Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. ANTONY C. KOMU (K.n.y. MHE. RAPHAEL J. MICHAEL) aliuliza:- Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ilianza mchakato wa kuifanya Jiji tangu mwaka 2012 baada ya kupata baraka za Rais Mstaafu, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kilimanjaro (RCC) na Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Moshi (DCC) na sasa mchakato huo umekamilika katika hatua zote za kikanuni. Je, ni lini Serikali itatangaza Manispaa ya Moshi kuwa Jiji?

Supplementary Question 1

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba yake kwa sababu hayupo, yupo safari.
Pamoja na majibu ya Naibu Waziri; jambo hili limechukua muda mrefu na kama nchi ilivyokwishaamua kwamba inakwenda kwenye mpango wa viwanda na uchumi wa kati, jambo hili ni muhimu sana. Sasa nataka kujua:-
(i) Ni lini sasa huo mchakato utakamilika ili jambo hili liweze kuanza?
(ii) Napenda kujua vilevile kutoka kwenye Serikali, ni mambo gani hayo hasa ambayo yamepelekea huo mchakato kurejeshwa tena kwenye kufanyiwa marekebisho na vitu kama hivyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kama nilivyosema kwamba tukifanya rejea Bunge lililopita, nilisema kuna timu ya TAMISEMI itapita maeneo mbalimbali; na lengo kubwa ni kubaini kwamba yale maombi yaliyoletwa kutoka katika Ofisi za Mikoa baada ya vikao vya RCC kukaa, kwamba maombi yale sasa wataalam wakienda kufanya tathmini wataona jambo lipi limekamilika na jambo lipi halijakamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri naomba nikujulishe kwamba ofisi yetu imeshatuma timu katika maeneo hayo yote na kazi hiyo wameshamaliza. Hivi sasa wana-compile ripoti yao baadaye kuweza kutushauri vizuri jinsi gani ya kufanya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Komu vuta subira jambo hili litaenda vizuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la pili kwamba mambo gani mwanzo yalikuwa hayajakamilika; ni kwamba ukiangalia Mji wa Moshi, square kilometer karibu 58 peke yake, yaani ni eneo dogo sana kuwa Jiji. Ndiyo maana walidhani kama ingewezekana ni kuongeza eneo lile la utawala na ndiyo maana nadhani wameona maeneo waliyokubaliana katika muhtasari wa mwisho, eneo limeongezeka mpaka maeneo ya Hai na maeneo mengine. Ina maana kwamba eneo limevuka kutoka zile square kilometer 58 imeenda mpaka karibu 142.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kulikuwa na mambo mengine hasa yanayohusu master plan. Kwa hiyo, vitu hivi vyote vilileta mrejesho, walipelekewa mrejesho watu wa Moshi kule kwenda kuvifanyia kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu ni kwamba marekebisho yale yameshafanyika, sasa wahakiki wetu walivyoenda kuangalia kule site, watajua ni jinsi gani vile vilivyoelekezwa vimeweza kufikiwa vizuri na baadaye Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana atafanya maamuzi. Naomba tusiwe na hofu, kila kitu kitaenda kwa utaratibu ambao umepangwa katika ofisi.

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. ANTONY C. KOMU (K.n.y. MHE. RAPHAEL J. MICHAEL) aliuliza:- Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ilianza mchakato wa kuifanya Jiji tangu mwaka 2012 baada ya kupata baraka za Rais Mstaafu, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kilimanjaro (RCC) na Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Moshi (DCC) na sasa mchakato huo umekamilika katika hatua zote za kikanuni. Je, ni lini Serikali itatangaza Manispaa ya Moshi kuwa Jiji?

Supplementary Question 2

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Mamlaka ya Mji Mdogo wa Namanyere ni moja ya mamlaka iliyotembelewa na timu ya uhakiki kutoka Serikali za Mitaa na kwa taarifa tulizozipokea ni kwamba mamlaka hiyo ilikuwa imetimiza vigezo vyote na kwamba kulikuwa na dosari ndogo ndogo ambazo kwa kweli wataalam wetu wameshaleta ripoti na kukamilisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua ni lini hasa wananchi wa Namanyere wategemee kupata hicho walichokiomba kuwa Mamlaka ya Mji kamili wa Halmashauri ya Mji?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakumbuka katika Bunge lilipita nilijibu swali la Mheshimiwa Mipata na kaka yangu Mheshimiwa Malocha pale, walipokuwa wanazungumza suala zima la Namanyere na sehemu ya Sumbawanga. Ndiyo maana kati ya tarehe 14 na 15, nilikuwa Rukwa na Katavi na niliweza kufika mpaka Namanyere. Hata hivyo, timu yetu ya wataalam ilifika Namanyere kufanya uhakiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali kwamba zoezi hili sasa litakuwa lipo katika stage ambayo ni muafaka sana, mambo yatakapokamilika.
Naomba Mheshimiwa Mbunge asiwe na hofu, ni kwamba yale maamuzi sahihi yatafikiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sio yeye peke yake, hata akina Profesa Maji Marefu hapa, mpaka Mzee wangu hapa wa Mpwapwa, wote wana masuala hayo hayo. Kwa hiyo, tuondoe hofu, ofisi yetu inafanya kazi, tutapata mrejesho muda siyo mrefu sana. (Makofi)

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. ANTONY C. KOMU (K.n.y. MHE. RAPHAEL J. MICHAEL) aliuliza:- Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ilianza mchakato wa kuifanya Jiji tangu mwaka 2012 baada ya kupata baraka za Rais Mstaafu, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kilimanjaro (RCC) na Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Moshi (DCC) na sasa mchakato huo umekamilika katika hatua zote za kikanuni. Je, ni lini Serikali itatangaza Manispaa ya Moshi kuwa Jiji?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Dodoma ni Makao Makuu ya nchi; na kwa kuwa Manispaa ya Dodoma imekamilisha vigezo vyote vya kupata hadhi ya kuwa Jiji; na kwa kuwa majengo ya Manispaa ya Dodoma yamejengwa kitaalam, yamefuata master plan, hakuna squatters. Ni lini Serikali sasa itatangaza Mji wa Dodoma kuwa Halmashauri ya Jiji? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani Mheshimiwa Lubeleje anafanya rejea ya siku alipokuwa akiniambia suala la Jiji la Dodoma; lakini nadhani ombi lake alivyokuwa anazungumza vile tukiwa barabarani, Mungu amelitilia tunu juu yake kiasi kwamba sasa hivi naona Serikali yote kiukubwa wake yote inahamia Dodoma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili nadhani halina mashaka, ni taratibu tu zitakamilika hapa na kwa sababu michakato mipana inakwenda na Serikali yote inahamia Dodoma, uwanja wa ndege unaimarishwa, basi nadhani vikao sahihi vitakaa na kufanya mapendekezo haya. Ofisi ya Rais - TAMISEMI haitasita kwa sababu nchi kwa ujumla wake sasa, Serikali yote inahamia Dodoma.
Kwa hiyo, ni mambo ya kimchakato tu, Mheshimiwa Lubeleje avute subira na tunavyoendelea kuliimarisha Jiji letu la Dodoma, nadhani itakuwa ni sehemu ya fahari ya Tanzania. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nataka kuongezea kwenye swali lililouliza kwamba je, ni lini Dodoma itatangazwa kuwa Jiji?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tu Dodoma sasa ndiyo tunafanya jitihada za kuhamia kwa sababu tayari imeshaamuliwa kuwa ndiyo Makao Makuu ya nchi yetu, kwa kawaida na kwa utaratibu ni lazima iwe Mamlaka ya Jiji. Kwa hiyo, utaratibu huu utakwenda sambamba na hii jitihada inayofanyika, lakini pia Dodoma ina faida kubwa kwamba walipokuwa wanatenga na kuitengenezea ramani yake, walitenga mipaka mikubwa, ina square kilometer zaidi ya 250,000. Kwa hiyo, ni eneo kubwa sana na linafaa na lina sifa zote kuwa Jiji. (Makofi)