Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Barabara ya Murushaka ni kiungo muhimu kwa Karagwe na Kyerwa na ni barabara muhimu sana kiuchumi, lakini barabara hiyo ni mbovu sana wala haipitiki kabisa:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kutengeneza barabara hiyo ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wa Kyerwa? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kwa lami barabara hiyo kwa sababu zaidi ya magari asilimia 90 yanayotoka Uganda na Kyerwa hutumia barabara hiyo iliyosahaulika?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza sijaridhika na majibu ambayo amenipa Mheshimiwa Naibu Waziri kwa sababu kusema hii barabara inapitika kila wakati si kweli! Barabara hii mwaka wa jana mzima ilikuwa ni barabara mbovu imejaa mashimo, magari yote yanayopita barabara ile yanaharibika sana. Kwa hiyo, kuna taarifa ambazo wamekuwa wakiletewa ambazo si sahihi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri. Swali la kwanza; je, yuko tayari yeye mwenyewe binafsi kwenda kuitembelea barabara ile na kuiona ili aone umuhimu wake kwa sababu taarifa ambazo wamekuwa wanaletewa sio za kweli?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Mheshimiwa Rais akiwa pale Nkwenda kwenye kampeni aliiona barabara ile ikiwa na umuhimu kwa kuwa barabara hii inapita katikati ya Wilaya. Aliahidi kutupa kilometa 20 akiingia tu madarakani. Hizo kilometa 20 zinaanza kujengwa lini? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikiri kwamba miongoni mwa Wabunge ambao wanakuja ofisini kila wakati kufuatilia ni pamoja na Mheshimiwa Bilakwate. Mheshimiwa Bilakwate ameifuatilia barabara hii na tumekuwa tukijaribu kuangalia katika hizi barabara mbili zote zinaanzia karibu sehemu moja kuishia karibu sehemu moja. Suala ni ipi kati ya hizi mbili ni muhimu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi kilichopita kama ambavyo tumeongea ofisini, ni kwamba uongozi wa Mkoa pamoja na Mbunge aliyepita waliona kwamba hii barabara ya kupitia Kigarama ndiyo ipewe umuhimu wa kwanza na hii ya kupitia Omurushaka nayo wakati Mheshimiwa Rais alipokuwa kule aliipa kipaumbele. Kwa hiyo, barabara zote mbili sisi kama Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano tumezichukua kwa umuhimu wake. Tutaanza na hii ambayo tumeshaanza kufanya kazi, tukiimaliza hii tutakuja kukamilisha hii nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wakati tunasubiri kuanza hii ya pili ambayo ndiyo anayoifuatilia kwa umakini sana Mheshimiwa, tunamwomba sana akubali kwamba ile kazi tunayoifanya kwanza ya kuimarisha ule mlima maana tatizo kubwa liko pale mlimani hasa. Ombi lake la kwanza nalikubali, nitakuwepo naye huko, tukaongee na wananchi kuthibitisha ahadi ya kiongozi wetu mkuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wakati huo huo afahamu mazingira tuliyonayo kutokana na hizi barabara mbili ambazo zote zinaonekana zina kipaumbele lakini viongozi wa Mkoa na Mbunge aliyepita inaonekana hiyo nyingine ndiyo waliitanguliza zaidi. Sasa ni suala la kutafuta namna gani zote mbili twende nazo kwa sababu zote zina umuhimu wa pekee na zinatoa huduma kubwa.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Barabara ya Murushaka ni kiungo muhimu kwa Karagwe na Kyerwa na ni barabara muhimu sana kiuchumi, lakini barabara hiyo ni mbovu sana wala haipitiki kabisa:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kutengeneza barabara hiyo ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wa Kyerwa? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kwa lami barabara hiyo kwa sababu zaidi ya magari asilimia 90 yanayotoka Uganda na Kyerwa hutumia barabara hiyo iliyosahaulika?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba niulize swali dogo la nyongeza. Wakati wa kampeni, Mheshimiwa Rais aliwaahidi wananchi wa Jimbo la Singida Mjini kwamba atajenga barabara kwa kiwango cha lami ya kuunganisha Kata zote za pembeni. Sasa, je, mchakato huu wa kujenga barabara utaanza lini? Ahsante sana.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tumepewa ahadi zote ambazo viongozi wetu, Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Makamu wa Rais, walizitoa sehemu mbalimbali za nchi, ahadi zote tunazo. Tulichowekea fedha ili tuweze kuanza kutekeleza katika mwaka huu wa kwanza tunaoanza ni zile barabara ambazo zilishaanza kufanyiwa kazi toka zamani na wakandarasi wako site.
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani tutakubaliana kwamba ni vyema tukamaliza kwanza ile kazi iliyoanza siku nyingi za nyuma ili wakandarasi wasiendelee kupata fedha bila kufanyia kazi kwa kutopewa fedha za ujenzi na hivyo wanaendelea kukaa pale bila kufanya kazi na tunalazimika kuwalipa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kipaumbele cha kwanza ni kukamilisha barabara ambazo zilianza. Nawahakikishieni Waheshimiwa Wabunge kwamba barabara zote ambazo Mheshimiwa Rais pamoja na Mheshimiwa Makamu wa Rais waliziahidi na bahati nzuri tumeshazipata, tutahakikisha tunazipangia ratiba ya utekelezaji katika kipindi kitakachofuata.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Barabara ya Murushaka ni kiungo muhimu kwa Karagwe na Kyerwa na ni barabara muhimu sana kiuchumi, lakini barabara hiyo ni mbovu sana wala haipitiki kabisa:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kutengeneza barabara hiyo ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wa Kyerwa? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kwa lami barabara hiyo kwa sababu zaidi ya magari asilimia 90 yanayotoka Uganda na Kyerwa hutumia barabara hiyo iliyosahaulika?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Barabara ya kutoka Mbeya hadi Mkiwa inaunganisha Mikoa mitatu ya Mbeya, Tabora na Singida na iliamuliwa kujengwa miaka 10 iliyopita. Sasa kipande cha kutoka Chunya hadi Itigi kitakamilika lini?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayoingelea Mheshimiwa Mbunge imepangwa katika bajeti ya mwaka huu utakaoanza Julai. Kwa kweli nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wameipitisha bajeti. Hivyo, ni wajibu wetu kuhakikisha bajeti hiyo tunaisimamia ili itekelezwe kama ilivyopangwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kusema ni lini barabara hii itakamilika, namwomba sana Mheshimiwa Mbunge atupe subira kwa sababu hivi vitu ni vya kitaalam, vinatakiwa vifuatane na mikataba ilivyo. Namhakikishia kwamba barabara hii itakamilika – hilo ndilo la msingi. Lini hasa; nadhani tusiende sana kwa undani kiasi hicho ili baadaye tukaja kushikana uongo hapa.

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Barabara ya Murushaka ni kiungo muhimu kwa Karagwe na Kyerwa na ni barabara muhimu sana kiuchumi, lakini barabara hiyo ni mbovu sana wala haipitiki kabisa:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kutengeneza barabara hiyo ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wa Kyerwa? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kwa lami barabara hiyo kwa sababu zaidi ya magari asilimia 90 yanayotoka Uganda na Kyerwa hutumia barabara hiyo iliyosahaulika?

Supplementary Question 4

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa suala la ujenzi wa barabara linaenda sambamba na uwekwaji wa alama za barabarani na kwa kuwa tayari Serikali imeshaanza kuweka alama hizi za barabarani kwa ajili ya watu wenye ulemavu kwa baadhi ya mikoa, kwa mfano Tanga, je, nini mpango wa Serikali kwa mikoa mingine?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba alama zote tunazoweka barabarani zinazingatia mahitaji maalum ya walemavu. Naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge na najua ameshakutana na Waziri wangu pamoja na wawakilishi wa walemavu ambao walikuja hapa Dodoma na wamelizungumzia hili suala kwa undani.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru kwa juhudi anazozifanya za kufuatilia mahitaji ya walemavu. Nina hakika kwa namna ambavyo ameanza tutafika mahali kila barabara ambayo walemavu wanaihitaji, tutaiwekea hayo mahitaji maalum kadri uwezo wa fedha utakavyokuwa unapatikana.