Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufungua na kutangaza maeneo ya uwekezaji Mkoani Kigoma?

Supplementary Question 1

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

(i) Je, ni maeneo yapi ambayo Serikali imeyaainisha katika Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya uwekezaji?

(ii) Je, ni shughuli zipi za kipaumbele zilizoainishwa kutangazwa katika maeneo hayo? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza. Mkoa wa Kigoma ni moja ya Mikoa ya kimkakati hapa nchini, hivyo maeneo ambayo tunaazimia kuyawekea uwekezaji wa kutosha ni kwenye uongezaji thamani katika mazao ya kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, azma hiyo, inadhihirika pale ambapo Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ameendelea kuboresha miundombinu wezeshi ikiwemo barabara za lami lakini pia, kupeleka umeme wa Gridi ya Taifa ili kuona namna gani tunaweza kuongeza thamani ya mazao ya kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari pale Kigoma tumeshaweka kiwanda kikubwa cha kuchakata chikichi lakini pili, kuna kiwanda kikubwa kinaenda kujengwa cha kuchataka sukari.

Mheshimiwa Naibu Spika, shughuli muhimu ambazo zinaweza kufanywa katika Mkoa wa Kigoma, mahsusi Buhigwe ambako Mheshimiwa Mbunge anatoka, na kwa kuwa tunajua wako mpakani na kuna masoko ya DRC na Burundi, kwa hiyo, tunataka tuone mazao ya tangawizi, kahawa, ndizi, parachichi na mazao mengine yanastawishwa na kuwekezwa katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie nafasi hii kuwaomba Halmashauri zote katika Mkoa wa Kigoma kutenga maeneo ya uwekezaji ili kuweza kufanikisha lengo na azma ya Mheshimiwa Rais wetu Mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuuweka Mkoa wa Kigoma kuwa Mkoa wa kimkakati, nakushukuru sana.