Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Ukosefu wa nyumba za walimu katika maeneo ya vijijini unasababisha Walimu kuhama maeneo hayo na hivyo kusababisha upungufu mkubwa wa Walimu, pia Halmashauri nyingi hazina uwezo wa kujenga nyumba za Walimu za kutosha kwa kutumia fedha zao za ndani. Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga nyumba za Walimu wa shule za msingi vijijini hasa ikizingatia kuwa vijijini hakuna nyumba ambazo Walimu wanaweza kupanga?

Supplementary Question 1

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri na hasa wazo la ku-design nyumba moja ambayo itaweza ku-accommodate Walimu sita kwa maana familia sita. Sasa swali langu ni kwamba je, Serikali haioni sasa kwamba kuna umuhimu wa kusambaza hii ramani ya design hii ambayo nyumba moja inaweza ika-accommodate Walimu sita kwa Halmashauri zote na maelekezo maalum ili shule ambazo zipo vijiji sana Halmashauri ziweze kutumia ramani hii na kujenga nyumba? Kwa sababu ukiweza kujenga nyumba mbili tu maana yake tayari ume-accommodate Walimu 12?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikiri katika Jimbo analozungumza Mheshimiwa Mbunge na mimi nilikuwa kule. Aliponiagiza yeye mwenyewe nitembelee Jimbo lake; nikatembelea miradi ya afya na kuona mambo mengine na changamoto za miundombinu. Naomba niseme ushauri huu tumeshaufanyia kazi Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuhakikisha ramani hizi zinakwenda kila Halmashauri. Tunachokifanya ni kuhakikisha tunaweka mkazo sasa, bajeti yoyote inayopatikana lazima tuelekeze katika mfumo wa ramani mpya ambayo kwa kiwango kikubwa ina tija sana katika Halmashauri zetu kuhusu suala la kupunguza tatizo la upungufu wa nyumba za Walimu katika Halmashauri zetu.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Ukosefu wa nyumba za walimu katika maeneo ya vijijini unasababisha Walimu kuhama maeneo hayo na hivyo kusababisha upungufu mkubwa wa Walimu, pia Halmashauri nyingi hazina uwezo wa kujenga nyumba za Walimu za kutosha kwa kutumia fedha zao za ndani. Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga nyumba za Walimu wa shule za msingi vijijini hasa ikizingatia kuwa vijijini hakuna nyumba ambazo Walimu wanaweza kupanga?

Supplementary Question 2

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa wananchi wengi wamejitolea kujenga maboma ambayo wamejitolea kujenga zahanati, nyumba za Walimu na mpaka sasa halmashauri hazijaweza kukamilisha. Je, ni lini sasa Halmashauri zitakamilisha miradi ambayo ni viporo ambavyo wananchi wameweza kujenga? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli maboma ni mengi na kumbukumbu yangu kati ya tarehe 12 na 13 nilikuwa kule Tabora katika Mkoa wako na nishukuru sana ushirikiano wako japokuwa ulikuwa na changamoto za kuuguliwa. Katika kupita huko huko katika Mkoa wa Tabora lakini na mikoa mingine tatizo la maboma limekuwa ni kubwa ndiyo maana katika maelekezo yetu tumeagiza kwanza lazima tumalize vile viporo vya mwanzo. Kama maboma ya ujenzi wa zahanati, nyumba za Walimu lazima tumalize hilo kwanza.
Waheshimiwa Wabunge, ndiyo maana mtaona katika maelekeo ya bajeti yetu itakayokuja ya mwaka mwingine wa fedha unaokuja, tutahakikisha suala zima la maboma sio suala katika sekta ya elimu peke yake hali kadhalika katika sekta ya afya tumalize hayo halafu ndiyo tuweze kuanza upya. Haiwezekani wananchi wamefanya nguvu kubwa za kutosha halafu nguvu zikapotea bure; Serikali imeliona hilo na ndio maana tuna mpango mkakati mpana sana kuondoa kero hiyo katika Jamhuri yote ya Tanzania.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Ukosefu wa nyumba za walimu katika maeneo ya vijijini unasababisha Walimu kuhama maeneo hayo na hivyo kusababisha upungufu mkubwa wa Walimu, pia Halmashauri nyingi hazina uwezo wa kujenga nyumba za Walimu za kutosha kwa kutumia fedha zao za ndani. Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga nyumba za Walimu wa shule za msingi vijijini hasa ikizingatia kuwa vijijini hakuna nyumba ambazo Walimu wanaweza kupanga?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Naomba kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kufanya bidii yote ya kutengeneza madawati kwa ajili ya watoto wa shule na kwa sababu madarasa hayatoshelezi kuna hatari ya madawati hayo kuharibika. Je, wakati haujafika sasa kuwa na mpango mzuri kama ulivyokuwa wa madawati kutengeneza madarasa hasa pale ambapo tunazingatia wananchi wameshajitolea kwa kiasi kikubwa? Je, ni mpango gani ambao Serikali unaweza ukaufanya ili tuwe na madarasa ya kutosha kuweka madawati ambayo tumeyatengeneza wote? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, kwanza naomba tuongeze juhudi kubwa za Watanzania; Mheshimiwa Rais alipotoa maelekezo kwamba tuondoe tatizo la kero wanafunzi kukaa chini na wengine kukaa katika mawe sasa watanzania tushirikiane kwa pamoja kutengeneza madawati.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri kwamba zoezi hili limefanikiwa kwa kiwango kikubwa sana lakini tulipongeze na Bunge lako hili kuhakikisha kwamba limeweza kutoa mgao wa madawati kwa Majimbo mbalimbali ili kuweza kupunguza ile kero ya madawati katika maeneo yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tatizo la kwanza ukipunguza maana yake tumetoa tatizo la wanaokosa shuleni, watoto elimu bure tumepata changamoto, tumepata madawati. Lakini sasa hivi tuna tatizo la vyumba vya madarasa hali kadhalika na vyoo, ndiyo maana katika mpango mkakati uliokuwepo hivi sasa katika bajeti hii ya mwaka wa fedha tunaoondoka nao tunaona kwamba kutakuwa na ujenzi wa madarasa katika maeneo mbalimbali na ujenzi wa matundu ya vyoo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, naomba niwahimize Watanzania wote, japokuwa Serikali itakuwa na mpango mpana sana kuhakikisha kwamba tunaondoa kero ya vyoo na kero ya vyumba vya madarasa hali kadhalika nyumba za Walimu kama nilivyosema awali, lakini niwaombe Watanzania tuendelee kushirikiana kwa pamoja vile vile kama tulivyofanya katika madawati, basi tufanye tena katika nyumba za Walimu na madarasa. Mwisho wa siku tukipata elimu bora, itakuwa ni kwa maslahi mapana ya nchi yetu. Ahsante sana.