshindwa. Nini kauli ya Serikali na je, itawasaidia wananchi wa Halmashauri ya Itigi?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, natambua mazingira ya kituo kilichopo Itigi na Mheshimiwa Mbunge amekuja mara kadhaa kulielezea jambo hilo na ameandika na barua ya kiofisi na nimemwahidi kwamba kwa hatua ambazo wameshazifanya wao, akiongoza yeye mwenyewe jitihada hizo na sisi kama Wizara tutawaunga mkono na binafsi nitafika katika Jimbo lake kuweza kuongeza nguvu kwa kuona mazingira yaliyopo na hatua ambazo zimeshachukuliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge, nimhakikishie, awahakikishie na vijana wetu kwamba jambo hilo ameshalifikisha na sisi tutalichukulia hatua zinazostahili kwa kulipa uzito unaostahili.