Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA (K.n.y MHE. RAPHAEL J. MICHAEL) aliuliza:- Hospitali ya Mawenzi ambayo ni ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro inakabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile uchakavu wa miundombinu yake, samani, mlundikano mkubwa wa wagonjwa kwa sababu Manispaa ya Moshi haina Hospitali ya Wilaya, upungufu wa Madaktari, wauguzi na wahudumu wengine wa afya:- (a) Je, ni lini hospitali hiyo itafanyiwa ukarabati ili iweze kufanya kazi zake kwa ufanisi na kuiongezea watumishi niliowataja? (b) Je, ni lini Serikali itakubali ombi la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi la kujenga Hospitali ya Wilaya? (c) Je, Serikali itasaidiaje Hospitali ya Mawenzi iweze kupata mkopo kutoka Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) ili iweze kuboresha miundombinu yake?

Supplementary Question 1

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Raphael Michael, Mbunge wa Moshi Mjini ametoka nje, naomba nitumie nafasi hii kwa sababu swali alilouliza linafanana kabisa na suala ambalo liko Tabora katika Hospitali yetu ya Mkoa ya Kitete, naomba niulize swali kwa Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, Hospitali yetu ya Mkoa wa Tabora ya Kitete ina tatizo lile lile la mlundikano wa wagonjwa kama ambavyo iko Moshi Mjini. Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Hospitali ya Wilaya inajengwa Tabora ili kuweza kupunguza huu mlundikano wa wagonjwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, Hospitali ya Mkoa wa Tabora ya Kitete ina upungufu mkubwa sana wa Madaktari, tuna Daktari Bingwa mmoja tu. Serikali inajipanga vipi kuhakikisha Hospitali ya Mkoa wa Tabora ya Kitete inapata Madaktari Bingwa wa kutosha?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, watu wanasema hata katika mpira vilevile, ikitokea mpira unapigwa golini halafu mtu kaondoka wewe piga goli tu. Kwa hiyo, naomba nimpongeze kwa hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Tabora ya Kitete aliyoizungumzia kwamba kwa sababu changamoto ni nyingi tuna mpango gani wa kuanzisha Hospitali ya Wilaya. Katika hili naomba nielekeze, tuweke vipaumbele katika Manispaa zetu kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Serikali iko tayari kabisa kushirikiana na wananchi wa Tabora ili kuhakikisha wananchi wa Tabora wanapata afya njema.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, napenda kuwashukuru wana Tabora kwa ujumla wao, kwa sababu nilipopita kule Tabora nimeona shughuli mbalimbali za kusimamia miradi. Nilitembelea Kituo cha Afya cha Itobo na kile kingine cha Bukene nimeona vifaa vya upasuaji vimewekwa kwa ajili ya akinamama. Kwa hiyo, juhudi zile wakati tukifanya mpango wa pamoja sasa kuimarisha Mkoa wa Tabora, kwa sababu tukiangalia sehemu ile hata watu kutoka Kigoma watakaopata matatizo wanaweza wakaja pale, ni vema kabisa tukaendelea kuweka nguvu. Katika mpango wetu mkakati wa Serikali kuimarisha Hospitali za Mikoa kupitia ule mradi mkubwa, nadhani tutaelekezana hapo baadaye jinsi gani tutafanya na Tabora ipewe kipaumbele kikubwa zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la watumishi kwamba hatuna Madaktari Bingwa, bahati nzuri katika mchakato tutakaoufanya ni pamoja na kuhakikisha Madaktari Bingwa wanafika katika kanda mbalimbali. Imeonekana mara nyingi sana Madaktari Bingwa wanaishia katika maeneo ya miji mikubwa sana hasa Dar es Salaam. Katika maeneo ya pembezoni Madaktari Bingwa hasa madaktari wa magonjwa ya akinamama (gyno) wanakosekana.
Mheshimiwa Naibu Spika, hili nililigundua hata nilipofika katika Mkoa wa Singida, kuna hospitali nzuri lakini Madaktari Bingwa wamekosekana na hata nilivyofika Songea jambo hili nililiona. Mpango wetu ni kwamba kupitia Wizara ya Afya vilevile tutafanya mkakati sasa kuweka mipango vizuri ili Madaktari Bingwa waweze kufika maeneo mbalimbali ikiwemo na Tabora, lengo kubwa wananchi wetu wapate huduma bora.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, TAMISEMI, napenda kumthibitishia Mheshimiwa Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini kwamba, Tabora ni mojawapo ya mikoa tisa ambayo Wizara ya Afya imeifanyia tathmini kwamba inayo uhaba mkubwa wa Madaktari Bingwa pamoja na Mikoa ya Kigoma, Mara, Katavi, Rukwa na Simiyu. Kwa hiyo, tutakapopanga Madaktari kwa mwaka huu wa fedha, tutatoa kipaumbele kwa Mkoa wa Tabora na mikoa mingine nane.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niombe Madaktari wote na wataalamu wa afya ambao mnatarajia kuomba kazi Serikalini kwamba tutawapanga katika mikoa hiyo tisa ndiyo kipaumbele chetu. Kwa hiyo, kama wanataka kukaa Dar es Salaam wajue hatutachukua daktari ambaye anataka kukaa Dar es Salaam. Nakushukuru.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA (K.n.y MHE. RAPHAEL J. MICHAEL) aliuliza:- Hospitali ya Mawenzi ambayo ni ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro inakabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile uchakavu wa miundombinu yake, samani, mlundikano mkubwa wa wagonjwa kwa sababu Manispaa ya Moshi haina Hospitali ya Wilaya, upungufu wa Madaktari, wauguzi na wahudumu wengine wa afya:- (a) Je, ni lini hospitali hiyo itafanyiwa ukarabati ili iweze kufanya kazi zake kwa ufanisi na kuiongezea watumishi niliowataja? (b) Je, ni lini Serikali itakubali ombi la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi la kujenga Hospitali ya Wilaya? (c) Je, Serikali itasaidiaje Hospitali ya Mawenzi iweze kupata mkopo kutoka Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) ili iweze kuboresha miundombinu yake?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa niaba ya wananchi wa Lupembe.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lililopo Moshi Mjini na maeneo mengine ndilo ambalo lipo katika Jimbo la Lupembe, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Naomba kujua ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Lupembe kwa kuwa hatuna hospitali katika jimbo na halmashauri ile. Tuna vituo vya afya viwili tu na wananchi wengi wanasafiri umbali mrefu zaidi ya kilomita 80 kwenda kutafuta hospitali. Kwa hiyo, ni lini sasa Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya katika eneo la Matembwe?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, analozungumza Mbunge ni kweli, ule Mkoa wa Njombe ni mpya na nilipofika pale katika Hospitali ya Kibena nimekuta changamoto nyingi kwa sababu watu wote wanakuja katika Hospitali ya Kibena hata wa kutoka maeneo ya Mheshimiwa Mbunge ambapo imekuwa ni kero kubwa sana na nashukuru na Wizara ya Afya vilevile kupitia viongozi wake wakuu walifika pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kufanya katika eneo lile kunakuwa na Hospitali ya Wilaya, nadhani sisi kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumelisikia hili lakini nimsihi Mheshimiwa Mbunge mchakato wa ujenzi wa Hospitali hiyo ya Wilaya uanzie kwao kwa sababu kuna suala la kutenga eneo na kuweka kipaumbele hiki cha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Tukifanya hivyo na sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI hatutasita kushirikiana na wananchi na viongozi katika eneo hilo kuhakikisha wananchi wanapata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana jana Kamati ya Bajeti ilikutana na Wizara yetu na Wizara ya Afya, lengo kubwa ni kuweka mipango kabambe ya kusaidia suala hili ili wananchi wote wapate huduma nzuri. Katika mipango hii kabambe inayokuja sasa naamini kwamba Mheshimiwa Mbunge akijipanga vizuri katika Jimbo lake na najua kwamba amejipanga vizuri sana, tutahakikisha kwamba hii mipango ya pamoja inakwenda vizuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, jana Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumetoa maelekezo kupitia kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri 181 katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, waainishe maboma ambayo hayajamaliziwa na changamoto mbalimbali ili Bunge hili lije katika mpango mkakati wa huduma ya afya katika ujenzi wa miundombinu. Kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Mbunge waanze kufanya ile needs analysis na kutenga eneo kwa ajili hiyo na tutaona ni jinsi gani tutashirikiana katika ujenzi wa hospitali hiyo.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA (K.n.y MHE. RAPHAEL J. MICHAEL) aliuliza:- Hospitali ya Mawenzi ambayo ni ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro inakabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile uchakavu wa miundombinu yake, samani, mlundikano mkubwa wa wagonjwa kwa sababu Manispaa ya Moshi haina Hospitali ya Wilaya, upungufu wa Madaktari, wauguzi na wahudumu wengine wa afya:- (a) Je, ni lini hospitali hiyo itafanyiwa ukarabati ili iweze kufanya kazi zake kwa ufanisi na kuiongezea watumishi niliowataja? (b) Je, ni lini Serikali itakubali ombi la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi la kujenga Hospitali ya Wilaya? (c) Je, Serikali itasaidiaje Hospitali ya Mawenzi iweze kupata mkopo kutoka Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) ili iweze kuboresha miundombinu yake?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa niliwahi kumlalamikia Mheshimiwa Naibu Waziri wakati tunakwenda Mpwapwa kwamba kuna vituo viwili vya afya ambavyo havijakamilika sasa ni miaka 10, Kituo cha Afya cha Mima na Kituo cha Afya cha Mbori na bajeti haijatengwa zaidi ya miaka 10. Je, unawaeleza nini wananchi wa maeneo hayo ya Mima na Mbori na kwamba vituo hivyo vitakamilika lini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, siku tulipokwenda pale Mpwapwa nilipokuwa na Mzee Lubeleje nikawaambia watu wa Mpwapwa, Mzee Lubeleje huyu nimemwita kama greda la zamani lakini makali yaleyale, alikuwepo na sasa amerudi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nlipofika pale Mpwapwa tulitoa maelekezo kwamba licha ya hivyo vituo anavyozungumza lakini Hospitali yao ya Wilaya walikuwa hawajaanza kutumia mifumo ya electronic. Siku nne zilizopita nimekwenda Hospitali ya Mpwapwa na mimi mwenyewe nilikuwa mteja wa kwanza kukata risiti ya mfumo wa electronic. Kwa hiyo, Mzee Lubeleje namuunga mkono kwanza katika hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo nini tumefanya? Ndiyo maana nimeeleza toka mwanzo tuna maboma mengi yamekaa muda mrefu, mengine yamekaa miaka saba, mengine miaka nane, wananchi wameshafanya juhudi ya awali, ndiyo maana nimesema hapa jana Kamati ya Bajeti ya Bunge hili ilikaa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Wizara ya Afya na jana tumeshatoa maelekezo kwenda kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri 181 waainishe maboma yote yamefikia hatua kiasi gani na yanahitaji fedha kiasi gani, lengo ni maboma yote haya yaweze kwisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukimaliza maboma yote tutakuwa tumepiga hatua moja kubwa sana. Imani yangu ni kwamba, haya maeneo mawili ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyasema ni miongoni mwa mambo ambayo tunaenda kuyafanyia kazi katika ule mpango mkakati mkubwa. Kwa hiyo, naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imejipanga katika hili na tunajipanga siyo Wizara ya Afya peke yake, siyo TAMISEMI peke yake halikadhalika Kamati ya Bunge ya Bajeti jana kikao hicho kilifanyika.