Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RISALA S. KABONGO aliuliza:- Hifadhi za Mikoa ya Kusini za Mikoa ya Kusini za Ruaha, Kitulo, Udzungwa, Mikumi na Katavi na maeneo mengine ya kihistoria husifika sana kwa vivutio vyake, lakini kutembelewa na idadi ndogo sana ya watalii na hivyo kuwa na mapato madogo na kuwa tegemezi kwa Hifadhi za Mikoa ya Kaskazini:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa muda mfupi na mrefu wa kuongeza idadi ya wageni katika hifadhi hizo? (b) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuboresha miundombinu ya barabara, malazi na viwanja vya ndege katika hifadhi hizo kwa matumizi ya watalii? (c) Je, kwa nini Serikali isishirikiane na wawekezaji binafsi ili kuwekeza katika maeneo ya utalii kwenye Hifadhi hizo za Mikoa ya kusini?

Supplementary Question 1

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini vilevile nilikuwa na maswali ya nyongeza.
Kwa kuwa Serikali kupitia mradi wa UNDP na USAID umepata Dola za Kimarekani 100,000 kwa ajili ya kufanya ukarabati mbalimbali kwa maeneo ya utalii; inaonekana kwamba Serikali imejipanga kukarabati uwanja wa Songwe, Katavi, Kigoma na Mpanda:-
Je, kwa kuwa mwaka 2009 Iringa iliteuliwa kuwa kitovu cha utalii, Serikali imejipangaje kuwekeza uwanja wa Nduli - Iringa ambao umekuwa na gharama kubwa sana za usafiri kuanzia Dola 180 mpaka Dola 200 kwa safari sawa na shilingi 400,000/= kutoka Iringa mpaka Dar es Salaam, Serikali imejipangaje kuwekeza katika uwanja huu? (Makofi)
Swali la pili; kwa kuwa Serikali imejipanga kuwekeza kwenye mahoteli, Serikali imejipangaje kutathmini viwango vya mahoteli ambavyo viko katika nchi hii, ukizingatia kwamba zoezi hili limefanyika baada ya uhuru; Mikoa ya Pwani, Dar es Salaam na Mikoa ya Manyara kwa kuweka madaraja ya nyota katika mahoteli? Ni eneo ambalo tunapoteza mapato sana na mahoteli mengi yanalipa kodi kutokulingana na nyota. Kwa mfano, hoteli ya nyota moja, nyota mbili, nyota tatu.
MHE. RISALA S. KABONGO: Je, Serikali imewekezaje katika upande huo?
Sambamba na hilo, Serikali imejipangaje kuboresha barabara ya kuelekea hifadhi ya Ruaha yenye kilomita 130 ambayo ina hali mbaya sana na kusababisha gharama za utalii kuwa kubwa katika Mikoa hii ya Nyanda za Juu Kusini hususan Hifadhi ya Ruaha ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kuhusu namna ambavyo Serikali imejipanga kuweza kuboresha uwanja wa ndege wa Iringa kwa sababu ambazo nilizisoma na ambazo na yeye amezirudia.
Kwanza, ni nia ya Serikali kuendelea kufanya utalii kuwa chanzo kikubwa cha mapato kwa Taifa hili. Kwa sababu hiyo, ili tuweze kufikia lengo hilo, lolote linaloweza kufanya Serikali ikafanya vizuri zaidi kwenye Sekta ya Utalii ni kipaumbele katika Wizara ya Maliasili na Utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, basi nilipotaja viwanja vya ndege na barabara na miundombinu mingine inayoboreshwa chini ya mradi huu ambao una ufadhili wa Dola milioni 100, huu ni mradi mmoja tu peke yake na jibu lililotolewa lilikusudia kujibu swali lililotolewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kusema tu kwa ujumla, Serikali inajipanga zaidi kutafuta miradi mingine zaidi na kutafuta fedha zaidi ili kuweza kuboresha maeneo yote ambayo yatachangia katika kuboresha Sekta ya Utalii kwa ujumla. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kutathmini viwango vya mahoteli, ameuliza swali ambalo sasa hivi liko mezani tayari na ninamshukuru Mbunge kwa mawazo haya mazuri ambayo yanaendana na jitihada za Serikali ambazo tayari zimekwishaanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatutafanya tu zoezi la kupanga hoteli kwenye madaraja, bali pia ni nia ya Serikali kuhakikisha kwamba tunatoa elimu na kusimamia wawekezaji wa Kitanzania waweze kufikia viwango hivyo. Hoteli nyingi za sasa hivi zilizopo, hata kabla hujaenda kuzipa madaraja, nyingi zinahitaji kufanyiwa kazi ili ziweze ziboreshe huduma ili kuweza kuwafanya watalii waweze kujisikia kwamba wamekaa kwenye hoteli.
Kwa hiyo, kwanza tutaanza kutoa elimu na hapa nitoe wito, wote wanaokusudia kuwekeza kwenye eneo hili, waweze kuwasiliana na Idara ya Utalii kwenye Wizara hii, pale ambapo watahitaji; au wanaweza kupata utaalam kutoka mahali pengine, lakini wote tuwe na nia ya kuweza kuboresha huduma za hoteli ili wageni wanapokuja waweze kujisikia kwamba wako mahali penye sifa zinazotakiwa na viwango.
Kwa hiyo, tunakusudia kuanza hivi karibu kupanga hoteli zote katika madaraja katika Mikoa yote, siyo tu kwa ajili ya kuboresha mapato ya Serikali lakini pia katika kuwafanya watalii waweze kupata huduma zinazostahili.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. RISALA S. KABONGO aliuliza:- Hifadhi za Mikoa ya Kusini za Mikoa ya Kusini za Ruaha, Kitulo, Udzungwa, Mikumi na Katavi na maeneo mengine ya kihistoria husifika sana kwa vivutio vyake, lakini kutembelewa na idadi ndogo sana ya watalii na hivyo kuwa na mapato madogo na kuwa tegemezi kwa Hifadhi za Mikoa ya Kaskazini:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa muda mfupi na mrefu wa kuongeza idadi ya wageni katika hifadhi hizo? (b) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuboresha miundombinu ya barabara, malazi na viwanja vya ndege katika hifadhi hizo kwa matumizi ya watalii? (c) Je, kwa nini Serikali isishirikiane na wawekezaji binafsi ili kuwekeza katika maeneo ya utalii kwenye Hifadhi hizo za Mikoa ya kusini?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, utalii ili uweze kuendelea vizuri na uweze kuboresha Pato la Taifa ni pamoja na ushirikishwaji wa wananchi wanaoishi kando kando ya Hifadhi hizi za Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nina mgogoro sasa hivi wa wafugaji zaidi ya ng‟ombe 5000 kwa vijiji vya Kijereshi na Nyamikoma katika Jimbo la Busega ambao wamekamatwa kwa sababu ya askari wa Game Reserves kuwasukumizia kwenye hifadhi ili waweze kutoza fedha hawa wafugaji. Hii mifugo ina zaidi ya siku tatu imefungiwa kwenye pori. Hivi kweli kama tunataka ushirikishaji mzuri na uhifadhi wa maliasili zetu.
Je, Serikali inachukua hatua gani sasa kuruhusu hiyo mifugo, kwa sababu ng‟ombe hawana tatizo, ili waweze kuachiwa…

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwamba ninaomba tamko la Waziri wa Maliasili kuhusiana na mifugo hii ambayo imeingizwa kwenye hifadhi kinyume cha utaratibu na kwa nini imeendelea kufungiwa kule isiachiwe? (Makofi)

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa…

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Nakushukuru kwa kunipa nafasi kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Chegeni, Mbunge wa Busega, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, wanavijiji wanaopakana na Mbuga ya Serengeti katika eneo la Busega na vijiji hivyo ambavyo Mheshimiwa Mbunge amevitaja, wameingiza ng‟ombe zaidi ya 6000 katika eneo lao na ng‟ombe hao wamekamatwa na Askari. Jana usiku nimetoa maagizo kwamba ng‟ombe hao waachiwe na wanavijiji wachukue ng‟ombe zao bila kuchelewa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kusisitiza kwa wafanyakazi wa mbuga ya Serengeti kuwaachia ng‟ombe hao mara moja. (Makofi)

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RISALA S. KABONGO aliuliza:- Hifadhi za Mikoa ya Kusini za Mikoa ya Kusini za Ruaha, Kitulo, Udzungwa, Mikumi na Katavi na maeneo mengine ya kihistoria husifika sana kwa vivutio vyake, lakini kutembelewa na idadi ndogo sana ya watalii na hivyo kuwa na mapato madogo na kuwa tegemezi kwa Hifadhi za Mikoa ya Kaskazini:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa muda mfupi na mrefu wa kuongeza idadi ya wageni katika hifadhi hizo? (b) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuboresha miundombinu ya barabara, malazi na viwanja vya ndege katika hifadhi hizo kwa matumizi ya watalii? (c) Je, kwa nini Serikali isishirikiane na wawekezaji binafsi ili kuwekeza katika maeneo ya utalii kwenye Hifadhi hizo za Mikoa ya kusini?

Supplementary Question 3

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa vile swali la Mheshimiwa Kabongo limefanana na matatizo yaliyoko katika Mbuga za Wanyama za Mkomazi; na kwa vile nilishaongea na Waziri wetu wa Utalii, kaka yangu Mheshimiwa Profesa Maghembe kwamba tembo wanatoka Mkomazi National Park wanaingia kwenye Loresho tulilowatengenezea wafugaji na inaharibu sana sehemu hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa TANAPA tuliwaeleza tatizo hili na kwamba watusaidie kuboresha intake ili maji yawe mengi wakati wanatafuta jinsi ya kuwapelekea tembo wale maji. Je, Waziri anaweza kunisaidia kueleza atachukua hatua gani ya dharura kuhakikisha kwamba yale maloresho na tenki letu la intake lililoharibiwa na tembo na wanyama wengine linaboreshwa ili wafugaji waendelee kupata maji wakati wanatafuta jinsi ya kusaidia wanyama hawa? Ahsante.

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, tutachukua hatua mbili. Kwanza ni kuhakikisha kwamba tunaongeza upatikanaji wa maji katika eneo ambalo hao tembo wanatoka kule kwenye National Park na pia tutafanya ukarabati wa maeneo ambayo yameharibiwa katika vijiji ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameyataja. (Makofi)