Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE (K.n.y MHE SELEMANI J. ZEDI) aliuliza:- Ujenzi wa vyumba vya upasuaji katika vituo vya afya vya Bukene na Itobo umekamilika na kwamba vifaa vyote kwa ajili ya kutoa huduma ya upasuaji vimeshafunguliwa ikiwa ni pamoja na vifaa vya kuhifadhia damu na mashine za kufulia. Je, ni jambo gani linazuia huduma za upasuaji kuanza katika vituo hivyo?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ningeomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri maswali mawili madogo ya nyongeza.
Kwa kuwa tatizo la Itobo linafanana kabisa na tatizo la Kata ya Lusu kuwepo kwa kituo cha afya ambacho kilijengwa na ADB chenye vifaa na vitendea kazi vya namna hiyo. Je, Serikali haioni wakati umewadia wa kuhakikisha wanapeleka Wataalam na katika kituo cha afya cha Lusu ili kuweza kutatua tatizo linalowakabili wananchi wa Lusu kwa sababu wanatembea zaidi ya kilometa 20?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kituo cha afya cha Zogolo kilichopo katika Kata ya Nzega ndogo ambacho majengo yake yamekamilika na baadhi ya majengo kwa ajili ya wodi kwa akinamama na theatre yanahitaji kumaliziwa na kituo cha afya kilichopo Kata ya Mbogwe ambacho hutumika kwa ajili ya kuhudumia Kata zaidi ya saba, je, Serikali haioni wakati umewadia wa kutenga fedha kwenda kusaidia nguvu za wananchi katika vituo hivi vya afya vya hizi Kata mbili cha Zogolo na Mbogwe ili wananchi wa maeneo hayo waache kusafiri masafa marefu kwenda kufuata huduma katika hospitali ya Wilaya ya Nzega?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna vituo hivi vilivyojengwa na ADB, kuna kule Itobo, Bukene na kituo cha Lusu. Si hivyo tu hata nilivyofika Masasi nilikuta kuna vituo vimejengwa. Changamoto kubwa ya vituo hivi ni kwamba vina vifaa vizuri sana, tatizo lake ni katika suala zima la wataalam.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumejielekeza, pamoja na Waziri wa Afya, kuona ni jinsi gani tutafanya katika ajira itakayokuja katika maeneo haya ambayo yana upungufu hasa wa Wataalam wale wa upasuaji na dawa za usingizi ili tukiwapata wataalam hawa tuweze kuwapeleka kwenye vituo hivyo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Hussein Bashe kwamba, Mkoa wa Tabora ni miongoni mwa mikoa ambayo tumeiwekea kipaumbele na hasa kutokana na vituo hivi kuwa na vifaa vyenye thamani kubwa sana, tusipovitumia kwa sasa vinaweza vikaharibika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, jambo hili katika mchakato huu unaokuja sasa hivi maeneo yale yote na maeneo mengine ambayo nimetembelea ambapo vituo vile vimejengwa, vitapewa kipaumbele katika upatikanaji wa Wataalam wanaokidhi kwa matumizi ya vile vifaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mchakato utakaokuja maeneo yale yote na maeneo mengine ambayo nimetembelea ambako vituo vimejengwa vitapewa kupaumbele katika upatikanaji wa wataalam wanaokidhi matumizi ya vifaa vile.
Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya suala la kituo cha Zogolo pamoja na Mbogwe, nimesema awali, katika bajeti ya mwaka huu watu walikuwa na malalamiko kwa kusema kwamba hawaoni jinsi gani Wizara ya TAMISEMI imekwenda kuhakikisha kwamba ukarabati umefanyika. Tulisema kwamba kupanga bajeti hizi za kumalizia inaanzia katika ngazi za Halmashauri. Ndiyo maana nimesema pale awali kwamba wiki iliyopita, Wizara ya Afya na TAMISEMI na Kamati ya Bajeti imekaa pamoja kubaini upungufu kama huo. Lengo letu kubwa ni kuja na mpango mkakati mpana zaidi ili kuhakikisha vituo hivi ambavyo vina suasua tutaweza kuvikamilisha wananchi wapate huduma bora.

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE (K.n.y MHE SELEMANI J. ZEDI) aliuliza:- Ujenzi wa vyumba vya upasuaji katika vituo vya afya vya Bukene na Itobo umekamilika na kwamba vifaa vyote kwa ajili ya kutoa huduma ya upasuaji vimeshafunguliwa ikiwa ni pamoja na vifaa vya kuhifadhia damu na mashine za kufulia. Je, ni jambo gani linazuia huduma za upasuaji kuanza katika vituo hivyo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri yanakubaliana na ukweli kwamba viko vituo vingi vya afya vyenye vyumba vya upasuaji nchini lakini havifanyi kazi kwa sababu mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, Benjamin Mkapa Foundation wamejenga vituo vingi karibu 20 Mkoa wa Rukwa vyenye vyumba vya upasuaji na havifanyi kazi kwa sababu ya kukosa wataalam. Huko Buchosa kuna kituo cha Mwangika, planning international wamejenga hakina Wataalam wa usingizi. Sasa nimwombe tu Waziri, kwamba labda wanaweza kuchukua takwimu kutoka Halmashauri zote ili kabla ya Bunge hili kuahirishwa tujue ni vituo vingapi ambavyo vina theatres na bado hazifanyi kazi kwa sababu ya upungufu wa Wataalam hawa wa usingizi.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba ushauri wa Tizeba japokuwa tumeshakuwa na current data lakini tutazifanyia kazi bila shaka.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE (K.n.y MHE SELEMANI J. ZEDI) aliuliza:- Ujenzi wa vyumba vya upasuaji katika vituo vya afya vya Bukene na Itobo umekamilika na kwamba vifaa vyote kwa ajili ya kutoa huduma ya upasuaji vimeshafunguliwa ikiwa ni pamoja na vifaa vya kuhifadhia damu na mashine za kufulia. Je, ni jambo gani linazuia huduma za upasuaji kuanza katika vituo hivyo?

Supplementary Question 3

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza linalofanana kabisa na swali la msingi la Mheshimiwa Zedi. Hakuna jambo linalosikitisha kama pale ambapo majengo ya Serikali ambayo yameanza kujengwa halafu yanaachwa nondo zinaoza na kusababisha hasara kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, Serikali inasema nini kuhusu jengo la upasuaji lililoanza kujengwa katika Wilaya ya Urambo ambayo mpaka sasa haijakamilika wakati huo jengo la upasuaji katika kituo cha Usoke halijakamilika, jengo la kliniki ya akinamama wajawazito katika Kata ya Usisya na Isongwa yote nondo zinaoza. Serikali inasema nini kuhusu uharibifu huu unaoendelea wakati wananchi wanahitaji huduma katika Wilaya ya Urambo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema hapa mwanzo, nikasema kwanza kuhusu majengo ambayo hayajakamilika wakati mwingine tunakuwa na makosa wakati wa budgeting. Wakati mwingine tunapanga bajeti, jengo halijakamilika na mwaka mwingine tunatenga bajeti bila kuangalia mradi uliopita. Kwa hiyo, kwanza katika vikao vyetu vya awali vya Halmashauri ni jambo la msingi kubainisha miradi ambayo haijakamilika na kuitengea fedha katika bajeti, kwa sababu bajeti hiyo ikishathibitishwa ndipo majengo hayo huweza kumalizika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana nampongeza Mheshimiwa Mama Sitta kwa sababu ana-concern kubwa kwa akinamama. Ndiyo maana nimesema kwamba kwa kuona umuhimu wa jambo hilo tumeelekeza Halmashauri zote na barua tumeshaiandika imeenda katika Halmashauri zote; kwamba kila Halmashauri ilete mchanganuo wa majengo ambayo hayajakamilika ili tuweze kupanga kwa pamoja. Jambo hili lilifanywa na Kamati ya Bajeti ya Bunge kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais, TAMISEMI wiki iliyopita.
Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu letu kubwa ni kupata mpango mkakati wa namna ya kufanya ili kuondoa haya maboma ambayo tangu mwaka 2007 – 2010 yalianzishwa na hadi sasa hayajakamilika. Kwa hiyo, Mheshimiwa Sitta nikuhakikishie kwamba mpango wetu uliokuwepo ni mpango wa pamoja baina ya Bunge na Wizara za Serikali kuhakikisha kwamba huduma za afya, ukamilishaji wa majengo unakamilika ili wananchi waweze kupata huduma bora.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE (K.n.y MHE SELEMANI J. ZEDI) aliuliza:- Ujenzi wa vyumba vya upasuaji katika vituo vya afya vya Bukene na Itobo umekamilika na kwamba vifaa vyote kwa ajili ya kutoa huduma ya upasuaji vimeshafunguliwa ikiwa ni pamoja na vifaa vya kuhifadhia damu na mashine za kufulia. Je, ni jambo gani linazuia huduma za upasuaji kuanza katika vituo hivyo?

Supplementary Question 4

MHE: STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa matatizo ya vyumba vya upasuaji yako pia kwenye Wilaya ya Nyamagana hasa, kwenye Hospitali yetu ya Sekou Toure ambayo Miundombinu yake ya theatre iliyopo sasa iko mbali kutoka kwenye Jengo ambalo ni labour ward. Pale kwenye jengo la labour ward tayari kuna jengo ambalo lilishaandaliwa lakini halina vifaa kabisa. Ni lini Serikali itakuwa tayari kupeleka vifaa vya upasuaji kwenye jengo hilo ambalo liko karibu sana na chumba wanachojifungulia akinamama, tukiamini kupatikana kwa vifaa hivi kutasaidia kuokoa maisha ya mama na mtoto yanajitokeza hasa wakati wa kujifungua?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, huyu Mbunge anayeuliza hivi kwanza tuelewe kwamba yeye ni Msukuma, kwa hiyo lugha yake lazima tuielewe vizuri. Najua kwamba Mbunge huyu yuko makini katika Jimbo la Nyamagana kwa sababu kazi aliyoifanya akiwa kama Mwenyekiti, Meya wa Jiji lile tunaitambua wazi. Kwa hiyo, nimthibitishie, hata maamuzi waliyofanya kufuma mifumo ya electronic mpaka sasa hivi wanakusanya kutoka 150,000 mpaka milioni tatu kwa siku, ni mchakato mkubwa sana ambao Mbunge huyu ameufanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kama Serikali tunasema kwamba, kwanza mimi mwenyewe nilimwambia nilipoongea naye hapo awali kwamba nitakwenda Mwanza, tutatembelea Sekou Toure, tutapanga kwa pamoja jinsi gani tutafanya ili vifaa tiba vipatikane. Vitapatikana wapi, tutajua katika mpango wa pamoja tutakapokaa pamoja, lakini nitakwenda kule Mwanza kubainisha kwanza mapato yao ya ndani wanayoyapata, lakini pia kuangalia fursa zipi nyingine tutakazozitumia ili wananchi wa Mwanza waweze kupata huduma bora.