Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Stephen Julius Masele
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shinyanga Mjini
Primary Question
MHE. STEPHEN J. MASELE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itataifisha Kiwanda cha Nyama Shinyanga Mjini baada ya mwekezaji kushindwa kukiendesha?
Supplementary Question 1
MHE. STEPEN J. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanda hiki kina umri wa miaka 42 zaidi hata ya umri wangu na tangu kimejengwa hakijawahi kufanya kazi. Nataka majibu ya uhakika kwamba ni lini kiwanda hiki kitafanya kazi na Serikali imetoa muda gani kwa mwekezaji huyu kuhakikisha kiwanda hiki kinafanya kazi?
Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanda hiki kimechukua maeneo na mashamba ya wananchi wa Kata za Chibe, Old Shinyanga pamoja Ndembezi. Je, Serikali iko tayari kuruhusu vijana kutumia maeneo hayo kwa kilimo cha bustani ili wajipatie kipato na ajira wakati tathmini hiyo inaendelea kwa miaka 42 ambayo wamesubiri?
Name
Charles John Mwijage
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muleba Kaskazini
Answer
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naelewa concern ya Mheshimiwa Mbunge anataka ajira kwa ajili ya wananchi wa Shinyanga, lakini anataka soko la uhakika kwa mifugo yote ya Kanda ya Ziwa. Katika miradi inayonipa shida ni pamoja na kiwanda hiki, huyu mwekezaji hakufanya vizuri. Katika watu ambao katika utendaji wangu wa kazi nakuwa mwangalifu nao ni mwekezaji huyu, siyo mwekezaji mzuri, nimemkabidhi kwa Treasurer Registrar anamfuatilia, kuna masuala ya kisheria. Huyu mtu ametumia kiwanda kile akakopa pesa, sasa anategea tumnyang‟anye kiwanda kile kusudi governments guarantee na pesa aliyokopa iishe, siyo mtu mzuri. Mjomba uniache nimfuatilie kwa uangalifu ili tutakapomkamata tumalize kitu once and for all.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kutumia maeneo, huyu mtu yuko under surveillance na nimekwambia siyo mtu mzuri. Kwa hiyo, maeneo yake msiyaguse asije akasema alishindwa kuendeleza kwa sababu tuligusa maeneo yake. Hata hivyo, ni katika maeneo ambayo nataka nitoe majibu yake haraka sana. Nikueleze, hata tajiri namba moja anafuatilia suala hili.
Name
Ally Seif Ungando
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kibiti
Primary Question
MHE. STEPHEN J. MASELE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itataifisha Kiwanda cha Nyama Shinyanga Mjini baada ya mwekezaji kushindwa kukiendesha?
Supplementary Question 2
MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Kibiti ni mojawapo ya Wilaya inayolima mihogo kwa wingi lakini ina tatizo la soko ambapo mihogo mingi hutegemewa kuuzwa kwenye Mwezi wa Ramadhani. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kupeleka kiwanda cha kuchakata mihogo katika Wilaya mpya ya Kibiti?
Name
Charles John Mwijage
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muleba Kaskazini
Answer
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanda cha mihogo, nakuomba Mheshimiwa Ungando uje unione nitakuelekeza kwa Meneja wa SIDO. Pia nitakwenda nawe bega kwa bega tuangalie fursa ya malighafi iliyopo na kiwanda cha namna gani kinaweza kuanzishwa katika mipango hii. Nitafanya kazi na wewe.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved