Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI (K. n. y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI) aliuliza:- Ni zaidi ya miaka mitano sasa tangu Meli ya MV Butiama isitishe huduma zake katika Ziwa Victoria kati ya Mwanza na Nansio (Ukerewe) hali inayosababisha shida na usumbufu mkubwa wa usafiri kwa wakazi wa Ukerewe. (a) Je, ni lini meli hiyo ya MV Butiama itatengenezwa na kuendelea kutoa huduma kati ya Mwanza na Nansio? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta meli mpya sasa ikizingatiwa kuwa meli ya MV Clarius imechakaa sana?

Supplementary Question 1

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na ninamshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri sana, nina maswali mawili ya nyongeza:-
Kwa kuwa wananchi wa Mwanza na Ukelewe wamepata usumbufu zaidi ya miaka mitano kwa kukosa usafiri; na kwa kuwa ni sehemu muhimu sana kwa wavuvi; ni lini sasa Serikali itawapa usafiri wa dharura wananchi wale ili waone umuhimu wa Serikali yao inavyowasaidia?
Swali la pili, kwa kuwa tatizo la Ukerewe linalingana kabisa na Tanga, wananchi wa Tanga, Pemba, Unguja pamoja na Bagamoyo wanahitaji meli kama hiyo ili iwasaidie; je, Serikali ina mpango gani wa kuwahakikishia wananchi wa Ziwa, umetaja Ziwa Nyasa, umetaja Ziwa Victoria, umetaja Ziwa Tanganyika; lakini je, katika Bahari ya Hindi wananchi wa Tanga, Pemba, Unguja na Bagamoyo ni lini na wao watapata meli ili na wao waepukane na kile kimbunga cha kila siku kufariki kwenye meli? Ahsante sana.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru Mheshimiwa Stephen Ngonyani, Mbunge wa Korogwe Vijijini kwa namna ambavyo ameniamsha namna ya kufuatilia masuala ya wananchi wa Korogwe Vijijini na mimi vilevile Namtumbo, kwa kweli ninaomba Wabunge wengine wafuate nyayo zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu dharura nadhani Mheshimiwa anafahamu kwamba tuna usafiri ambao sasa hivi upo, isipokuwa hautoshelezi. Kwa masuala ya dharura usafiri unapatikana, nia yetu kubwa ni kuondokana na meli hizi chakavu, tuzitengeneze na tulete mpya. Kwa hiyo, masuala ya dharura siyo tatizo yamekuwa taken care off.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali la pili niliwahi kujibu swali kama hilo katika Bunge hili kwamba katika miaka ya 1980 - 1990 tuliamua kuingiza sekta binafsi katika shughuli za usafiri na kwa upande wa meli tulianzia na upande wa Bahari ya Hindi unafahamu kwamba kuna wasafirishaji binafsi wengi wanafanya shughuli hizo za usafiri. Kama ombi lako maana yake unataka Serikali iondoe hiyo sera ilete sera nyingine tutaliwasilisha Serikalini likajadiliwe tuone hasara na faida yake, kwa sasa naomba tuendelee kupata huduma za meli kutoka kwa wasafirishaji binafsi, TACOSHILI tulishaisimamisha miaka ya 1990.

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ngonyani hasa sehemu (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi tunavyoongea upo usafiri wa kudumu baina ya Dar es Salaam, Unguja na Pemba. Ipo meli ambayo inaitwa MV Mapinduzi II ambayo ni meli ya kisasa inayosafiri baina ya Unguja na Pemba na tutaongea na Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano huko Zanzibar kuhakikisha kwamba meli hii inasafiri kutoka Pemba kwenda Tanga kama ilivyokuwa hivyo zamani.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI (K. n. y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI) aliuliza:- Ni zaidi ya miaka mitano sasa tangu Meli ya MV Butiama isitishe huduma zake katika Ziwa Victoria kati ya Mwanza na Nansio (Ukerewe) hali inayosababisha shida na usumbufu mkubwa wa usafiri kwa wakazi wa Ukerewe. (a) Je, ni lini meli hiyo ya MV Butiama itatengenezwa na kuendelea kutoa huduma kati ya Mwanza na Nansio? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta meli mpya sasa ikizingatiwa kuwa meli ya MV Clarius imechakaa sana?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.
Kwa kuwa kulikuwa na ahadi ya Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kununua meli katika maziwa makuu matatu kwa maana ya Ziwa Tanganyika, Ziwa Victoria na Ziwa Nyasa, na katika bajeti hii ya Mawasiliano na Uchukuzi kuna ununuzi wa meli moja ya Ziwa Victoria, lakini hivi karibuni Waziri wa Katiba na Sheria alisikika akipongeza uundwaji wa meli mpya ya mizigo na abiria katika Ziwa Nyasa. Je, ni lini sasa meli mpya itapelekwa katika Ziwa Tanganyika ili tuachane na meli ya MV Liemba?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kiongozi wetu wa Serikali ya Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kuleta meli mpya katika maziwa yote makuu matatu na ahadi hiyo ilirudiwa na Rais wa Awamu ya Tano Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwamba atatekeleza ahadi hiyo ambayo mwanzo ilitolewa na Mheshimiwa Kikwete.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie hili tuliloliongelea katika jibu langu la swali la msingi ndiyo kuanza kutekeleza ahadi ya viongozi hawa wakuu, tunaanza na meli ya MV Victoria na unafahamu kwamba wakati kuna meli ndogo inatengenezwa kule Nyasa baada ya hapo tutafuatia na meli katika
Ziwa Tanganyika na hatimaye ahadi hizo za viongozi wakuu zitatekelezwa katika kipindi hiki cha miaka mitano tulichoahidi. Tuanze na hatua moja halafu tutasonga mbele.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI (K. n. y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI) aliuliza:- Ni zaidi ya miaka mitano sasa tangu Meli ya MV Butiama isitishe huduma zake katika Ziwa Victoria kati ya Mwanza na Nansio (Ukerewe) hali inayosababisha shida na usumbufu mkubwa wa usafiri kwa wakazi wa Ukerewe. (a) Je, ni lini meli hiyo ya MV Butiama itatengenezwa na kuendelea kutoa huduma kati ya Mwanza na Nansio? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta meli mpya sasa ikizingatiwa kuwa meli ya MV Clarius imechakaa sana?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru.
Katika Awamu ya Nne, Serikali ya Ujerumani ilileta maombi nchini mwetu kutaka kufanya ukarabati meli ya MV Liemba ambayo ipo toka Vita Kuu ya Kwanza kama sentiment value ya Serikali ile walitoa offer ya kuitengeneza na kui-refurbish na kuifanya i-comply na sea worthiness kwa asilimia mia moja lakini hawakupewa jibu sahihi.
Je, Serikali mko tayari kukaa nao tena ili sasa offer ile iweze kufanywa na meli ile iweze kutengenezwa na ili iweze kutoa huduma kwa uhakika kwa wananchi wa Ziwa Tanganyika?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kulikuwa na mpango na sasa hivi mpango huo upo, mimi mwenyewe kama mwezi mmoja uliopita nilikuwa na mazungumzo ya kina na Waziri wa Maendeleo wa Ujerumani, mpango huo upo na tunaendelea nao ili MV Liemba ambayo imedumu kwa muda mrefu iweze kufanya kazi kama inavyopaswa.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI (K. n. y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI) aliuliza:- Ni zaidi ya miaka mitano sasa tangu Meli ya MV Butiama isitishe huduma zake katika Ziwa Victoria kati ya Mwanza na Nansio (Ukerewe) hali inayosababisha shida na usumbufu mkubwa wa usafiri kwa wakazi wa Ukerewe. (a) Je, ni lini meli hiyo ya MV Butiama itatengenezwa na kuendelea kutoa huduma kati ya Mwanza na Nansio? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta meli mpya sasa ikizingatiwa kuwa meli ya MV Clarius imechakaa sana?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.
Kwa kuwa kulikuwa na mpango ambao ulisemekana kwamba Serikali ilikuwa inanunua meli tatu Korea Kusini na sasa hivi katika majibu ambayo yanatolewa na Serikali ni kama mpango ule umekufa kabisa.
Je, Serikali ituambie ina mpango gani kuhakikisha kwamba hizo meli ambazo zilikuwa zinunuliwe kutoka Korea Kusini zinanunuliwa na kupelekwa katika maziwa yote matatu?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mhimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa tulikuwa na mazungumzo na Serikali ya Korea na mimi nilikaa miezi miwili iliyopita nilizungumza na Balozi wa Korea na mazungumzo hayo bado yanaendelea, lakini itategemea hasa Exim Bank ya Korea itaamua vipi ndiyo tutaendelea na utaratibu huo.