Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Dhahabu ni kati ya madini yanayozalishwa na wachimbaji wadogo wadogo Mkoani Katavi; na kumekuwepo na suala la asilimia hafifu ya dhahabu ya Mpanda Kati ya 60% hadi 90%. Uhafifu huu ulitokana na ukweli kwamba sehemu ya asilimia ni madini mengine kama fedha, shaba na kadhalika, lakini katika mauzo wachimbaji wamekuwa wakilipwa thamani ya dhahabu tu. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwawezesha wachimbaji hawa kwa kuwapatia teknolojia sahihi ya kutofautisha dhahabu, shaba na fedha ili kuongeza thamani na pato halisi kwa wachimbaji hao na kuinua Pato la Taifa?

Supplementary Question 1

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri ambayo kimsingi yana afya, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa mpango huo mzuri wa Serikali ili wachimbaji wadogo waweze kufikia hatua ya kupata mpango huo mzuri, ni lazima wawe na maeneo. Naibu Waziri anasema nini kwa maana ya kutenga maeneo kwa eneo hilo la Mpanda? Hilo ni swali la kwanza. (Makofi)
Swali la pili, nafahamu Wizara kwa ujumla wake imekuwa ikisaidia wachimbaji wadogo nchini. Je, ni utaratibu upi unaotumika kwa maana ya suala zima la utoaji ruzuku kwa wachimbaji hawa wadogo? Naliuliza hilo ili iwe faida kwa wachimbaji wote wadogo nchini? Nakushukuru.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nipate ridhaa yako nimshukuru sana Mheshimiwa Kapufi. Kwanza nampongeza kuwa mchimbaji mdogo kati ya wachimbaji wadogo maarufu hapa nchini. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Kapufi kama mdau mzuri na ni mchimbaji mzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, nampongeza sana Mheshimiwa Kapufi kwa kuwawakilisha vyema wananchi wa Mpanda. Mheshimiwa Kapufi nikuhakikishie kwamba wananchi wako ambao ni wachimbaji wadogo, kama ambavyo wewe unachimba nao watafikia kiwango chako cha uchimbaji kama unavyoendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naomba nijielekeze kwenye maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kapufi. Ni lini Serikali itawatengea maeneo wachimbaji wadogo?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa hivi Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) anafanya tathmini kwa mambo matatu; tathmini ya Kijiokemia, tathmini ya Kijiolojia na tathmini ya Kijiofizikia na mwezi wa saba tunaanza kuwatengea maeneo hayo. Zoezi la kuwatengea wananchi maeneo litakuwa ni endelevu; kuanzia mwezi wa saba na kuendelea tutafanya kazi ya kuwatengea maeneo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa Serikali imetenga hekta 12,000 kwa ajili ya kuwatenga maeneo, kadhalika, imetenga shilingi milioni 640 kwa ajili ya Wakala wa Jiolojia kutathmini maeneo ambayo yatatengwa. Maeneo ambayo tutayatenga ni mengi sana ikiwa ni pamoja na Lindi, Geita, Sambaru – Singida, pamoja na Londoni. Maeneo mengine tutakayotenga kule Mpanda ni pamoja na eneo la Dirifu, Katuma, Society pamoja na eneo la Katasunga. Maeneo yote ya Mpanda Mheshimiwa Kapufi tutaendelea kuyatenga. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la pili kuhusu utaratibu wa ruzuku, ni kweli kabisa mwaka 2015/2016, Serikali ilitenga shilingi bilioni 7.24 na mwaka huu kwa ridhaa ya Waheshimiwa Wabunge tumetenga shilingi bilioni 6.68, hii ni kwa ajili ya kuwagawia wananchi kama ruzuku.
Mheshimiwa Naibu Spika, niongeze kidogo kuhusu hili. Utaratibu tunaotumia kwa sasa, kwanza kabisa leseni lazima ziwe za Watanzania peke yake kwa asilimia mia moja. Hilo la kwanza. Pili, leseni hizo lazima ziwe hai na zinafanyiwa kazi; na tatu, tunawahamasisha sana wananchi wajiunge kwenye vikundi ili ruzuku hii iwanufaishe Watanzania wengi. La nne, tumeongeza sasa badala ya kutenga dola 50,000 kwa msimu huu, tutatenga dola 100,000 kwa kila atakayekidhi vigezo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ningesema mengi sana kwenye eneo hili, lakini niwahamasishe Watanzania; Mheshimiwa Kapufi na Waheshimiwa Wabunge wengine ili waweze kunufaika na ruzuku hii.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Dhahabu ni kati ya madini yanayozalishwa na wachimbaji wadogo wadogo Mkoani Katavi; na kumekuwepo na suala la asilimia hafifu ya dhahabu ya Mpanda Kati ya 60% hadi 90%. Uhafifu huu ulitokana na ukweli kwamba sehemu ya asilimia ni madini mengine kama fedha, shaba na kadhalika, lakini katika mauzo wachimbaji wamekuwa wakilipwa thamani ya dhahabu tu. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwawezesha wachimbaji hawa kwa kuwapatia teknolojia sahihi ya kutofautisha dhahabu, shaba na fedha ili kuongeza thamani na pato halisi kwa wachimbaji hao na kuinua Pato la Taifa?

Supplementary Question 2

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza naomba ni-declare interest, na mimi ni mchimbaji mdogo japokuwa sijawahi kunufaika kutokana na mfumo mbovu wa Serikali. (Kicheko)
Tatizo lililoko Mpanda Mjini linafanana na lililoko katika Jimbo langu la Ulanga. Je, sasa Serikali haioni umuhimu wa kuwaelimisha na kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo wa Jimbo la Ulanga ili waweze kuyathaminisha madini haya wanayoyapata ili waweze kuyauza katika thamani halisi inayoendana na soko?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, tunaona umuhimu, hilo la kwanza. Tunaona umuhimu wananchi wako Mheshimiwa Mbunge kuendelea kuwaelimisha, lakini siyo kuwaelimisha tu, hata kuwapatia ruzuku wakikidhi vigezo. Napenda tu kusema katika Jimbo la Ulanga, maeneo ya Mvomero, maeneo ya Iringa, maeneo ya Singida, yote kwa pamoja tunaendelea kuyatathmini tuwatengee wananchi. Kwa hiyo, pamoja na kutoa elimu, tunawahamisha Waheshimiwa Wabunge wawahamishe wananchi washirikiane na Waheshimiwa Wabunge ili kunufaika na rasilimali hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwezi wa kwanza mwaka huu, Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini amekaa sana na wachimbaji wadogo Wawakilishi wao wa Katavi, Singida pamoja na kwa Mheshimiwa Mbunge wa Ulanga. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mlinga nakuhakikishia tutaendelea kusaidiana na wananchi wako kuwaelimisha waweze kunufaika na mapesa haya.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Dhahabu ni kati ya madini yanayozalishwa na wachimbaji wadogo wadogo Mkoani Katavi; na kumekuwepo na suala la asilimia hafifu ya dhahabu ya Mpanda Kati ya 60% hadi 90%. Uhafifu huu ulitokana na ukweli kwamba sehemu ya asilimia ni madini mengine kama fedha, shaba na kadhalika, lakini katika mauzo wachimbaji wamekuwa wakilipwa thamani ya dhahabu tu. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwawezesha wachimbaji hawa kwa kuwapatia teknolojia sahihi ya kutofautisha dhahabu, shaba na fedha ili kuongeza thamani na pato halisi kwa wachimbaji hao na kuinua Pato la Taifa?

Supplementary Question 3

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na kuitaja Singida, naomba atusaidie kwamba makampuni yale ambayo yanachukua leseni halafu wanakaa nayo muda mrefu bila kufanyia kazi na hivyo kuwafanya wachimbaji wadogo wasiende kufanya uchimbaji kwenye maeneo yenye madini kama Londoni, Sambaru, Muintiri, Sekenke pamoja na Mkalama. Ninaomba atoe tamko hapa kwa makampuni hayo na ni lini atatekeleza? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzia sasa na kuanzia huko nyuma na tunaendelea kufanya hivyo. Naomba nichukue nafasi hii kutoa rai kwamba wachimbaji wote ambao hawayafanyii kazi maeneo yao, Serikali itayachukua na huo ni utaratibu wa kisheria. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Madini kifungu Na. 36(1), Sheria Namba 14 ya mwaka 2014 inakataza mwekezaji yeyote kushikilia maeneo bila kuyaendeleza. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mlata kwamba wananchi wa Sekenke, Sambaru, Londoni, Muintiri na wananchi wengine wote tunawapatia maeneo kutokana na wawekezaji ambao hawayaendelezi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili niwahakikishie na niwaombe sana Watanzania kwamba sasa tunatekeleza sheria. Maeneo yote ambayo yalikuwa hayafanyiwi kazi na wawekezaji na hasa wawekezaji wa nje, lakini hata wawekezaji wa ndani ambao walikuwa hawayaendelezi, sasa sheria inaanza kuchukua mkondo wake. Maeneo tutayachukua, tutayatumia kwa ajili ya wachimbaji wadogo waweze kupata maeneo ya uhakika kwa ajili ya kujipatia kipato.
Kwa hiyo, namshukuru Mheshimiwa Mlata, kama ambavyo siku zote anafanya; na Kampuni ya Ashanti Mining ambayo iko kwake, tunafanya mazungumzo nayo ili ikiwezekana na yenyewe iweze kuachia maeneo kwa ajili ya wananchi wa Singida.