Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mboni Mohamed Mhita

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. MBONI M. MHITA (K. n. y. MHE. SHABAN O. SHEKILINDI) aliuliza:- Jimbo la Lushoto linakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji hususan katika maeneo ya Umiri, Makanya, Kwemashai, Gare, Mlola, Mbwei, Malibwi na Kilole:- Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi hao maji safi na salama ili waondokane na adha hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo ya maji katika Jimbo la Lushoto yanafanana sana na matatizo ya Jimbo la Handeni Vijijini. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuweza kufanya ziara katika Jimbo la Handeni Vijijini na kujionea matatizo ya Maji katika Jimbo hili? Je, yuko tayari ama anatoa commitment gani kwa fedha ambazo amesema zitatoka kwa miradi ya maji katika Jimbo la Lushoto? Ahsante sana.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na swali la mwisho. Mheshimiwa Naibu Waziri anatoa commitment gani; tayari Bunge lako limeshapitisha bajeti ya Mwaka wa Fedha wa 2016/2017 na katika bajeti hiyo kuna shilingi bilioni 3.4 kwa ajili ya Lushoto, kwa hiyo, hakuna commitment zaidi ya hiyo. Nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge sasa ashirikiane na Halmashauri ili kuendelea sasa kufanya matumizi ya hizi fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo ya Handeni. Tayari tuna mradi wa HTM ambao utekelezaji wake unaanza mwaka wa fedha unaokuja. Ni mradi mkubwa ambao utapitia maeneo mengi katika Mji wa Handeni na hatimaye kuhakikisha kwamba, tunakamilisha mradi huu. Maeneo ambayo hayatafikiwa na mradi huo Halmashauri zihakikishe kwamba, zinatumia fedha iliyopangwa kwa ajili ya ama kuchimba visima au kutengeneza mabwawa kwa ajili ya kuhakikisha kwamba, wananchi wote wa eneo hilo wanapata huduma ya maji. Kama fedha hazitatosha zilizopangwa basi ni wajibu wa Halmashauri kuhakikisha wanaleta maombi ili tuweze kutenga fedha katika Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. MBONI M. MHITA (K. n. y. MHE. SHABAN O. SHEKILINDI) aliuliza:- Jimbo la Lushoto linakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji hususan katika maeneo ya Umiri, Makanya, Kwemashai, Gare, Mlola, Mbwei, Malibwi na Kilole:- Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi hao maji safi na salama ili waondokane na adha hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Tatizo la Lushoto linalingana kabisa na Korogwe Vijijini hasa kwenye Mji Mdogo wa Mombo. Serikali kwa kupitia Benki ya Dunia ilitenga milioni 900 kwa mradi wa maji ambao unakwenda kutoka Vuga mpaka Mombo kwa kupitia Mombo kwenda Mlembule. Mradi huu umekamilika kwa asilimia 80, tatizo ni kwamba, wananchi wanaolinda chanzo cha maji katika Wilaya ya Bumbuli au katika Mji wa Bumbuli ambao wanatoka Vuga walikuwa wanaomba wapatiwe maji na sasa hivi Serikali iliahidi kwamba, wale wananchi wanaolinda chanzo cha maji watapatiwa maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini mradi huu wa Mombo ambao Serikali imetumia gharama zaidi ya milioni 900, lakini mpaka sasa hivi haujakamilika?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maji na Umwagiliaji katika Sera yake na katika mipango yake imeweka mpango kwamba, Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/2017 kwanza inakamilisha miradi iliyokuwa inaendelea kabla haijaingia katika miradi mipya. Kwa hiyo, mradi wako Mheshimiwa Mbunge ambao umeuita ni mradi wa Benki ya Dunia na imebakia kidogo mradi huo utakamilika, lakini pia ni sambamba na kuwapelekea maji wananchi wa eneo ambalo ni chanzo cha maji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yetu imepanga kwamba, maeneo yote ambayo maji yanatoka katika lile eneo, basi maji lazima na huko yapatikane. Kama utaratibu huo haukuwepo, naomba Mheshimiwa Mbunge pamoja na
Halmashauri washauriane ili mwaka wa fedha 2017/2018 tuweze kutenga fedha kuhakikisha wale wananchi wa kwenye chanzo cha maji wanapata maji.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. MBONI M. MHITA (K. n. y. MHE. SHABAN O. SHEKILINDI) aliuliza:- Jimbo la Lushoto linakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji hususan katika maeneo ya Umiri, Makanya, Kwemashai, Gare, Mlola, Mbwei, Malibwi na Kilole:- Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi hao maji safi na salama ili waondokane na adha hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa, vilevile katika Jimbo langu la Mpwapwa kuna matatizo makubwa sana ya maji katika Vijiji vya Mima, Chitemo, Berega, Nzase, Lupeta, Bumila na Makutupa na kulikuwa na mradi mkubwa sana wa maji na mpaka sasa umechakaa. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuusaidia ule mradi uanze kuhudumia wananchi wa vijiji hivyo?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ipo tayari na ndiyo maana inatenga bajeti na imetenga bajeti kwenye Wilaya zote ikiwemo pamoja na Wilaya ya Mheshimiwa Lubeleje. Katika malengo yetu tunakamilisha miradi inayoendelea, lakini pia, tunaomba Halmashauri mtuletee maombi ya fedha kwa ajili ya ukarabati wa miradi ya zamani ili iendelee kufanya kazi kama ambavyo nilijibu katika swali la msingi la Mheshimiwa Abood kule Morogoro kwamba, tunataka tuhakikishe kwamba, miradi yote inayoendelea inakarabatiwa, ili kuondoa matatizo ya uvujaji wa yale mabomba unaosababisha maji kupotea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa tu kwamba, tuko pamoja na yeye na Serikali iko pamoja na Halmashauri yake. Kinachotakiwa watumie fedha tuliyowapa, lakini mwaka wa fedha utakaokuja basi walete maombi tena ili tuweze kutoa hiyo fedha.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MBONI M. MHITA (K. n. y. MHE. SHABAN O. SHEKILINDI) aliuliza:- Jimbo la Lushoto linakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji hususan katika maeneo ya Umiri, Makanya, Kwemashai, Gare, Mlola, Mbwei, Malibwi na Kilole:- Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi hao maji safi na salama ili waondokane na adha hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa, Bunge lililopita kuna fedha zilikuwa zimetengwa kwa ajili ya ile miradi 10 ya World Bank katika Vijiji Mji vya Mji wa Korogwe ikiwemo Lwengela Relini, Lwengela Darajani na Msambiazi. Je, Serikali ina mpango gani kwa sababu kwenye bajeti hii sijaona hiyo fedha? Safari iliyopita hawakupewa zile fedha, safari hii wana mkakati gani kuhakikisha kwamba vijiji hivi vinachimbiwa vile vile visima virefu kama ambavyo ilikuwa imepangwa?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya Miradi ya World Bank ambayo haikukamilika, kama ambavyo nimeshajibu awali kwamba, katika bajeti tuliyoitenga mwaka huu, basi tuhakikishe kwamba tunakamilisha kwanza ile miradi ambayo haikukamilika kabla hatujaingia kwenye miradi mipya.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, natambua pia, kwamba, eneo la Korogwe lina matatizo makubwa ya maji, baadhi ya vijiji bado havijapata. Kupitia mradi wa HTM ambao chanzo chake nacho kinatoka katika ule Mto Ruvu tutahakikisha kwamba, sehemu ya maji hayo yanapita kwenye Vijiji vya Korogwe ili kuhakikisha kwamba, wananchi wote wa eneo la Korogwe wanapata maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ambayo hayatafikiwa na mradi tuhakikishe kwamba tunashirikiana na Halmashauri kwa ajili ya kuchimba visima au kujenga mabwawa. Kama fedha haipo katika Mwaka wa Fedha 2016/2017 basi wahakikishe wanaharakisha kuleta maombi, ili katika bajeti ya mwaka 2017/2018 tunatoa fedha. Katika hiki kipindi nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutatembelea hilo eneo, tutatembea kuja kujionea hali halisi.