Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:- Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya M. Kikwete aliahidi kujenga barabara za Mji wa Maswa zenye urefu wa kilometa tatu ndani ya Halmashauri ya Mji Mdogo wa Maswa. Je, ni lini barabara hizo zitaanzwa kujengwa?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza napenda kujua usanifu huu wa kina umeanza lini na utaisha lini?
Swali la pili ningependa kujua kwa sababu nimefuatilia kwa muda mrefu ahadi hii ya Mheshimiwa Rais kumekuwa na mkanganyiko wa kutokujua, kwamba fedha za ujenzi wa barabara hizi kilometa tatu zitatoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa au zitatoka katika Serikali Kuu? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema katika jibu langu la msingi kwamba bajeti ya fedha hii imetengwa katika mwaka huu wa fedha 2016/2017 ambayo bajeti tumepitisha si muda mrefu sana katika Ofisi ya Rais TAMISEMI. Lengo kubwa ni kwamba fedha zile sasa zitatoka ilimradi detailed design iweze kukamilika, mara baada ya hapo sasa tutajua gharama halisi ya ujenzi wa barabara hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namuomba Mheshimiwa Stanslaus avutea subira tu na kwa sababu unajua kwamba ofisi yetu, imejielekeza sasa imejipanga jinsi gani tutafanya kutatua tatizo la miundombinu katika Halmashauri mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, jambo la kwamba hizi fedha zitatoka wapi aidha Halmashauri au zitatoka wapi hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais ambaye ni mstaafu regardless hizo fedha kama zitatoka Halmashauri lakini lengo kubwa ni kwamba kazi hii lazima itekelezwe. Na ndio maana hata kama ukifanya rejea bajeti yetu ya mwaka huu tumetenga takribani bilioni 245 na bilioni hizi maana yake kulikuwa na mgawanyiko wa maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna takribani shilingi bilioni 43 kwa ajili ya miradi ile ya kuondoa vikwazo maeneo mbalimbali zingine ni kwa ajili katika Halmashauri mbalimbali. Lakini ukifanya rejea sana katika hiki kipindi cha miaka mitano, kupitia mradi wetu wa uboreshaji wa miji mbalimbali, unaona Miji mingi sasa hivi imebadiika, lakini tunaenda hivyo maana yake tunaenda katika hatua sasa za Halmashauri. Lengo langu na jukumu letu kubwa ni nini kama Serikali, tutahakikisha miradi hii ambayo ni kipaumbele ambayo imetolewa ahadi na viongozi wetu wakuu wa nchi tutahakikisha kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI inasimamia na miradi hii iweze kutekelezeka. Kwa sababu lazima tulinde imani ya viongozi wetu wameifanya na jambo hili tumejipambanua wazi kwamba ahadi zote zilizopangwa lazima tuzitekeleze kwa kadri tulivyowaahidi.

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:- Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya M. Kikwete aliahidi kujenga barabara za Mji wa Maswa zenye urefu wa kilometa tatu ndani ya Halmashauri ya Mji Mdogo wa Maswa. Je, ni lini barabara hizo zitaanzwa kujengwa?

Supplementary Question 2

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Tatizo la Maswa Mashariki linalingana kabisa na tatizo la Mji wa Mombo, katika Halmashauri ya Korogwe Vijijini. Rais wa Awamu ya Nne aliaahidi kwamba atajenga kiwango cha lami barabara kilometa 1.5 na Rais wa Awamu ya Tano alivyokuja vilevile alitoa ahadi hiyo kwamba atatekeleza ahadi ya ambayo imeachwa na Rais Mstaafu. Lakini mpaka leo hii hakujafanyika kitu cha aina yoyote, je, Serikali inasemaje kuhusiana na Mji wa Mombo ambao wananchi wake wanategemea sana mpaka sasa hivi kungekuwa na barabara ya lami lakini hakuna kinachoendelea

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ahadi hii ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais lakini tunaona kulikuwa na faraja kubwa sana, wakati Rais Mstaafu anatoa ahadi hiyo Waziri wake wa Ujenzi ni Dkt. John Pombe Magufuli. Then katika uchaguzi wa mwaka huu sasa yule aliyekuwa ni Waziri wa Ujenzi sasa hivi ndio Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama tukisema ndugu zetu wa Korogwe Vijijini ni watu ambao mmelamba dume katika mchezo wa karata. Naomba nikuambie hii ahadi ya Rais itakuwepo pale pale na ndio maana ukiangalia katika harakati hizo juzi juzi nilipita Korogwe kwa mama yangu, jinsi ujenzi wa kituo kikubwa cha mabasi kinavyofanyika. Maana yake ni kazi kubwa inafanyika na siyo kituo cha mabasi maana yake ni suala zima la ujenzi wa miundombinu ya barabara ya lami. Maana yake mambo haya yote katika Mkoa wa Tanga kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais kwa kweli yatatekelezwa tufanye subira tu.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:- Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya M. Kikwete aliahidi kujenga barabara za Mji wa Maswa zenye urefu wa kilometa tatu ndani ya Halmashauri ya Mji Mdogo wa Maswa. Je, ni lini barabara hizo zitaanzwa kujengwa?

Supplementary Question 3

MHE ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyo kwenye Mji mdogo wa Maswa tuna tatizo kama hilo kwa Mji wetu Mdogo wa Mbalizi, ambapo Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kumalizia kipande kidogo cha barabara ya kilometa moja na pia aliahidi kumalizia ujenzi wa stand pale Mbalizi lakini mpaka leo hakuna chochote kinachofanyika labda ningepena Waziri ajaribu kutoa ufafanuzi ni lini ujenzi huo utaanza? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI YA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Ujenzi kwanza naomba tukiri wazi kwamba bajeti katika kipindi ambacho Dkt. John Pombe Magufuli anaahidi bajeti yake ndio kwanza hii tunaanza bajeti ya kwanza na baadaye tuna miaka mitano. Lakini ameahidi stand na amewaahidi barabara ya kilomita moja. Mheshimiwa Mbunge, naomba nikwambie kwamba, ahadi ya Rais itakuwepo palepale na kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu kazi hii na sisi tuliopewa dhamana ya kuisimamia, tutaisimamia kwa karibu zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutaisimamia kwa karibu zaidi, lengo ni kwamba, ahadi ya Rais aliyoitoa, ujenzi wa stand, ujenzi wa barabara ya kilometa moja itafanyika na muweze kuona kwamba, maeneo mbalimbali sasa hivi stand zinajengwa kupitia miradi yetu sio stand tu, kuna ma-dampo, kuna barabara. Kwa hiyo, nikwambie Mheshimiwa Mbunge ni kwamba, katika maeneo ya Mbalizi ni kwamba, watu wawe na subira hii ndio bajeti yetu ya kwanza imeanza. Imani yangu ni kwamba, maeneo ya Mbalizi, kama Mheshimiwa Rais alivyoahidi, suala lile litatekelezwa.

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:- Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya M. Kikwete aliahidi kujenga barabara za Mji wa Maswa zenye urefu wa kilometa tatu ndani ya Halmashauri ya Mji Mdogo wa Maswa. Je, ni lini barabara hizo zitaanzwa kujengwa?

Supplementary Question 4

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.
Nataka kuuliza swali la nyongeza. Katika ziara ya Mheshimiwa Rais, alipita katika Kijiji cha Budarabujiga aliyeko madarakani Mabasabi na Ikindilo, aliahidi kivuko pamoja na barabara hiyo, ni lini itatekelezwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi ya kivuko, ahadi kama ya barabara, ahadi zote kama nilivyosema awali na ninajua na nyie watani zangu huko Wasukuma mambo mengi sana mmeahidiwa huko hasa katika suala zima la maboti na maeneo mbalimbali.
Mimi imani yangu kubwa ni kwamba, Dkt. John Pombe Magufuli ndani ya miaka hii mitano atafanya mambo ya mfano sana ambayo hatujawahi kuyaona. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, na haya yanajielekeza jinsi gani amejipanga Serikali yake katika ukusanyaji wa mapato, kwa mara ya kwanza mnaona rekodi kubwa katika ukusanyaji wa mapato kutoka kukusanya kwanza bilioni 600 mpaka bilioni 800, sasa tunaanza kukusanya one point something trillion, sio jambo la mchezo! Na mnaona jinsi gani pesa wakandarasi waliokuwa wamesimamisha miradi yao sasa wakandarasi wako site wanaanza kufanya kazi kwa ajili ya umakini wa ukusanyaji wa kodi.
Kwa hiyo, naomba niwaambie, mkakati huu unaoenda wa kukusanya fedha katika Serikali maana yake utaenda sambamba na kuhakikisha zile ahadi zote na miundombinu iliyokusudiwa inaweza kutekelezwa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.