Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Katika Mwaka wa Fedha 2014.15 Serikali iliunganisha umeme kwenye vijiji vinne tu katika Wilaya ya Hanang; hata hivyo, Mwaka 2015/2016, Serikali iliahidi kuunganisha umeme vijiji vingine 19:- Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi hiyo, ambayo inasubiriwa kwa hamu na wananchi wa Wilaya ya Hanang?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu mazuri yenye kuwaletea matumaini wananchi wa Hanang. Sasa naomba niulize maswali madogo mawili, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kwa kutambua kwamba, Wilaya ya Hanang ilisahauliwa katika Awamu ya kwanza na ya pili, sasa atakubaliana na mimi, na ninahakika atakubaliana na mimi kwamba, vijiji hivyo vya Hanang alivyovitaja sasa vitakuwa Awamu ya tatu viwe vya kwanza katika kupewa umeme katika Awamu hiyo ya tatu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; najua kwamba, awamu ya kwanza na ya pili ilipewa vijiji vichache mpaka sasa havijapata umeme. Je, Naibu Waziri atakubaliana na mimi kwamba, katika muda mfupi unaokuja vijiji hivyo vichache vipate umeme basi, ili viwape matumaini wananchi wa Hanang?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nirekebishe kidogo kwamba, katika Jimbo la Hanang kwa kweli, hatukupeleka vijiji vingi! Ni vijiji saba tu ambavyo tulivipatia umeme kwenye REA awamu ya pili, lakini niongezee kwa Mheshimiwa Mbunge kama alivyosema vijiji 19 ambavyo vilikusudiwa kupewa umeme kwenye REA awamu ya pili vyote vitakamilika ndani ya siku 20 zilizobaki. Kwa hiyo, awamu ya pili itakamilisha vijiji vyako Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu na vijiji vingine 44 ulivyoomba na vyenyewe vitapatiwa umeme kwenye REA awamu ya tatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu vile Vijiji vya Kisambalang, Dang‟aida, Dawidu, Mwanga na Wandolendode, vyote vitapatiwa umeme katika awamu ya tatu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusiana na uhakika kwamba, je, muda uliobaki kweli kazi iliyobaki itakamilika?
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kufunga miundombinu mikubwa kwenye Jimbo la Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu imekamilika, kazi iliyokuwa imebaki sasa ni kusambaza transformer kama 10 ambazo tuliahidi. Bado transformer tano kukufungia Mheshimiwa Mary Nagu, mwezi ujao nadhani tutakamilisha transformer zote 10.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini baada ya kusema hayo, vile vijiji vingine 44 ambavyo umeviomba pamoja na shule za sekondari, vituo vya afya kwa bilioni 15.8 tulizokutengea nadhani tutakamilisha kazi yote Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge, pesa ambazo mmetutengea kwa mwaka huu, bilioni 587 ambazo ni kwa ajili ya kuwasambazia umeme vijijini, zote tutazitumia kwa kazi hizo na vijiji vyote vilivyobaki vitapata umeme kwenye mradi kabambe wa REA awamu ya tatu unaoanza mwezi Julai mwaka huu.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Katika Mwaka wa Fedha 2014.15 Serikali iliunganisha umeme kwenye vijiji vinne tu katika Wilaya ya Hanang; hata hivyo, Mwaka 2015/2016, Serikali iliahidi kuunganisha umeme vijiji vingine 19:- Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi hiyo, ambayo inasubiriwa kwa hamu na wananchi wa Wilaya ya Hanang?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kazi nzuri ambayo Wizara hii imefanya sasa naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, kuna baadhi ya Vijiji vikiwemo Ng‟ang‟ange, Pomelini, Masege, Mwatasi, Kesamgagao, Masisilo, Ukumbi na vijiji vingine umeme tayari umeshafungwa na umefika, sasa tatizo ni kuwasha! Ni lini utawashwa ili wananchi sasa waendelee kuishi kwa matumaini na mategemeo makubwa kwa Serikali hii ya Awamu ya Tano?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, yeye suala lake ni kuwasha tu, lakini miundombinu yote ipo. Nimeshaongea na Meneja, wiki ijayo Jumanne atamwashia Mheshimiwa Mwamoto katika vijiji vyake vyote. Kwa hiyo, kwake umeme utawaka bila wasiwasi.