Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 imelenga kuanzisha Mfuko Mkubwa kwa ajili ya kutoa mkopo kwa wafanyakazi na wajasiriamali wadogo kwa masharti nafuu. Je, Serikali imefikia hatua gani katika utekelezaji wa jambo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba awe specific kama Serikali ina mkakati wowote kuhakikisha inaijengea SIDO uwezo ili iweze kutoa mafunzo ya biashara pamoja na masoko kwa wafanyabiashara wadogo wadogo ama wajasiriamali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, kwa kuwa wajasiriamali wadogo wadogo waliokuwa wengi, mitaji kwao ni tatizo na kwa kuwa nchi za wenzetu huko nje zina kawaida ya kutoa kipindi fulani kwa wajasiriamali wadogo wadogo ili kuwasamehe kodi waweze kuwa na nguvu ya kimtaji na waendelee zoezi la kulipa kodi. Napenda kujua kama Serikali yetu ya Tanzania ina mkakati wowote wa kutoa grace period kwa hao wajasiriamali wadogo wadogo. Ahsante.

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, SIDO pamoja na kutoa mafunzo kwa wajasiriamali, inao Mfuko Maalum unaohusisha kutoa pesa. Hata hivyo, SIDO kwa kushirikiana na TBS wanakwenda mbali kwa kuwaongoza wajasiriamali namna ya kutengeneza bidhaa zao ziweze kufaa kwenda sokoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ndiyo swali ambalo Waziri wa Fedha ametujibu hivi punde. Si kivutio, si uwezeshaji, ni msamaha wa kodi tu. Mazingira bora ya biashara ni kivutio kikubwa kuliko ile kumpa pesa. Kwa hiyo, Serikali itahakikisha mazingira bora ya biashara yanapatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeanzisha incubators na Serikali ya India inakuja kutusaidia kuwawezesha wajasiriamali wadogo waweze kumudu shughuli, waweze kufanya packaging, waweze kwenda kwenye masoko na tutaanzisha mitaa huko vijijini, small industries street kusudi muweze kufanya kazi kule badala ya kudondosha pesa au kuwapa msamaha ya kodi. Misamaha ya kodi mwenye pesa ameshasema kwamba haitakuwepo ila tutaboresha mazingira.

Name

Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 imelenga kuanzisha Mfuko Mkubwa kwa ajili ya kutoa mkopo kwa wafanyakazi na wajasiriamali wadogo kwa masharti nafuu. Je, Serikali imefikia hatua gani katika utekelezaji wa jambo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kikwazo kikubwa sana cha biashara kuendelea katika Taifa letu ni riba kubwa inayotolewa na mabenki ya biashara ambayo sababu yake ni kiwango kilichowekwa na Benki Kuu ya Tanzania.
Je, Serikali ina mpango gani dhidi ya kusaidia wafanyabiashara dhidi ya riba kuwa inayotolewa na mabenki, kikwazo hicho ambacho BOT ndiyo imekuwa msingi mkubwa ili kuwezesha watu wengi kufanya biashara zenye sura ya miradi na siyo biashara za uchuuzi?

Name

Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Benki Kuu itaendelea kusimamia sekta ya fedha ili kuhakikisha kwamba riba zinapungua na ndiyo maana katika mapendekezo ya Mpango tulioleta, moja ya hatua ambazo Serikali inachukua ni kuhakikisha kwamba, taasisi za umma sasa zinafungua akaunti Benki Kuu ili tuhakikishe kwamba fedha nyingi ambazo zilikuwa zinatumika na mabenki kwa ajili ya kufanya bashara, fedha za Serikali bila Serikali yenyewe kupata faida, sasa zinaweza zikatumika ili hayo mabenki sasa yaende huko kwa kupeleka huduma kwa wananchi vijijini. Hii ni hatua mojawapo ya kusaidia kupunguza riba ili wananchi wetu waweze kunufaika zaidi.