Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:- Wakulima wa tumbaku wamekuwa wakilipwa kwa dola pindi wanapouza mazao yao:- (a) Je, nani huwapigia hesabu za kitaalamu? (b) Je, wakulima wote wamefunguliwa akaunti benki?

Supplementary Question 1

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Naibu Waziri amesema kwamba watumishi ambao wameajiriwa na ushirika huo wanapewa semina mbalimbali za kitaalamu na kwa kuwa kama tunavyofahamu suala la hesabu kwa nchi yetu ni tatizo, hawajui hesabu, je, Serikali inajua kwamba mpaka hivi sasa wanunuzi wa tumbaku ambao wamejitawala wanadaiwa na wakulima shilingi bilioni 14 za mwaka 2014/2015 ambazo hawajalipwa mpaka sasa? Je, Serikali inasemaje kufuatilia suala hilo? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, mpaka hivi sasa soko la mwaka huu halijaanza, linasuasua na unapochelewa kupima tumbaku maana yake unapunguza kilo za tumbaku. Je, Serikali inasema nini kufuatilia suala la soko la tumbaku kwa sasa hivi ili liweze kukamilika kwa muda muafaka?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kama anavyosema kwamba wakulima wa tumbaku wa Tabora na wa mikoa mingine wanadai fedha nyingi, wanawadai vyama vya ushirika pamoja na wanunuzi wa tumbaku. Serikali imekuwa ikiendelea na jitihada za kuhakikisha kwamba fedha hizi zinalipwa. Tayari mafaili ya watu waliohusika na ubadhirifu mkubwa katika Mkoa wa Tabora yameshawasilishwa Polisi taratibu nyingine ziendelee ili wahusika waweze kupelekwa mbele ya sheria ikiwezekana wakulima waweze kupata fedha zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu soko la tumbaku, ni kweli kama Mheshimiwa alivyosema kwamba suala la soko la tumbaku bado linasuasua na Serikali imekuwa ikijitahidi kufanya njia mbalimbali ili kuhakikishia wananchi kwamba soko halitapata shida. Jitihada hizi ni pamoja na kuhakikisha kwamba wanapatikana wanunuzi wengine wa tumbaku ili kuondoa ukiritimba wa wanunuzi wachache ambao mara nyingi wao ndiyo wanaoamua bei lakini vilevile wao pekee ndiyo wanaendesha soko la tumbaku. Tunaamini kwamba wanunuzi wengine wakipatikana itaondoa tatizo hili na italeta ushindani na hivyo kuondoa tatizo katika bei na soko la tumbaku.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tulishaahidi kwamba tukitoka kwenye Bunge hili tutaenda Tabora na maeneo mengine kwa wadau wa tumbaku tujadiliane namna bora ya kuboresha zao la tumbaku. Nimhakikishie tu kwamba pamoja na Mheshimiwa Mwigulu Nchemba kuhama, ambaye ndiye aliyetoa ahadi, ahadi ile ilikuwa ni ya Wizara na iko pale pale. Niwahakikishie tu kwamba tukimaliza bajeti Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ataelekea Tabora kwa ajili ya kwenda kuongea na wadau kuhusu masuala ya tumbaku.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:- Wakulima wa tumbaku wamekuwa wakilipwa kwa dola pindi wanapouza mazao yao:- (a) Je, nani huwapigia hesabu za kitaalamu? (b) Je, wakulima wote wamefunguliwa akaunti benki?

Supplementary Question 2

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wakulima wa tumbaku wamekuwa wakikopwa na pesa zao zinachukua muda mrefu sana kuja kulipwa, Serikali ina utaratibu gani wa kuwasaidia wananchi hawa wanaolima tumbaku hasa Mkoa wa Tabora kuhakikisha kwamba wanalipwa pesa yao na riba kama wanavyofanya mabenki?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa utaratibu wa tumbaku kuchukuliwa na baadaye ndipo wakulima hulipwa kumesababisha matatizo makubwa sana na ndicho hasa chanzo cha kurundikana kwa madeni mengi ya wakulima kutoka kwenye Vyama vya Ushirika. Tunafahamu kwamba mfumo mzima wa ushirika siyo kwenye tumbaku tu lakini katika mazao mengi una changamoto na ndiyo maana Bunge hili lilifanya uamuzi mzuri sana wa kuleta Sheria mpya ya Tumbaku, Sheria Na.6, 2013 ili kuondokana na changamoto hizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaendelea kuimarisha ushirika ili isitokee tena kwamba wakulima wanachukuliwa tumbaku yao na wanakaa miaka mingi bila kulipwa. Kwa hiyo, tunaamini kwamba kwa mfumo huu wa ushirika ambao tunauleta sasa haitawezekana tena wananchi kukopwa lakini tunahakikisha kwamba tumbaku ya wananchi inakuwa inalipwa moja kwa moja. Badala ya kuchukua kwanza na kulipa baadaye ni kwamba tutakuwa tunatumia mfumo kama ule wa korosho ambapo tumbaku ikishakusanywa kwenye Vyama vya Msingi wanunuzi wanakuja kununua pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inafahamu changamoto hii, inafanyiwa kazi na tunaamini katika mfumo uliokuja wa Vyama vya Ushirika utarekebisha matatizo makubwa ambayo yametokea. Vilevile sheria hii imeweka mazingira mazuri sana ya kuwabana na kuwafikisha katika vyombo vya sheria si tu wafanyakazi wa Vyama vya Ushirika lakini vilevile hata Maafisa Ushirika ambao wanashirikiana katika kuwahujumu wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilieleze tu Bunge lako Tukufu kwamba changamoto kubwa iliyoletwa na mfumo wa ushirika ambao tunauondoa ni kwamba kumejengeka utatu usio mtakatifu kati ya viongozi wa Vyama vya Ushirika, mabenki na watendaji wa Serikali. Kwa hiyo, tunahakikisha kwamba utatu huu ambao umeleta matatizo kwa wananchi unavunjwa ili wananchi waweze kupata haki yao na kusiendelee kutokea changamoto katika zao la tumbaku.

Name

John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:- Wakulima wa tumbaku wamekuwa wakilipwa kwa dola pindi wanapouza mazao yao:- (a) Je, nani huwapigia hesabu za kitaalamu? (b) Je, wakulima wote wamefunguliwa akaunti benki?

Supplementary Question 3

MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nimuulize Waziri swali dogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Bodi ya Tumbaku inafanya kazi ndani ya Serikali na kwa maagizo ya Serikali; na kwa kuwa Bodi ina upungufu wa fedha unaosababisha kutokupatikana wanunuzi wengi wa kutosha, je, Serikali iko tayari kuwaongezea Bodi ya Tumbaku pesa ili waongeze wanunuzi wa tumbaku na kuongeza masoko? Ahsante.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Bodi ya Tumbaku inakabiliwa na changamoto za fedha. Hata hivyo, Serikali imekuwa ikijaribu kuangalia uwezekano wa Bodi za Mazao kujitegemea zaidi badala ya kutegemea ruzuku ya Serikali. Kwa hiyo, utaratibu ambao unatumika ni kuhakikisha kwamba Bodi ya Tumbaku inaweza ikapata fedha za kujiendesha yenyewe bila kupata ruzuku kubwa kutoka Serikalini. Ndiyo maana tunafikiria kuwa na Mfuko wa Bodi ya Tumbaku kama ilivyo kwenye korosho na kahawa ili wadau wenyewe waweze kujiendesha bila kuingiliwa na Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimueleze vilevile Mheshimiwa Mbunge kwamba suala la soko la tumbaku ni zaidi ya ukosefu wa fedha kwa Bodi ya Tumbaku. Soko la tumbaku linaathirika na namna zao linavyochukuliwa duniani. Wote mnafahamu kwamba tumbaku ndiyo zao la pekee ambapo kunakuwa na vita sana kwa hiyo inafanya wanunuzi wengi mara nyingine wasijiingize kwenye tumbaku. Hata hivyo, tunaendelea kutafuta aina zingine za tumbaku ambazo zinawavutia watumiaji wengi hasa Wachina.
Mheshimiwa Naibu Spika, watumiaji wa China wanapendelea tumbaku inayozalishwa Zimbabwe. Kwa hiyo, tumeongea na Bodi ya Tumbaku wajaribu kuangalia ni namna gani tumbaku ambayo inazalishwa katika maeneo mengine kama Zimbabwe na ambayo inapendwa na watumiaji wengi wa China inaweza ikaoteshwa nchini. Kwa hiyo, jitihada zinaendelea kwa ajili ya kuweza kuimarisha bei ya tumbaku.

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:- Wakulima wa tumbaku wamekuwa wakilipwa kwa dola pindi wanapouza mazao yao:- (a) Je, nani huwapigia hesabu za kitaalamu? (b) Je, wakulima wote wamefunguliwa akaunti benki?

Supplementary Question 4

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri alipojibu maswali ya nyongeza amesema kwamba makampuni ya wanunuzi ni machache yako kama matatu na yanafanya kiburi kwa sababu kwao ni cartel na amesema kwamba Wachina wana nafasi ya kununua tumbaku hapa kwetu kwa sababu Wachina ni wengi sana hapa duniani. Je, Serikali inasemaje kuyaleta Makampuni ya Kichina kuja kununua tumbaku hapa Tanzania na kuwapunguzia wakulima adha wanayopata?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba Serikali inatambua changamoto inayoletwa na ukiritimba katika ununuzi wa zao la tumbaku. Ndiyo maana Wizara yangu imechukua hatua kadhaa ili kutafuta wanunuzi wengine. Nipende tu kumtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba wiki mbili zilizopita tumekutana hapa Dodoma na Balozi wa China ili kuangalia uwezekano wa kuwapata wanunuzi zaidi. Tumeongea nao ili confideration of China Industries waweze kuruhusu kampuni zao ziweze kuja kununua tumbaku Tanzania, mijadala hiyo inaendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tumeongea na watu wa Vietnam ili kuangalia uwezekano wa kuwapata wanunuzi kutoka Vietnam. Kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba jitihada zinaendelea na tuna hakika kwamba wanunuzi wengine wa tumbaku watapatikana.