Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wetu na Watanzania zaidi ya 75% wanategemea kilimo kama ajira ya kuendesha maisha yao:- Je, ni lini Serikali itaanzisha miradi mikubwa ya kuhifadhi maji (water reserves) ili kuwa na scheme itakayowezesha wakazi wa Kata za Mnazi, Lunguza na Mng‟aro kuendesha shughuli zao za kilimo msimu mzima?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Waziri, lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Kwa kuwa skimu ambazo amezitaja zinapita nje ya Vijiji vya Langoni A, Langoni B, Mkundyambaro na Mkundyamtae, je, Serikali haioni sasa kwamba kuna umuhimu wa kipekee wa kuwapa wananchi wa vijiji hivyo bwawa la kuhifadhia maji?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne tarehe 10 Julai, 2014, alipita katika Kata ya Mng‟aro na akatoa ahadi kuboresha miundombinu ya maji ambayo ni chakavu toka mwaka 1972. Upembuzi yakinifu umefanyika, gharama ya ukarabati ni shilingi 157,200,050/=Mheshimiwa Mwenyekiti, . Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kutimiza agizo hilo la Rais? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Rashid Shangazi, tangu niteuliwe kuwa Naibu Waziri ameshakuja ofisini mara nne kwa ajili ya kufuatilia miundombinu ya umwagiliaji pamoja na maji ya kunywa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, swali (a) kwamba Serikali inafanya upembuzi wa awali ili kuweza kubaini maeneo mengine yanayoweza kujengwa mabwawa. Kwa sababu hiyo, kwenye utafiti huo utahusisha pia vijiji ambavyo Mheshimiwa Shangazi amevitaja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kuna ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne ya kukarabati miundombinu ambayo imefanya kazi kwa muda mrefu na inaelekea kupunguza ufanisi wake. Mheshimiwa Rais aliahidi kutoa shilingi milioni 152 kwa ajili ya ukarabati huo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi hiyo tumeipokea na tutaifanyia kazi.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wetu na Watanzania zaidi ya 75% wanategemea kilimo kama ajira ya kuendesha maisha yao:- Je, ni lini Serikali itaanzisha miradi mikubwa ya kuhifadhi maji (water reserves) ili kuwa na scheme itakayowezesha wakazi wa Kata za Mnazi, Lunguza na Mng‟aro kuendesha shughuli zao za kilimo msimu mzima?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii adimu ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kama ilivyo Wilaya na Mlalo, Wilaya ya Hanang‟ ina bwawa ambalo lilikuwa likikusanya maji ya Mlima Hanang‟ kwa scheme ambazo zinaweza zikatumika kwa umwagiliaji. Ni miaka mitano sasa tumekuwa tukiomba bwawa hilo likarabatiwe na bado hatujafanikiwa.
Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kunisaidia kuwahakikishia wananchi wa Hanang‟ kwamba kama anavyoomba Mbunge wa Mlalo na Mbunge wa Jimbo la Hanang‟ analiomba hilo.

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba nimjibu Mheshimiwa Mary Nagu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nilikumbushe Bunge lako kwamba kupitia Bunge hili tulipitisha Sheria Namba 5 ya mwaka 2013, Sheria ya Umwagiliaji na pia tulianzisha Tume ya Umwagiliaji. Katika mwaka wa fedha 2015/2016, Serikali imetenga bilioni 53 kwa ajili ya kuendeleza na kukarabati mabwawa ambayo yanajihusisha na shughuli za umwagiliaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafanyia mapitio, mabwawa haya yote ambayo yanaweza kuongeza maeneo ya umwagiliaji, lakini pia mabwawa mengine ambayo yatasaidia wananchi wetu kuweza kupata maji. Ni azma ya Serikali ya Awamu ya Tano kwamba tunataka tuongeze kiwango cha upatikanaji wa maji vijijini na mijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, sehemu zingine tutatumia mabwawa, sehemu zingine tutatumia mito na sehemu nyingine tutatumia maziwa. Kwa hiyo, kazi hii tutakwenda kufanya, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba nitafika huko kwenda kuangalia bwawa analoliomba ili kusudi tuweze kuona nini kifanyike. Ahsante.