Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY (K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais kwenye kampeni za uchaguzi aliahidi kupanua mpaka wa Game Reserve iliyoko Maswa:- Je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali iliongeza mipaka yake ikawafuata wananchi katika vijiji vinane vya Mwamumtani, Mwalali, Ndung‟wa, Ndinho, Ntantulu, Kiliju, Longalombogo na Shishani na haikuwashirikisha wananchi, je, ni lini sasa eneo hili litarudi kwa wananchi kwa kuwashirikisha wananchi?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa amesema umegaji wa eneo hili haujaleta tija na haujamaliza changamoto ya wananchi na kwa kuwa Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni akiwa kwenye Kijiji cha Nanga katika Kata ya Kinameli aliliona hili na alitaja Sheria ya Ardhi, Na.4 akasema kwamba akiwa Rais eneo hili atalirudisha kwa wananchi. Je, kwa nini Mheshimiwa Naibu Waziri anapingana na ahadi ya Rais?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, nazingatia kujibu kwa kifupi, moja kwamba zoezi lililofanyika huko nyuma la upanuzi wa mipaka halikushirikisha wananchi na ni lini Serikali itashirikisha wananchi? Kwanza si kweli kwamba Serikali inaweza kupanua mipaka ya eneo lolote lile hasa mipaka ya wananchi wanaopakana na hifadhi bila kushirikisha wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, bado Serikali ina nia njema ya kufanya zoezi la kupitia mipaka kwa namna bora zaidi kuliko ilivyokuwa siku za nyuma. Ndiyo maana nimesema kwenye jibu la msingi kwamba tunakwenda sasa kushirikisha Wizara nyingi zaidi na tunakwenda kufanya ushirikishwaji zaidi katika hatua hii lakini mara hii tunakwenda kuweka vizuri kumbukumbu ili hata vizazi vijavyo vije kuona kwamba zoezi hilo lilifanyikaje kuliko ilivyokuwa siku za nyuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili la ahadi ya Mheshimiwa Rais ikihusisha Sheria Namba 4, napenda kujibu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza haiwezekani kabisa tukafika mahali tukaweza kupingana na maelekezo ya Mheshimiwa Rais. Hilo ni jambo ambalo haliwezekani kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama alikuwa anataka kujua utekelezaji sasa wa hiyo ahadi ya Mheshimiwa Rais ambayo aliitoa, Rais akishatoa ahadi maana yake tayari ni amri kwetu sisi watekelezaji. Nimekwishamwambia kwenye jibu la msingi na jibu lake litakuwa ni hilo na hapa nitoe tu wito kwa ufupi hata kwa maswali ya nyongeza mengine kama inawezekana basi jibu litakuwa ni hilihili tu kwamba Waheshimiwa Wabunge wote wavute subira, wasubiri utaratibu huu ambao Serikali inaenda kufanya kwa kushirikisha Wizara nilizozisema ili twende tukatafute suluhu sasa ya matatizo haya kama nilivyokwishayasema.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY (K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais kwenye kampeni za uchaguzi aliahidi kupanua mpaka wa Game Reserve iliyoko Maswa:- Je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Japokuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amesema majibu yatakuwa ni yaleyale na mimi naomba nikumbushie.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Maswa linafafana na tatizo lililoko Ulanga katika Kata ya Ilagua, Lupilo, Minepa na Milola ambapo Mheshimiwa Rais aliahidi kuhalalisha hili eneo la buffer zone ili wananchi hawa wafaidi tunu ya pekee ya ardhi tuliopewa. Je, ni lini Serikali itahalalisha na itatekeleza ahadi hii ili wananchi hawa wafaidi?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante. Kwanza nimshukuru pia Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maliasili kwa majibu mazuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tu nimkumbushe Mheshimiwa Mbunge kwamba maswali haya mengi yanayohusiana na migogoro ya mipaka na hasa pale yanapogusa Wizara zaidi ya moja tulikwishayazungumzia na kuyatolea maelekezo. Kama alivyojibu Naibu Waziri wa Maliasili Wizara tutakwenda kukaa, tutafika kwenye maeneo ambayo yanahusika baada ya wataalam kuwa wamepitia maeneo hayo na kujua ile mipaka inayolalamikiwa kuona kama kweli mpaka ulipanuliwa na kufuata watu au mahitaji ya watu yamekuwa ni makubwa kiasi kwamba sasa inahitajika kuangalia upya mipaka iliyowekwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, suala hili ningeomba sana Waheshimiwa Wabunge wawe na uvumulivu kwa sababu ni maeneo mengi yana mgogoro huo na maeneo mengi yanahitaji pia kupitiwa upya ili kuweza kukidhi ile haja ambayo Waheshimiwa Wabunge wanaiona kwamba inafaa kwa wakati huo. Ahsante.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY (K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais kwenye kampeni za uchaguzi aliahidi kupanua mpaka wa Game Reserve iliyoko Maswa:- Je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, sisi suala la Pori la Mukungunero ni tofauti na maeneo mengine kwa sababu mauaji yamekwishatokea, maaskari watatu walikwishauawa pale, wananchi walishaandika barua mpaka kwa Waziri Mkuu na Waziri Mkuu akapeleka suala hili Wizara ya Maliasili lakini tangu mwaka 2013 suala la Mukungunero halijashughulikiwa. Naomba suala la Mkungunero sasa litazamwe kwa jicho lingine la haraka. Je, ni lini sasa Wizara ya Maliasili itaishughulikia barua iliyoandikwa kwao na Waziri Mkuu aliyepita?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, jibu fupi kabisa, naomba nimjibu Mheshimiwa Mbunge swali lake la nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kwa maelezo aliyoyatoa ni wazi kwamba suala hili la Mkungunero, kwa jinsi swali lilivyoulizwa na uhalisia ulivyo lina upekee kama ambavyo na yeye ameweza kubainisha. Kwa hiyo, ushughulikiaji wa suala hili ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii unavuka mipaka, unahusisha masuala yanayohusiana na Wizara ya Mambo ya Ndani. Hapo unahusisha polisi na mambo mengine ya utendaji wa Kiserikali lakini nje ya mipaka ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Hata hivyo, kwa sababu ni suala linalohusiana na Wizara ya Maliasili na Utalii basi tutakwenda kuona namna ambavyo tunashirikiana na vyombo vingine ambavyo vinahusika katika kuweka msukumo kukamilisha ushughulikiaji wa changamoto hii.