Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO (K.n.y. MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI) aliuliza:- Sekta ya maliasili na utalii ni rasilimali inayobeba uchumi wa Tanzania, ikitumika vizuri kwa uendelevu, italeta maendeleo katika jamii na uchumi wa nchi kwa ujumla:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza kuipa kipaumbele sekta ya utalii? (b) Je, ni lini Serikali itaboresha mazingira ya kazi ya askari wanyamapori?

Supplementary Question 1

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Kwa kweli ni miongoni mwa Mawaziri ambao wanatoa majibu ambayo hayana ukakasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo naomba niulize swali dogo la nyongeza. Pamoja na maboresho hayo lakini kumekuwa na malalamiko kuhusu wale wapagazi kunyanyasika kwa kulipwa kiwango kidogo. Je, ni lini Seikali itaweka utaratibu wa kuboresha maslahi yao?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sikudhani Chikambo, Mbunge wa Viti Maalum kutokea Mkoa wa Ruvuma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimesema kwenye majibu yangu ya swali la msingi, kwamba tutaboresha hali za wafanyakazi wanaotoa huduma kwenye sekta ya utalii kwa ujumla wake na wapagazi ni sehemu yao. Watalii wakifika kufanya utalii katika nchi yetu mojawapo ya vitu vitakavyofanya wao wanaofika kwanza waendelee kubaki kwa muda mrefu zaidi lakini pia kuweza kuvutia watalii wengine kuja ni pamoja na aina ya huduma wanazozipata na huduma hizo zinatolewa na wale ambao wamepewa fursa hiyo na Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kuboresha mazingira ya watenda kazi hawa ni jambo la msingi na Serikali inalizingatia ili kwa kufanya hivyo tuweze kuvutia watalii zaidi na wakija waweze kukaa kwa muda mrefu zaidi kwa ajili ya tija ya mapato kwenye sekta ya utalii.

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO (K.n.y. MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI) aliuliza:- Sekta ya maliasili na utalii ni rasilimali inayobeba uchumi wa Tanzania, ikitumika vizuri kwa uendelevu, italeta maendeleo katika jamii na uchumi wa nchi kwa ujumla:- (a) Je, ni lini Serikali itaanza kuipa kipaumbele sekta ya utalii? (b) Je, ni lini Serikali itaboresha mazingira ya kazi ya askari wanyamapori?

Supplementary Question 2

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa askari wengi wa wanyamapori huwa wanapata athari ama wanafanya kazi katika mazingira magumu ya wanyama wakali. Je Serikali inawafidia nini wale askari wa wanyamapori ambao wanaathiriwa na wanyamapori wakali?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Faida Bakar, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze kwa kuwa imekuwa ni jambo la kawaida na linalojitokeza mara nyingi sana tunapowazungumzia askari wa wanyamapori tunazungumzia juu ya yale ambayo si ya maslahi zaidi kwao na mara nyingi ni lawama tu juu ya utendaji wao wa kazi. Kwa hiyo, kutokana na mwelekeo huu mpya wa Mheshimiwa Faida Bakar wa kuona kwamba na askari wa wanyamapori na wenyewe wana haki zao na maslahi yao yanapaswa kuboreshwa kutokana na kazi ngumu wanayoifanya natoa pongezi juu ya hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kujibu swali lake ni kwamba kwa mujibu wa kanuni na taratibu za ajira zilizopo na kwa mujibu wa sheria maslahi au haki za wafanyakazi hawa ambao ni askari wa wanyamapori zinazotokana na mazingira yao ya kazi zimezingatiwa. Ili kuongeza tija kwenye eneo hili huko tuendako na mkakati wa Kitaifa wa kuboresha zaidi ulinzi wa rasilimali zetu, Serikali inao mpango wa kuboresha hali na mazingira ya kazi hii ikiwa ni pamoja na ulipaji wa fidia, vifuta jasho pamoja na vifuta machozi kwa namna ambavyo itaonekana inafaa. Tutapitia utaratibu huo ili kuboresha mazingira na kuongeza ari zaidi kwa wafanyakazi wetu ikiwa ni pamoja na askari wa wanyamapori.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WATU WENYE WALEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini naomba nilipe taarifa Bunge lako Tukufu kwamba Serikali kupitia Bunge hili limeshapitisha Mfuko wa Fidia kwa wafanya kazi wote wanaoumia katika nchi yetu ya Tanzania wakiwa kazini. Mfuko huu ni kwa wafanyakazi ambao wapo kwenye private sector na wafanyakazi ambao wanafanya kazi ndani ya Serikali yetu. Katika Mfuko huo utaratibu umewekwa ambapo waajiri sasa wameanza kuchangia na pale ambapo mfanyakazi anapoumia kazini akiwa sekta binafsi ama Serikalini Mfuko huo sasa una jukumu la kulipa fidia kwa kuzingatia kanuni na taratibu zilizowekwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba niwahakikishie Wabunge, Ofisi ya Waziri Mkuu imeanza kusimamia utaratibu huo. Mfuko huo utaanza kazi hiyo mwaka huu ili kuweza kutatua tatizo la wafanyakazi wengi wanaoumia kazini wakiwemo hao askari wa wanyamapori pia.