Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Kata za Semembela, Isagenhe na Kahama ya Nhalanga hazina kabisa mawasiliano ya simu za mkononi:- Je, ni lini Kata hizi zitapatiwa huduma hii muhimu ya mawasiliano ya simu za mkononi?

Supplementary Question 1

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mwaka jana Bunge lililopita mwezi wa nne niliuliza swali hili hili la kufuatilia ujenzi wa minara hii na jibu nililopewa lilikuwa kwamba, kazi ya ujenzi imeanza na mpaka Waziri wa Mawasiliano wakati ule alinipa barua ya commitment ambayo nilikwenda kuwaonesha wananchi lakini mpaka sasa hivi hakuna chochote ambacho kimefanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, nataka kujua inakuaje makampuni ya simu...
MWENYEKITI: Swali la pili eeh?
MHE. SELEMANI J. ZEDI: Inakuwaje Makampuni ya Simu pamoja na ruzuku wanayopewa kutoka kwenye Mfuko wa Mawasiliano kwa wote yanashindwa kukamilisha ahadi zao?
Swali la pili, Serikali ilituambia kwamba imebaini Makampuni ya Simu yanakuwa reluctant, ni wazito kwenda kujenga minara vijijini kwa sababu ya kifaida kwamba hakuna faida wanapoweka minara vijijini na wakasema kwa kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote watahakikisha kwamba, minara ya vijijini inajengwa kwa ruzuku ya 100%.
Je, mpango huo upo? Unaendelea na kama unaendelea ni vijiji gani ambavyo wameshabaini na vitanufaika kwa mpango huo?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumjibu Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwenye Bunge hili mwaka 2014/2015, tulisemea maeneo hayo na ni kweli kwamba Makampuni mengi ya Simu, Airtel, Tigo, Vodacom, Zantel wanachelewesha kupeleka mawasiliano vijijini. Kwa mantiki hiyo ndiyo tuliamua kuleta Halotel au Viettel kwa ajili ya kupeleka mawasiliano vijijini haraka. Kwa mtazamo huo huo kuanzia mwezi Mei mwaka huu mpaka mwezi Oktoba mwaka huu, Kampuni ya Halotel au Viettel itajenga takribani mawasiliano kwenye vijiji 1800. Tunaamini na vijiji vya Mheshimiwa Mbunge vilevile vitapata huduma hiyo.

Name

Suleiman Ahmed Saddiq

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Kata za Semembela, Isagenhe na Kahama ya Nhalanga hazina kabisa mawasiliano ya simu za mkononi:- Je, ni lini Kata hizi zitapatiwa huduma hii muhimu ya mawasiliano ya simu za mkononi?

Supplementary Question 2

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri; kwa kuwa tatizo la Kahama la mawasiliano ya simu linafanana na tatizo la Mvomero na kwa kuwa tumepeleka maombi kwa kampuni mbalimbali za simu, na kampuni hizo zimeahidi kujenga minara katika Kata ya Luale, Kikeo, Kinda, Pemba na Kibati. Kwa kuwa minara hiyo hadi leo bado haijajengwa, je, Serikali iko tayari kupeleka ruzuku ya Mfuko wa Mawasiliano katika Kata hizo ili wananchi wa Mvomero sasa wapate mawasiliano ya uhakika? (Makofi)

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iko tayari kupeleka ruzuku lakini tatizo kubwa sio ruzuku, tatizo kubwa tunatoa ruzuku, lakini makampuni yenyewe hayako tayari. Kwa mtazamo huo, kama nilivyosema kwamba Serikali iliingia na mkataba na kampuni ya Halotel au Viettel kwa ajili ya kupeleka mawasiliano kwenye maeneo hayo. Naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, eneo lake litakuwepo kwenye mpango wa kupelekwa mawasiliano mwaka huu.

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Kata za Semembela, Isagenhe na Kahama ya Nhalanga hazina kabisa mawasiliano ya simu za mkononi:- Je, ni lini Kata hizi zitapatiwa huduma hii muhimu ya mawasiliano ya simu za mkononi?

Supplementary Question 3

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Kwa kuwa tatizo la Bukene linafanana kabisa na Korogwe Vijijini hasa kwenye Kata ya Kizara. Mwaka 2012 tulimchukua Naibu Waziri hapa alikwenda mpaka kule akawaahidi wananchi wa Kizara kwamba mwishoni mwa mwaka 2012 mnara utapatikana. Cha kushangaza mpaka leo hii hakuna cha mnara wala namna ya kupata mnara. Je, ni lini sasa Serikali itawapelekea wananchi wa Kizara mnara?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tutagawa fomu kwa ajili ya Waheshimiwa Wabunge wote ambao wanahitaji mawasiliano kwenye vijiji vyao ili na sisi tuwe na database ya uhakika. Pia nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba kijiji chake kama nilivyosema mwaka huu kitapelekwa mawasiliano, kupitia kwa kampuni ya Viettel au Halotel Tanzania. (Makofi)