Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA aliuliza:- Halmashauri za Mkoa wa Mtwara kwa kushirikiana na Kampuni ya HELM wanakusudia kujenga Kiwanda cha Mbolea huko Msanga Mkuu, Mtwara Vijijini. Je, ni lini Serikali itaridhia mradi huo kuanza?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri lakini nilitaka kwanza afanye marekebisho ya jina, naitwa Hawa na siyo Awa. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, napenda kujua huo mwaliko wa HELM umetumwa lini ili tuweze kufuatilia?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Mheshimiwa Waziri amekuwa akituhamasisha sana Wabunge kuwahamasisha wawekezaji katika mikoa yetu. Napenda kufahamu ni vivutio gani anavyo ambavyo angependa pale tunapohamasisha tuviseme ili tusikwame kama ambavyo viongozi wa Mkoa wa Mtwara walivyokwama katika suala hili la kiwanda cha HELM?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, sawa. Nahitaji kutoa maelezo kidogo kwa lile la kwanza hata home boy wangu amuita hivyo hivyo. Lile jina ambalo siwezi kulisema hata home boy wangu huwa anamwita hivyo hivyo. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ni kwamba kampuni ya HELM imealikwa na TPDC siku 10 zilizopita. Mimi pamoja na yeye Mheshimiwa tutawasiliana na TPDC na kwa kauli yangu nawaagiza TPDC wawasiliana na huyo mwekezaji na watoe taarifa wakati tukiwa hapa Dodoma.
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie vivutio wanavyovizungumzia, tatizo hasa siyo vivutio ni ucheleweshaji wa mradi walioupata watu wa Mtwara. Kilichopelekea ucheleweshwaji wa mradi ni taarifa za kisayansi. Wakati tukiwa na TCF 2 Mtwara tulikuwa hatuna uhakika kama gesi ile ingeweza kutosha mahitaji yetu hasa mahitaji ya umeme. Uvumbuzi wa gesi TCF 2.17 za Ruvu, zimetupa kiburi na kujidai kwamba tunaweza kuwasha mitambo. Ndiyo maana tarehe 10 Julai, kuna mwekezaji nakwenda kuzindua mtambo wake wa megawati 400 pale Bagamoyo. Kwa hiyo, hayo yaliyopita yamekwisha, ukitaka vivutio vinapatikana kwenye Investment Policy, viko wazi na vingine nitaandika kwenye jedwali. Ninyi njooni mnione mimi, mwekezaji akikwama mje mnione, ikikwamishwa na Wizara yoyote njooni mnione mimi. Mimi ndiyo receptionist, nitaweza ku-clear matatizo yanayokwamisha uwekezaji.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA aliuliza:- Halmashauri za Mkoa wa Mtwara kwa kushirikiana na Kampuni ya HELM wanakusudia kujenga Kiwanda cha Mbolea huko Msanga Mkuu, Mtwara Vijijini. Je, ni lini Serikali itaridhia mradi huo kuanza?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Kiwanda cha Chai cha Mponde kimefungwa takribani miaka mitatu sasa na Msajili wa Hazina alivyokuja alitamka kuwa zimetengwa shilingi bilioni 4 na kwenye bajeti ya mwaka huu hazipo. Je, Serikali ina mpango gani wa kufungua Kiwanda cha Chai Mponde ili wakulima wale wasiendelee kupata adha ile?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Kiwanda cha Mponde, shilingi bilioni 4, usitegemee pesa ya kuingia kwenye viwanda uione kwenye bajeti yangu, tunawasiliana na watu wenye pesa watawekeza pale. Nimekwenda mbele zaidi, nafanya mazungumzo na Serikali ya Misri kusudi chai ya Kagera - Maruku na chai ya Mponde - Tanga iuzwe moja kwa moja Misri. Mimi nina maslahi na kiwanda cha Mponde.