Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Serikali imekuwa na azma nzuri kujenga zahanati katika kila kijiji na kituo cha afya katika kila kata nchi nzima:- (a) Je, ni lini Serikali itapanua Chuo cha MCH Mbulu kinachotoa cheti kuwa sehemu ya Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya na Binadamu kwa kuwa tayari Baraza la Madiwani limekubali kutumia ardhi yake ya akiba? (b) Je, kwa nini Serikali isitembelee chuo hicho ili kujionea fursa zilizopo? (c) Je, ni kwa nini pia Chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Tango FDC kisitumike kama chuo cha VETA kwa sababu kwa sasa hakina taaluma nzuri katika fani mbalimbali?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali kuhusu vyuo hivi viwili vilivyoko Wilayani Mbulu, nami naomba kuuliza maswali madogo ya nyongeza. Kwa kuwa katika Chuo cha MCH - Mbulu hadi sasa wanafunzi wetu wamesitishiwa huduma ya chakula kutokana na madeni makubwa walionayo wazabuni. Je, ni lini Serikali itarudisha huduma hiyo ya chakula ili wanafunzi wetu wasome kwa amani? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mbulu kuna jengo la ghorofa lililojengwa takribani miaka mitatu na liko chini ya kiwango na kwa sasa halitoi huduma iliyokusudiwa. Je, Serikali inachukua hatua gani kuja kubomoa hilo jengo na kujenga jengo lingine jipya ili liweze kutoa huduma kwa hospitali yetu na chuo kwa ujumla?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza linahusu chakula kwa wanafunzi wa Chuo cha Mbulu. Kwa mwaka mmoja uliopita, Serikali iliondoa utaratibu wa kupeleka bajeti ya chakula kwenye vyuo vyote vya MCH nchini na vyuo vyote ambavyo viko chini ya Serikali na badala yake huduma hizo zimekuwa zikitolewa na sekta binafsi kwa makubaliano na miongozo maalum inayotolewa na Serikali. Kwa maana hiyo, chuo hiki kinapaswa kifuate utaratibu huo mpya wa Serikali ili wanafunzi wapate huduma hiyo kutoka kwa washitiri binafsi.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la jengo, kwa sababu ni swali jipya na jengo hilo silifahamu vizuri, naomba nisitoe commitment yoyote ile, ila nimuahidi tu Mheshimiwa Issaay kwamba tutaongozana ama nitamkuta Jimboni baada ya Bunge la bajeti ili nilitembelee jengo lenyewe, nijue ni mradi wa nani, chanzo cha fedha za kutekeleza mradi huo ni kipi na niweze kujua nitamshauri vipi yeye pamoja na uongozi mzima wa Halmashauri ya Mbulu ili tuweze kuona mradi huo ukitekelezeka kwa manufaa ya umma.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Serikali imekuwa na azma nzuri kujenga zahanati katika kila kijiji na kituo cha afya katika kila kata nchi nzima:- (a) Je, ni lini Serikali itapanua Chuo cha MCH Mbulu kinachotoa cheti kuwa sehemu ya Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya na Binadamu kwa kuwa tayari Baraza la Madiwani limekubali kutumia ardhi yake ya akiba? (b) Je, kwa nini Serikali isitembelee chuo hicho ili kujionea fursa zilizopo? (c) Je, ni kwa nini pia Chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Tango FDC kisitumike kama chuo cha VETA kwa sababu kwa sasa hakina taaluma nzuri katika fani mbalimbali?

Supplementary Question 2

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Pamoja na majibu hayo ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, katika Jimbo la Mafinga wananchi wa Kijiji cha Lungemba wamepisha eneo kwa ajili ya upanuzi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Lungemba na uthamini umeshafanyika. Je, ni lini sasa Serikali itawalipa wananchi wale ambao wamejitolea ardhi yao kwa ajili ya upanuzi wa Chuo cha Maendeleo ya Lungemba?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri kabla ya Bunge la bajeti nilifika Jimboni kwa Mheshimiwa Chumi na nafahamu miradi mbalimbali ambayo inatekelezwa pale. Kama kumbukumbu zangu ziko sahihi tayari zimetengwa shilingi milioni 200 kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi wa eneo lile. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kulikuwa kuna mgogoro kidogo, kuna baadhi ya wananchi walikubali kuchukua hiyo fidia ambayo walikuwa wanapewa, lakini kuna baadhi ya wananchi hawakukubaliana na fidia ambayo ilikuwa inatolewa na hivyo hawakuzichukua na ulipaji wa fidia ukawa kama umesimama. Hivyo, namsihi Mheshimiwa Mbunge, akishirikiana na viongozi wenzake kwenye Halmashauri, watumie jitihada za kuwashawishi wananchi wakubaliane na fidia ambazo zinatolewa na Serikali ili chuo hicho kiweze kuendelezwa na wananchi waweze kupata huduma inayostahili. Nitoe rai kwa wananchi wa eneo lile kwamba miradi ya maendeleo inapokuja kwenye maeneo yao waikumbatie na badala ya kukwepa fidia washirikiane na Serikali ili kuendeleza miradi husika.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Serikali imekuwa na azma nzuri kujenga zahanati katika kila kijiji na kituo cha afya katika kila kata nchi nzima:- (a) Je, ni lini Serikali itapanua Chuo cha MCH Mbulu kinachotoa cheti kuwa sehemu ya Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya na Binadamu kwa kuwa tayari Baraza la Madiwani limekubali kutumia ardhi yake ya akiba? (b) Je, kwa nini Serikali isitembelee chuo hicho ili kujionea fursa zilizopo? (c) Je, ni kwa nini pia Chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Tango FDC kisitumike kama chuo cha VETA kwa sababu kwa sasa hakina taaluma nzuri katika fani mbalimbali?

Supplementary Question 3

MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Katika Wilaya yangu ya Kibondo, Jimbo la Muhambwe, kuna Chuo cha MCH ambacho kwa muda mrefu sasa karibu miaka mitano wamejaribu kujenga maabara, wamekwishafikia mpaka ngazi ya kupaua, wamekwishaweka mbao mwaka wa pili na nusu sasa na hakijapauliwa. Ni lini Serikali itapeleka pesa kwa ajili ya kupaua jengo hilo la maabara?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini? Ni pale ambapo uwezo wetu wa kibajeti utaruhusu.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:- Serikali imekuwa na azma nzuri kujenga zahanati katika kila kijiji na kituo cha afya katika kila kata nchi nzima:- (a) Je, ni lini Serikali itapanua Chuo cha MCH Mbulu kinachotoa cheti kuwa sehemu ya Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya na Binadamu kwa kuwa tayari Baraza la Madiwani limekubali kutumia ardhi yake ya akiba? (b) Je, kwa nini Serikali isitembelee chuo hicho ili kujionea fursa zilizopo? (c) Je, ni kwa nini pia Chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Tango FDC kisitumike kama chuo cha VETA kwa sababu kwa sasa hakina taaluma nzuri katika fani mbalimbali?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba niulize swali la nyongeza, kwa kuwa, hali ya Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Tango, FDC inafanana na kile cha Mtawanya, kilichopo Mkoani Mtwara, je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuboresha miundombinu ya chuo hicho lakini pia kuboresha utoaji wa taaluma katika Chuo hicho cha Maendeleo ya Wananchi Mkoani Mtwara?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, Serikali ina mpango mkakati mpya kabisa wa kufanya maboresho kwenye Vyuo vyote vya Maendeleo ya Wananchi hapa nchini. Mpango wetu ni kwamba, tayari tumeanza mazungumzo na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ili tuweze kuvihamishia kwenye Wizara hiyo badala ya kubaki navyo sisi kwenye Wizara yetu. Lengo hasa ni kuboresha mitaala inayotolewa kwenye vyuo hivi lakini kuboresha administration ya vyuo hivi na kuongeza bajeti. Kwa maana hiyo, Mheshimiwa Chikota, mpango tulionao ndiyo huo.