Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Katika bajeti ya 2013/2014, Serikali iliahidi kujenga Mahakama ya Wilaya ya Chunya. Je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na pia nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini pamoja na majibu hayo nina maswali madogo mawili ya nyongeza:-
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amenihakikishia kwamba Serikali imetenga fedha sasa kwa ajili ya kujenga Mahakama ya Wilaya katika Wilaya ya Chunya, je, ni lini Mheshimiwa Waziri atakuja Chunya ili nimwonyeshe viwanja vilivyo ambavyo Halmashauri imetenga kwa ajili ya kazi hiyo?
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, Jimbo langu lina tarafa mbili, Tarafa ya Kiwanja na Tarafa ya Kipembawe. Tarafa ya Kiwanja ina Mahakama za Mwanzo mbili, moja iko Chunya, nyingine iko Makongorosi. Tarafa ya Kipembawe haina Mahakama ya Mwanzo hata moja. Sasa je, Serikali inasemaje kuhusu kuleta Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Wilaya ya Chunya ili Halmashauri iweze kumtengea eneo la kuweka Mahakama hiyo katika Tarafa ya Kipembawe?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimefarijika sana kumsikia Mheshimiwa Mbunge akisema viwanja tayari wanavyo na hivi majuzi tu nimetoka kujibu swali la Mbunge wa Temeke nadhani, nikielezea tu kwamba ni vizuri Wabunge sasa hivi mkahamasisha Halmashauri zenu kutuainishia viwanja ambavyo tayari vina hati iweze kuwa rahisi kwa Mahakama kuweza ku-identify maeneo hayo na kuweza kujenga maana pesa angalau sasa hivi tunayo ya kuweza kuanza ujenzi wa Mahakama za Mwanzo, Wilaya na hata Mahakama Kuu. Na tunashukuru kwamba kiwanja anacho Mheshimiwa Mwambalaswa, nitamfikishia ujumbe huu Mtendaji Mkuu wa Mahakama. Ningefurahi kama rai yake aliyoitoa hapa itafuatiwa na barua ili itiwe na kumbukumbu kabisa kwenye mafaili yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kuhusu Kipembawe kwamba hakuna Mahakama ya Mwanzo, ningemwomba, hiki ndiyo kipindi ambacho Mahakama inaangalia priorities tuanzie wapi katika kujenga jumla ya Mahakama 50 za mwanzo. Tafadhali tunaomba alete andiko la hayo mahitaji yawekwe pia kwenye file tuweze kuliangalia pamoja na mambo mengine.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Katika bajeti ya 2013/2014, Serikali iliahidi kujenga Mahakama ya Wilaya ya Chunya. Je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru kwa kunipa nafasi, nina swali moja la nyongeza. Tatizo la ukosefu wa Mahakama katika Wilaya ya Chunya ni sawasawa na tatizo llililopo katika Mahakama ya Herujuu. Jengo lililokuwepo la tangu enzi za ukoloni limebomoka kabisa hivyo huduma ya Mahakama wanakaa chini ya miti. Je, ni lini Serikali itatoa pesa kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama ya Herujuu?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri mbele yenu kwamba hali ya miundombinu ya Mahakama nchini si nzuri. Nikielekeza macho tu, upande wa Mahakama za Mwanzo tunahitaji ili tuwe na access to justice sawasawa tuwe na Mahakama za Mwanzo katika kila Kata. Tuna kata zaidi ya 3,900 nchini lakini Mahakama tulizojenga mpaka sasa hazizidi 900, kwa hiyo pengo ni kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Josephine Genzabuke, kuhusu mahitaji halisi katika eneo lake, tunaomba atuandikie hiki ndiyo kipindi ambacho tunaangalia mahitaji kufuatana na demand iliyopo katika maeneo yote tuliyonayo. Kwa hiyo tunasubiri ndani ya siku mbili, tatu atatufikishia hayo mahitaji ya jimbo lake.